Waislamu walipuka
·
Wachoma, wavunja makanisa,
wapora vifaa vya ibada
·
Wavamia polisi kumteka
aliyenajisi kitabu cha Kurani
·
Ilikuwa wamuue kwa
kumchinja mchana hadharani
Na Happiness Mnale
KUNDI kubwa la
waislamu wenye imani kali, jana lilizusha vurugu kubwa zilizoambatana na
kuchomwa moto na kuharibiwa kwa makanisa manne ya kikristo Jijini Dar es Salaam,
katika kile kilichoelezwa kuchukizwa na kitendo cha kijana mmoja wa kikristo
aliyedaiwa kukimwagia haja ndogo kitabu kitakatifu cha Kurani.
Waislamu hao waliokuwa
na jazba kubwa, walichukua hatua ya kufanya uharibifu huo, baada ya kushindwa
kwa jaribio la kukiteka kituo kidogo cha polisi cha Mbagala kwa nia ya
kumchukua kijana anayetuhumiwa kufanya tukio hilo Emanuel Josephat(14)ili
wamuue kwa kumchinja hadharani kama adhabu kwa kosa hilo.
Vikosi vya polisi
wenye silaha na mabomu ya machozi na maji ya kuwasha walipambana na waislamu
hao ambao walizidi kuongeza kila dakika, hivyo kufunga shughuli zozote za
kijamii katika barabara ya Kilwa, eneo lote la Mbagala.
Wakiwa na silaha za
mawe, kundi hilo lilivamia mitaani na kuchoma kanisa la Kiinjili la Kilutheri
Tanzania(KKKT)Mbagala Zakhem, na lile la Assembly of God (TAG), huku wengine
wakiharibu Kanisa la Anglican,kuvunja vioo katika kanisa la Wasabato, na kuchukua
vifaa vya muziki na ibada na kuviunguza hadharani.
Waislamu hao
waliyaponda mawe na kuyaharibu magari ya polisi namba T142 AVV,PT 0966 na T 325
BQP,basi la uda na gari la waandishi wa habari kutoka Clouds.
Jitihada za kamanda
wa polisi wa mkoa wa Polisi wa Temeke, David Misime kujaribu kuzuia kuenea kwa
ghasia hizo kwa kuwatumia viongozi wa kiislamu zilionekana kugonga mwamba
kutokana na viongozi hao kuwatetea waumini wao.
viongozi wa dini
hiyo akiwemo Sheikh wa Wilaya ya Temeke, Sheikh wa Taasisi na Jumuiya za
Waislamu kukaa kikao na kamanda wa Polisi Wilaya ya Temeke, David Misime,
walifikia muafaka wa kuwatuliza wasialamu hao lakini hali iliendelea kuwa
mbaya.
Chanzo cha vurugu
hizo, ni ubishani wa kitoto uliozuka baina ya mtoto Emmanuel na rafiki yake
Zakaria Hamis (12) anayesoma shule ya msingiChamazi siku ya jumatano wiki hii.
Inadaiwa kwamba
mtoto Zakaria alimwambia rafiki yake ambaye pia ni majirani, kwamba msahafu huo
ni mtakatifu na kwamba mtu yeyote ambaye angekiharibu kwa jambo lolote iwe ni
kukichana kwa makusudi, kukitemea mate ama kukikojolea angekufa pale pale, au
kugeuka mnyama.
Katika ubishi huo,
mtoto Emmanuel aliamua kukojolea msahafu huo, akitaka kuona kama kweli angekufa
ama kudhirika jambo ambalo halikumpendeza rafiki yake ambaye alikwenda
kuwaeleza wazazi wake.
Baba mzazi wa
Zakaria, aliwaambia waandishi wa habari kwamba, kutokana na tukio hilo
alilazimika kwenda kwa wazazi wa Emmanuel na kisha kwenda kwa mjumbe ambaye
aliwalekeza kwenda kituo cha polisi kuandikisha maelezo na kisha kushikiliwa
kwa muda.
Wazazi wote
walikubaliana kuyamaliza mambo hayo, kwa kumwonya mtoto huyo, lakini habari za
kuaminika zinasema kuwa baadhi ya viongozi wa kiislamu hasa msikiti wa Chamazi,
waling’aka na kutaka jambo hilo lifikishwe ngazi za juu za uongozi wa kiislamu.
Viongozi wa kikristo
Katika
hatua nyingine, viongozi wa kikristo walikataa kuzungumza jambo lolote kutokana
na vurugu hizo na kuchomwa kwa makanisa yao. Jitihada za kuwapata askofu wa
KKKT, Anglikani, TAG na Sabato hazikuweza kuwafanya wazungumze lolote hasa kila
mmoja kudai kwamba jambo hilo ni zito na lingetolewa maamuzi kamili kesho
jumamosi (leo)
Hadi tunakwenda
mitamboni zaidi ya waislamu 100 walikuwa wamekamatwa, huku vurugu ziliendelea kupinga kukamatwa kwa wenzao na jeshi la polisi,
licha ya kuombwa na viongozi wao kuwa watulivu kwa kuwa jambo hilo sasa
linashughulikiwa na mamlaka za juu.
No comments:
Post a Comment