Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

BURUDANI




Arusha watawala Ruaha Half Marathon 2012

Na Mwandishi Wetu, Iringa

WAKAZI wa mjini Iringa mwishoni mwa wiki walishuhudia kwa mara ya kwanza wanariadha zaidi ya 320 wakichuana katika mbio za barabarani za Ruaha Half Marathon huku wanariadha kutoka mkoani Arusha wakitawala.
Katika mbio hizo, zilizoanzia mnara wa saa karibu na ofisi za Manispaa ya Iringa na kuelekea njia ya kwenda Ruaha National Park na kurudi hadi uwanja wa Samora  ambako zilihitimishwa, kwa upande wanaume Alphonce Felix kutoka sekondari ya Winning Spirit alishika nafasi ya kwanza akitumia saa 1:03.09 huku kwa wanawake, Mary Naali kutoka klabu ya Skytel akishinda kwa saa 1:13.01.
Alphonce alifuatiwa na Dickson Marwa wa klabu ya Mbui ya jijini Dar es Salaam 1:03.29 huku nafasi ya tatu ikikamatwa na Saidi Makula wa Winnig Spirit 1:03:29 mshindi wa nne Getuni Tsekeway pia wa Arusha 1:04.06 wakati aliyefunga tano bora alikuwa ni mwenyeji, Moses Mwadeni aliyetumia saa 1:11:18.
Naali ambaye kwa muda huo kaweka rekodi kwa wanawake hapa nchini, alifuatiwa kwa mbali na Stephancy Perkins kutoka Australia aliyetumia saa 1:32.55, Natali Struble wa Marekani alishika nafasi ya tatu kwa saa 1:38.50 huku nafasi ya nne ikienda kwa Yoko Imamura wa Japan 1:59.00 wakati Mia Mjengwa wa Iringa alifunga tano bora akitumia saa 2:03.00.
Mbio hizo, ambazo zimepangwa kufanyika kila mwaka Jumamosi ya mwisho wa Mei, kwa mwaka huu wa kwanza zilishirikisha wanariadha chipukizi wengi kutoka Iringa na mikoa za jirani na baadhi wa kimataifa wa hapa nchini na kutoka nje.
Ruaha Half Marathon, iliratibiwa na kudhaminiwa na shirika lisilo la kiserikali
la Mindset Empowerment (ME), lenye makao yake makuu mjini Iringa, zikiwa na ujumbe wa kulinda na kuboresha mazingira, ambapo kauli mbiu yake ikiwa ni ‘Mazingira bora kwa utalii endelevu, okoa mto Ruaha’.



Lowassa apewa heshima
Tamasha la Upendo Radio

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa jimbo la Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, atakuwa mgeni wa heshima katika tamasha la kuhitimisha mpango wa kuchangisha fedha za kuiwezesha Upendo Redio FM ya jijini Dar es Salaam  kupanua usikivu wake.

Wakati Lowassa akipewa heshima hiyo kama muumini wa Kanisa la KKKT –Mashariki na Pwani na mwasisi  wa redio hiyo iliyoanzishwa mwaka 2004, Askofu wa Kanisa hilo, Dk. Alex Malasusa,  atakuwa mgeni rasmi.

Tamasha hilo la aina yake litakalopambwa na waimbaji mahiri kutoka ndani na nje ya Tanzania, litafanyika Mei 27 kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, likilenga kukusanya sh mil. 220 kusaidia upanuzi wa masafa ya redio hiyo.

Kwa mujibu wa mmoja wa wadau wa tamasha hilo, siku hiyo itakuwa ni hitimisho la tamasha hilo lililozinduliwa Februari 19 na Askofu Msaidizi wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani, George Fupe.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baada ya tamasha hilo kuzinduliwa siku hiyo kwenye kanisa la KKKT-Magomeni, michakato mbalimbali ya kulifanikisha iliendelea ikiwemo kugawa kadi za michango, ambayo itakabidhiwa siku hiyo.

Chanzo hicho kilidokeza kuwa, mkakati uliopo ni kuongeza usikivu wa redio hiyo kutoka mikoa mitano ya sasa hadi 12. Mikoa ambayo Upendo Radio inapatikana, ni Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Zanzibar na baadhi ya maeneo  ya mkoa wa Iringa na kuongeza kuwa kama mambo yatakwenda vizuri kupitia tamasha hilo, mikoa zaidi itafikiwa.

Kati ya waimbaji ambao watapamba tamasha hilo la aina yake, ni Faraja Ntaboba kutoka DR Congo, Sarah K  kutoka Kenya, Jennifer Mgendi, Jackson Benti na Joshua John Mlelwa wa Tanzania.

Aidha kwa wale ambao hadi sasa hawajapata kadi rasmi kupitia katika makanisa ya DMP, zitapatikana getini siku ya tamasha hilo, huku wito ukitolewa kwa wadau kujitokeza kwa wingi kufanikisha shughuli hiyo.
                                                                         Mwisho 




 Big brothe Stargame

Watatu wang’oka mjengoni

WASHIRIKI  watatu kati ya wane waliokua kwenye hatari ya kutoka kwenye shindano la Big Brother Stargame,  Luke, Yadel (Liberia) na Dalphin (Siera Lione)  waliondolowa ndani ya jumba hilo baada ya  kupata  moja moja  kila mmoja huku Zainab wa Siera Lione, alinyakua kura 13, kati ya kura 15 zilizopigwa..

Kwa hatua hiyo, Luke alimuacha mpwe mshiriki mwenzake, Jesica (Namibia) ambae alikua na mahusiano nae, awali washiriki hao waliweza kukaa kwa muda mrefu na kujadiliana ikiwemo mipango ya kuooana hapo baadae ambapo walipigana mabusu ya mwisho mwisho.
**

 ambae alikua na mahusiano na mshiriki mwenzake, Jesicca, akiponea tundu la sindano  baada yausiku wa kuamkia jana waliliaga jumba hilo kufuatia kupata kura chache za kuwawezesha kubaki ili kuwania kitita ha dola za kimarekani 300000.

Washiriki walioaga ndani ya jumba hilo ni  Luke, Yadel (Liberia) na Dalphin (Siera Lione) hata hivyo mbali ya kutolewa kwa washiriki hao ambao katika hatari ya kutoka wawilikua nne akiwemo Zainab (Siera Lione) yeye aliponea tundu la sindano na kuamishiwa kwenye jumba la Upville ambalo linakariwa na washiriki maalum kutoka nchi saba za afrika wakiwemo wasanii,wanamitindo na wacheza filamu nyota.

Hata hivyo, mshereheshaji wa shindano hilo, IK alipomwita jukwaani Zanab na kumweleza kua amebahatika kubakia ila  kwa jumba la Upville, alisshukuru huku akisema kua alipokua ndani ya jumba la Downville, wengi walimchukulia kama mkosaji ikiwemo vitendo vuya kugombana mara kwa mara ikiwemo na mshiriki mwenzake, Seydou (Angola).

Katika kura zilizopigwa Zainab alipata jumla ya kura, 13, Yadel na Luke, kila mmoja waliambulia kura moja moja huku Dalphin akiambulia patupu kwa kukosa kura hata mopja kati ya kura 15 zilizopigwa.

Mambo ndanio ya jumba hilo yanazidi kunoga kwa nyumba zote mbili, huku safari hii washiriki walio jumba la Upville ndio zamu yao ambapo wanatakiwa kuingizwa kwenye hatari ilikupigiwa kura. IK aligeukia kwa washiriki wa jumba hilo na kuwatangazia juu ya kujiandaa ambapo zoezi hilo la kuwapendekeza lilitarajia kuanza mapema jana.

Shindano hilo ambalo linarushwa moja kwa moja kila siku katika ving’amuzi vya Dstv  chaneli 198.



Small augua


MWIGIZAJI mkongwe wa vichekesho nchini Said Ngamba maarufu kwa jina la Mzee Small amelazwa katika hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam baada ya kuugua ghafla.

Mzee small anayesumbuliwa na maradhi ya shinikizo la damu kiasi cha kushindwa kuongea, aliugua ghafla juzi jioni muda mfupi baada ya kutoka Mwanza alikokwenda kwenye shughuli za kisanii.

Akizungumza na Tanzania Daima mwigizaji mwenzake Chausiku maarufu kwa jina la Bichau alisema kabla ya kuugua mzee small alikua mwenye afya njema hadi walipoachana kwenye uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) waliporejea kutoka Mwanza.

Kwa mujibu wa bi chau walikwenda Mwanza Ijumaa iliyopita kusherehesha shughuli ya walemavu wa ngozi iliyoandaliwa na Madaktari wa Hospitali ya Bugando jijini humo.

“Tuliondoka Dar es Salaam na ndege ya jioni Ijumaa tukalala Mwanza jumamosi tukafanyakazi iliyotupeleka ilikua ni shughuli ya walemavu wa ngozi pale Bugando hospitali iliandaliwa na madaktari wa chuo cha Bugando.

“Jumapili jioni tuliondoka Mwanza sasa kabla sijafika nyumbani kwangu Magomeni nikapokea simu kutoka kwa binti yake mzee small akanipa taarifa za ugonjwa… nilishtuka nikawaambia wampeleke hospitali,” alisema bi chau swahiba wa nguli huyo wa vichekesho.

  
Kwa upande wake mke wa mzee small alisema bado hali ya mumewe haijatengemaa hivyo kuomba dua za watanzania.


“Analo tatizo la presha na huwa anajikuna na kuvimba lakini safari hii amevimba shavu moja na kadri muda unavyokwenda hali yake inazidi kuwa mbaya,” alisema mke wa mzee small akiwa nyumbani kwake Tabata Kimanga kabla ya kumpeleka hospitali.

Katika maelezo yake mke wa mzee small alisema juzi usiku walimpeleka mumewe hospitali ya KLM iliyopo Tabata ambapo alipewa dawa ya kupunguza shinikizo la damu kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani.


Hata hivyo hali ya msanii huyo iliendelea kuwa mbaya hadi alipokimbizwa hospitalli ya amana jana mchana.

Mwisho…

No comments:

Post a Comment