WAZIRI wa
Nishati na Madini Profesa Sospeter
Muhongo amesema kuwa watu ambao wataingia mikataba mibovu katika
Wizara yake watafukuzwa kazi
pamoja na kushitakiwa kwa mujibu wa sheria.
Muhongo
aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Shirika
la Mafuta Tanzania (TPDC),alisema kuwa watu ambao wataingia mikataba mibovu
watashitakikwa pamoja na kufukuzwa ili
kuleta ufanisi wa kazi na usimamiaji
wa miradi.
Alisema kuwa kilio chake ni mikataba ambayo inatakiwa
kupitishwa kwa vigezo vilivyowekwa kwa maslahi ya
taifa na sio kuwafurahisha
wawekezaji ambao wanataka faida
nyingi huku taifa likishindwa
kunufaika na uwekezaji.
Muhongo
alisema kuwa kwa mtu yeyote ambaye
atahusika na fununu za rushwa
katika Wizara hii mtu huyo atafukuzwa kazi baada
ya kujiaminisha kutokana
na fununu katika
kujenga Tanzania iliyosalama.
Waziri
alisema kuwa bodi ambazo ziko katika wizara yake lazima zifanye
kazi kwa uhakika katika kusimamia mikataba ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kuwa ni mibovu.
Muhongo
alitataka bodi ya TPDC kupitia mikataba
yote ambayo imeombwa na ameibaini kuwa
na mapungufu hali ambayo inahitaji
kuangaliwa kwa umakini kwa
maslahi ya taifa katika mali ghafi ya
gesi na mafuta.
“Bodi isiwe
kama sehemu ya kujipatia posho na
wanaotaka posho na kushindwa kwenda na
kasi hii ni bora wajitoe ili kupata watu wengine ambao ni waadilifu katika kufanya kazi ya usahuri”.alisema
Profesa Muhongo
Alisema kuwa katika
mambo mengine ambayo ni mzigo
katika baadhi taasisi ni kuwa na kesi ambazo haziishi na kuwa mradi kwa
makampuni ya uwakili sasa zifike mwisho
katika kuokoa fedha za wananchi.
Muhongo
alisema makampuni ambayo yanashindwa
kufikia asilimia 8 yasipewe usimamiaji ili
kupewa watu wengine ambao wataweza kuendesha kesi hizo ambazo zinakuwa
mzigo na watu katika miradi.
Aliitaka bodi
bodi hiyo kutopokea mikataba minginea mpaka watakapokamilisha iliyopo ambayo baada ya
kupitia kulionekana kuna upungufu ambapo ni kazi ya bodi kushauri
serikali na kupata wawekezaji wenye sifa.
“Wawekezaji wamekuwa na kauli nyingi juu ya kuangalia masilahi yao hivyo ni bora kujiaminisha na vitu ambavyo wanataka
kuvifanya na si kukubali gesi ikatoka tutakwa hatujafanikiwa tunachotaka”.alisema
Profesa Muhongo
Alisema kuwa lazima shirika liwe na miradi ya gesi na
mafuta ili kuzuia mchezo wa
wafanyabiashara ambao wanaweza kusema mafuta
yameadimika ili kupandisha bei ya mafuta.
mmmmmmmmmmmmmmmmmm
SHIRIKISHO la Vyama
vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limeshangazwa
na kitendo kilichofanywa na madaktari wanaofanya kazi chini ya usimamizi wa madaktari bingwa
(interns), na kusema kuwa hatua waliochukua inaweza kuleta vurugu ndani ya
nchi.
Madaktari wanaofanya kazi chini ya
usimamizi wa madaktari bingwa (interns), ambao walisimamishwa wakati wa mgomo
wa madaktari juzi walijitokeza na kuomba radhi kwa wananchi na serikali kwa
kushiriki migomo na kusababisha madhara makubwa kwa baadhi ya wananchi.
Madaktari hao ambao walikusanya
saini zaidi ya 200 kutoka kwa wenzao, walienda mbali zaidi na kuapa kwamba
hawako tayari kushiriki tena kwa namna yoyote katika migomo inayoweka rehani
maisha ya wananchi.
Akizungumza na Tanzania Daima
Jumatano, Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholaus Mgaya, alisema kuwa, hatua
iliyochukuliwa na madaktari hao ni cha kushangaza kwa kuwa bado madai
waliyokuwa wakihitaji yameshindwa kutekelezwa jambo linaloweza kuchangia kuwepo
kwa vurugu.
Mgaya, alisema kuwa Tucta alielewi
ni kitu gani kimewasibu madaktari hao hadi kufikia hatua ya kuomba radhi.
Alisema kuwa inawezekana madaktari
hao sio wanachama wa vyama vya wafanyakazi hivyo wameshindwa kujua sheria za
kuitisha kwa mgomo.
“Sasa inatupa mashaka juu ya mgomo
wao…maana hawajapata walichogomea wanaanza kuomba radhi hapa ni lazima ‘system’
imefanyakazi yake na inawezekana kulikuwa na mamluki wengi katika mgomo ule,”
alisema.
Katibu Mkuu huyo, alisema kuwa
Tucta imejipanga kukutana na viongozi wa madaktari hao ili kuweza kuwaelewesha
maana ya mgomo na kuacha kutoa matamko yasiyo kuwa na tija.
Alisema madaktari hao wakiingia
katika vyama vya Wanyakazi wataweza kujua sheria za kuitisha mgomo na
kuhakikisha wanasimamia na kupata kile walichokuwa wanakihitaji kuliko
wanavyofanya sasa.
“Hawa waliotoa tamko hilo inaelekea hawapo
katika chama cha wafanyakazi, hivyo wakiingia katika vyama wataacha kutoa
matamko ya aina hiyo maana wanaonekana hawaelewi na wanajifunza,” alisema
Hata hivyo Mgaya alisema kuwa inaonyesha
madaktari hao kama wametishwa na kulazimika kutoa tamko hilo.
“Hapa kuna jambo limefanyika kwa kuwa hata Dk
Steven Ulimboka hatumsikii tena, lazima kuna kitu kinafanyika lakini hatua
waliyoifanya watapata hasara zaidi kwani hawawezi kukutana tena na serikali
…kwa kifupi wamekalia kuti kavu,” alisema
Mwisho
-->
Mwili wa Mhashamu Askofu William Paskali Kikoti wa Jimbo la Mpanda, aliyefariki Agosti 28 2012 katika Hospitali ya Rufaa Bugando kwa shinikizo la damu, utazikwa kesho katika Kanisa Kuu la Mt Imakulata jimboni humo. MIsa ya mazishi itaanza saa 4:00 asubuhi
Misa ya kumwombea na kuaga mwili wa Marehemu kule Mwanza ilifanyika janakatika Kanisa Kuu la Epifania kuanzia saa 6:00 Mchana na mara baada ya Misa mwili wa Marehemu Askofu Kikoti ulisafirishwa kwa ndege kwenda Jimboni Mpanda jana 30 Agosti 2012 saa 8:00 mchana.
Marehemu Askofu Paskal Kikoti alizaliwa tarehe 3 Mwezi Machi 1957 katika kijiji cha Ihambo, Parokia ya Nyabula Jimbo katoliki la Iringa.
Alipata elimu ya msingi huko Ihimbo kuanzia mwaka 1967 hadi 1973.
Alisoma masomo ya Sekondari kidato cha Kwanza hadi cha Nne katika Seminari ya Mafinga kuanzia mwaka 1974 hadi 1977 na akaendelea na maomo ya kidato cha Tano na cha Sita katika Seminari ya Nyegezi Mwanza kuanzia mwaka 1978 hadi 1980.
Marehemu Askofu Kikoti alijiunga na jeshi la Kujenga Taifa katika Kambi ya Makutupora kuanzia mwaka 1980 hadi 1981.
Mwaka 1982 hadi 1983 alisoma Elimu ya Falsafa katika Seminari Kuu ya Ntungamo na baadaye akjiunga na Seminari Kuu ya Kipalapala kwa Masomo ya TaaliMungu (Theolojia) kuanzia mwaka 1983 hadi 1988 .
Alipata daraja la Upadri tarehe 29 Mwezi Juni 1988.
RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA, NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE, APUMZIKE KWA AMANI- AMINA
Madaktari: Kuna kikosi cha kumuua
Ulimboka
*Wadai kutishiwa maisha, waomba
ulinzi UN
*Wasema Ulimboka alimtambua afisa
aliyemteka
Na Irene Mark
BAADA ya kutekwa, kupigwa na kutelekezwa kwa Mwenyekiti wa
Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, viongozi wa vyama vya
madaktari wamedai maisha yao
yako hatari hali iliyowalazimu kuomba ulinzi Umoja wa Mataifa na makundi
mbalimbali ya kutetea haki za binadamu.
Madaktari hao wamesema hawana imani na maofisa wa serikali
ya Rais Jakaya Kikwete, wanaotishia usalama wa maisha yao kwa namna tofauti hasa baada ya tukio la
Dk. Ulimboka la Juni 27 mwaka huu.
Barua ya madaktari hao kwenda kwa Mwakilishi Mkazi wa Umoja
wa Mataifa hapa nchini ya Julai 7, 2012, madaktari wameeleza namna maofisa wa
serikali wanavyotishia usalama wa maisha yao
hao na kuwaeleza namna walivyowatuma wenzao Afrika Kusini kuhakikisha Dk.
Ulimboka anapoteza maisha.
Pia barua hiyo yenye kumb. Na.MAT/UN/SU/01, imetumwa kwa
Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi,
Shirika la Human Rights Watch na Amnesty International.
Taasisi nyingine zilizopelekewa nakala ya barua hiyo ambayo
Tanzania Daima ina nakala yake ni Kituo cha Haki za Binaadam (LHRC), SIKIKA
Tanzania, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Chama cha Waandishi wa Habari
Wanawake (TAMWA).
“Hata hivyo, watu kutoka serikalini waliihakikishia MAT
kwamba timu ya wasaidizi wao imeenda Afrika Kusini kuhakikisha Dk. Ulimboka
anarudi nyumbani akiwa maiti.
“Kwa kuongezea hapo, viongozi wa MAT tunapokea vitisho kwa
njia ya ujumbe mfupi wa maandishi kwenye simu na wakati mwingine tunapigiwa
simu na namba zisizopatikana tukitishiwa maisha,” ilieleza sehemu ya barua hiyo
iliyosainiwa na Dk. Mkopi.
Aidha, barua hiyo imeuomba Umoja wa Mataifa kuwahakikishia
madaktari usalama wa Dk. Ulimboka kwenye hospitali anayotibiwa na kuwalinda
madaktari wengine hasa viongozi wa vyama na jumuiya ya madaktari.
Kadhalika barua hiyo imeuomba umoja huo kuushauri mfumo wa
sheria za Tanzania
kutokubali kutumika kwa faida za kisiasa na kulitaka Bunge kubaki na majukumu
yake ya Kikatiba ya kuiwajibisha serikali kwa vifo vya watu kama
matokeo ya mgomo unaoendelea.
Katika barua hiyo madaktari hao wameeleza namna Dk. Ulimboka
alivyoteswa na watekaji hao kwa kung’olewa kucha, meno na kuumizwa sehemu
mbalimbali za mwili wake huku akimtambua ACP Msangi kuwa miongoni mwa watekaji
hao.
Walieleza namna polisi wa kituo cha Bunju walivyoshindwa
kuwapa ushirikiano kwa haraka ili kumuwahisha majeruhi huyo kwenye Hospitali ya
Taifa Muhimbili na jinsi walivyokuwa wakizuiwa na magari ya askari kwa lengo la
kumchelewesha asipate huduma za kitabibu.
“Akiwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi Kitengo cha
Mifupa Muhimbili (MOI), Dk. Ulimboka licha ya maumivu makali aliyokuwa nayo
alimtambua ACP Msangi kuwa ni miongoni mwa waliomteka na kumtesa,” ilieleza
sehemu ya taarifa hiyo na kubainisha kwamba ACP Msangi ni kiongozi wa tume
iliyoundwa kuchunguza suala hilo .
Ikulu yasononesha viongozi wa dini
Baadhi ya viongozi wa dini waliojitolea kusuluhisha mgogoro
baina ya madaktari na serikali, wameeleza kusononeshwa na jibu la Ikulu la
kukataa kuonana nao huku wakibainisha kwamba jukumu lao kubwa ni kuhakikisha
amani inatawala.
Akizungumza kwa niaba ya viongozi hao, Msemaji wa Kamati ya
Vijana wa Baraza Kuu la Waislamu (Bakwata), Said Mwaipopo, alisema licha ya
jibu hilo
wanaendeleza juhudi za kuhakikisha mgogoro huo unamalizika kwa njia za amani.
“Hatukatishwi tamaa na jibu la Ikulu kazi yetu kubwa ni
kuhakikisha amani inakuwepo… ndiyo maana jana tulikutana na viongozi wa
madaktari tukawaeleza kwamba njia bora ya kufanya ni kuandika barua na kuieleza
jamii kupitia vyombo vya habari kwamba wanaomba msamaha kwa Rais, wananchi na
serikali.
“Kitu kinachotusikitisha vijana wale walikataa ushauri wetu
tukagundua kwamba inawezekana nyuma yao
kuna siasa zinaingia,” alisema Mwaipopo.
Akijibu suala hilo
Katibu wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Edwin Chitage, alikiri kukutana na viongozi
hao jana na kueleza kwamba walichokubaliana ni kusubiri barua rasmi kutoka
Ikulu ikiwataka madaktari hao kuandika barua kuomba msamaha kwa Rais,
Watanzania na serikali.
“Ni kweli lakini alichokisema Mwaipopo ni kwamba alipigiwa
simu na watu waliodai kwamba wako Ikulu, hivyo wakawaambia viongozi hao wa dini
watuambie madaktari tuandike barua ya kuomba msamaha.Tunaomba msamaha kwa
nini,” alihoji.
Dk. Mkopi aliongeza kuwa madai yao
hayajatekelezwa licha ya kuwepo kwa muda mrefu tangu mwaka 2005 na kwamba kama serikali haina dhamira ya kweli ya kumaliza mgogoro
huo utaendelea hata baada ya miaka 10.
Kukutana na Dk.
Mwinyi
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Dk. Godbless Chale
alisema walipokea simu kutoka kwa Waziri mpya ya Afya na Ustawi wa Jamii Dk.
Hussein Mwinyi ikiwataka kwenda kumweleza sababu za mgomo wao.
“Kweli Dk. Mwinyi alitupigia simu akatuita alisema hajui
madai yetu hivyo twende tukamweleze hivi kwa akili ya kawaida kweli ofisi
inakosa nyaraka za kumbukumbu?!! Tunaona hayupo ‘serious’.
“Kabla hajatuita
wizara yake iliteua wajumbe watatu Naibu Katibu Mkuu, Naibu Mganga Mkuu Dk.
Donald Mbando na Mkurugenzi wa Rasilimali tukaketi nao kuwaeleza siku chache
baadaye waziri anasema hajui madai yetu hii tumeona ni ‘kamchezo’ wanataka
kutufanyia,” alisema Dk. Godbless.
Mwisho
Dk. Slaa, Mnyika, Lema wabanwa
*Nchimbi awaagiza polisi kuwahoji
*Adai Chadema ni wazee wa tuhuma
Na Salehe Mohamed, Dodoma
SIKU moja baada ya
viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kudai kimebaini
mikakati ya makusudi ya usalama wa taifa kutaka kuwadhuru baadhi ya viongozi
wake, Waziri wa Mambo ya Ndani, Emanuel Nchimbi, ameliagiza Jeshi la Polisi
liwahoji.
Akizungumza na waandishi
wa habari jana mjini hapa, Waziri Nchimbi alisema licha ya jeshi la polisi
kusita kuwahoji viongozi hao kwa madai ya kutoaminika, lakini sasa ameliagiza
liwahoji na kuzifanyia uchunguzi tuhuma zao.
Alisema kama tuhuma hizo
zitathibika si za kweli watachukuliwa hatua kulingana na sheria za nchi.
Juzi, Chadema kupitia kwa
Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ilieleza kubaini mkakati wa makusudi wa
kuwadhuru viongozi wakuu wa chama hicho, na kudai kuwa mpango unaratibiwa na
baadhi ya vigogo katika idara ya usalama wa taifa, kwa lengo la kudhoofisha
harakati za kufichua ufisadi na kudhoofisha serikali na chama kinachotawala.
Viongozi wanaolengwa
katika mkakati huo ni Katibu Mkuu Dk. Willibrod Slaa, Mbunge wa Ubungo John
Mnyika na Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbles Lema.
Freeman Mbowe, alisema
taarifa za uhakika zilizoangukia mikononi mwa intelijensia ya chama hicho
zinathibitisha dhamira ya vigogo hao kuwadhuru viongozi wao na kuwataka
wananchi wasisite kupigania haki yao , hata kama dhamira hiyo chafu itafanikiwa.
Alisema mpango huo
unaratibiwa na mmoja wa viongozi wa juu kutoka Idara ya Usalama wa Taifa (jina
linahifadhiwa). Vile vile, alimtaja mmoja wa watu wanaofuatilia nyendo za
Mnyika na kwamba mkakati wa kwanza wa kumdhuru mbunge huyo ni kumuwekea sumu au
kuvamiwa na watu watakaodhaniwa kuwa ni majambazi.
Hata hivyo katika hilo , Nchimbi alisema
viongozi wa Chadema kwa muda mrefu wamekuwa na tabia ya kuvichonganisha vyombo
vya dola na wananchi ili visiaminike.
Alisema suala la
kuwalinda raia limesemwa kwenye Katiba na sheria kuwa ni jukumu la jeshi la
polisi, hivyo mtu yeyote anayesema hana imani na jeshi hilo ana matatizo.
Alibainisha kuwa ingawa
viongozi wa polisi walimuambia hawawezi kuwahoji viongozi wa Chadema waliosema
hawana imani na jeshi hilo ,
amewaagiza wahojiwe bila kujali walichokisema.
“Ninyi Chadema …wazee wa
tuhuma kwa miaka minne mmekuwa mkitoa tuhuma kwa JWTZ, polisi na usalama wa taifa,
sasa tukiwachagua kuongoza nchi itakuwaje?” aliuliza Nchimbi.
Alisema iwapo itatokea
siku moja jeshi la polisi likatangaza kupumzika kwa muda wa saa nne bila
kukamata wala kuhoji jambo lolote nchi itakuwa kwenye hali mbaya hivyo ni vema
wanasiasa wakajiepusha na kauli zenye lengo la kubomoa.
“Hawa viongozi wa Chadema
wanajitafutia umaarufu wa kisiasa, wao wanajua sehemu za kupeleka taarifa zao
na zinavyofanyiwa kazi, sasa kwa nini wanatumia njia zisizostahili?” alihoji.
Nchimbi aliongeza kuwa
Chadema imeshajenga tabia ya kuvituhumu vyombo vya dola na imeshafanya hivyo
kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ), usalama wa taifa na sasa polisi.
Alibainisha kuwa tabia
hiyo inaonyesha namna viongozi wa chama hicho wasivyo makini katika kupigania
matatizo ya wananchi na kugeuka kuwa walalamikaji wa mambo yao binafsi.
Nchimbi pia alitumia
fursa hiyo kukemea tabia ya viongozi wa kisiasa kuvishutumu vyombo vya dola
hadharani bila kufikisha malalamiko yao
ndani ya utaratibu unaostahili na kusema kuwa unavivunja moyo.
Waziri huyo alisema
serikali haifanyi kazi kwa fitna, visasi au majungu kwani kama
ingekuwa inafanya hivyo ingewakamata viongozi wa Chadema waliokuwa wakihusishwa
na kifo cha kada mwenzao marehemu Chacha Wangwe.
Alisema pamoja na
viongozi wa Chadema kutajwa sana
kwenye ajali hiyo serikali iliyapuuza madai hayo na dereva wa marehemu Wangwe
alifikishwa mahakani na kushtakiwa.
“Tutafute majukwaa ya
kunufaika kisiasa kwa njia zilizo bora si hili linalofanywa na Chadema,
wanachokifanya ni kulibomoa taifa badala ya kulijenga.
Nchimbi aliwataka
wananchi na wanasiasa waondoe hofu
iliyoanza kujengwa kuwa polisi haiaminiki na badala yake washirikiane na jeshi hilo kikamilifu.
Madaktari bingwawamjibu Kikwete
- Sasa
waitaka serikali iwatimue na wao pia
- Waliofukuzwa
wasema Rais amepotoshwa
- Bunge
lachafuka kupigwa kwa Ulimboka
Na waandishi wetu, Dodoma , Dar
AGIZO la Rais Jakaya
Kikwete kuwataka madaktari wanaoendelea na mgomo kua chakazi limechukua sura
mpya baada ya madaktari bingwa ambao awali hawakuhusika kabisa na mgomo huo,
kutoa tamko wakimtaka kiongozi huyo wa nchi kuwatimua wao kwanza kabla ya wale
wa ngazi ya chini.
Badala yake, Madaktari
bingwa ambao walitangaza kujiunga na wenzao juzi, baada ya kupigwa na
kujeruhiwa vibaya kwa Dk Steven Ulimboka, walisema wataendelea na mgomo wao hadi
hapo serikali itakapowarejesha kazini madaktari na madaktari wanafunzi wote
waliofukuzwa .
Akitoa tamko la madaktari
bingwa waliokutana kwa dharura jana na kamati ya jumuiya ya madaktari kujadili
hotuba ya rais Kikwete, kiongozi wa mabingwa hao Dk. Catherine Mng’ong’o
alisema huo ni msimamo wa madaktari wenzake, huku akitaka kufunguliwa kwa meza
ya majadiliano ya dhati yenye nia ya kumaliza mgogoro wao.
“Madaktari bingwa
hatuwezi kuyfanyakazi bila madaktari wa chini yetu… kama
serikali imedhamiria kuwafukuza kazi hawa na interns (waliopo kwenye mafunzo ya
vitendo) ianze na sisi.
“Tupo tayari kufukuzwa
iwapo madai yetu ya msingi hayatatekelezwa na kama
kuondoka waanze kutufukuza sisi kwanza,” alisema Dk. Mng’ong’o baada ya
kumalizika kwa kikao cha madaktari bingwa kilichoketi kwa zaidi ya saa tano
kwenye viunga vya hospitali hiyo.
Alisema hata wao hawana
sababu ya kuendelea kufanyakazi katika mazingira magumu na kuwaona watanzania
wakifa kwa kukosa vifaatiba na dawa.
Dk. M’ong’o alisema
madaktari hapa nchini wamefanyakazi katika mazingira magumu kwa muda mrefu
hivyo wakati wa kubadili hali hiyo umefika na kuwasaidia watanzania maskini
wanaotibiwa kwenye hospitali hizo.
Jumuiya yasema JK kadanganywa
Kwa upande wao viongozi
wa Jumuiya ya Madaktari nchini wameelezea masikitiko yao , ya namna
Rais Kikwete alivyopewa taarifa za uongo na wasaidizi wake.
Akizungumza na waandishi
wa habari nje ya jengo la watoto kwenye hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)
Katibu wa Jumuiya hiyo Dk. Edwin Chitage alisema wapo tayari kumweleza ukweli
rais kwa kuwa wasaidizi wake wameshindwa kufanya hivyo.
“Rais hajapata taarifa
sahihi… tupo tayari kumweleza ukweli kwa sababu wasaidizi wake wanamdanganya,
tunasikitika kuona watanzania wakidanganywa.
“Wanaelezwa hoja dhaifu
za kuonyesha kwamba madaktari hatuna uzalendo wakati madai yetu pia ni kwa
maslahi ya wagonjwa wote hasa pale tunapodai mazingira bora ya kazi.
Katibu huyo alisema moja
ya madai yao
yalikuwa kuomba kila hospitali ya wilaya ipate mashine moja ya X-ray kwa vile,
haiwezekani nchi nzima kukosa mashine ya CT-Scan wakati bei yake ni sawa na
gari aina ya shangingi moja la kiongozi wa serikali,” alisema Dk. Chitage.
Katibu huyo alikiri
kwamba posho ni sehemu ya madai yao
huku akisisitiza kwamba hawang’ang’ani nyongeza hiyo badala yake kuwepo kwanza
na mazingira bora ya kazi ili kutoa tiba sahihi kwa mgonjwa.
Dk. Chitage alisema
hawapendi kubishana na mamlaka ya rais huku akisisitiza uwezo wa kumaliza hili
ni Kikwete kukaa nao meza moja kwa ajili ya kuzungumza badala ya kutoa vitisho.
Waomba kukutana na Rais
Madaktari hao walisema
kuwa sasa wanaomba kukutana na rais ili kujadili hatima ya mfomo huo.
“Tunamheshimu rais na
mamlaka zote ila tunachoamini ni kuwepo kwa meza huru ya majadiliano kati yetu
na yeye kwa sababu nafasi ya kumaliza kero hii anayo,” alisema.
Naye Makamu Mwenyekiti wa
jumuiya hiyo Dk. Godbless Charles alihoji sababu za kuwepo kwa taarifa tofauti
kuhusu ongezeko la mishahara wakati waliishauri serikali kuwa wazi kuhusu
nyongeza hiyo.
“Kumekua na majibu
tofauti mfano Waziri wa Afya na UStawi wa Jamii aliliambia Bunge kwamba
nyongeza ya mishahara ni asilimia 15. Hotuba ya rais Kikwete inasema nyongeza
hiyo ni asilimia 20 wakati ripoti ya wataalam iliyokutana na kamati ya Waziri
Mkuu ilipendekeza asilimia 25 je, nia ya serikali iko wapi?
“Wakati viongozi wa
serikali wakitoa taarifa zinazotofautiana ripoti ya ufafanuzi wa madai na hoja
za madaktari iliyotokana na majadiliano ambapo tulikua wajumbe hatukutoa
pendekezo lolote juu ya ongezeko la mshahara,” alisema Dk. Godbless.
Alisema tangu kuanza kwa
mgogoro kati ya madaktari na serikali jumla ya vikao sita viliketi kati ya
hivyo vikao vinne vilijadili juu ya uboreshaji wa huduma za afya kwa
watanzania.
“Ni masikitiko yetu kuwa
ripoti ya ufafanuzi wa hoja na madai yetu iliyotolewa Juni 31 mwaka huu,
taarifa ya waziri wa afya, taarifa ya waziri mkuu ndani ya Bunge na hotuba ya
rais haikuzungumzia kwa jinsi gani serikali itaboresha huduma za afya kwa
watanzania,” alisisitiza Dk. Godbless.
Katika hotuba yake kwa
wananchi rais Kikwete aliwataka madaktari wote waliogoma kuchakazi kwa kuwa
viwango vikubwa vya mishahara wanaoyitaka serikali haiwezi kuilipa.
Kipigo cha Dk. Ulimboka
Akizungumzia kutekwa,
kupigwa na kutelekezwa kwenye msitu wa Pande alikofanyiwa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Madaktari Tanzania Dk. Steven Ulimboka alisema wameshtushwa na kauli ya rais
Kikwete.
Kwa mujibu wa Dk. Godbless
kauli ya rais Kikwete kwamba serikali yake haihusiki na kitendo hicho
kimeingilia uhuru wa tume hiyo ambayo tangu awali madaktari na wanaharakati
waliipinga.
“Tume imeundwa kuchunguza
suala hilo na
mpaka sasa hakuna mwenye uwezo wa kudhibitisha kwamba serikali inahusika… je ni
sahihi kwa rais kutangaza waziwazi kwamba serikali yake haihusiki?
“Kauli hiyo haitoi uhuru
kwa tume kueleza ukweli wa tukio kwa sababu tume hiyo imeundwa na serikali
yenyewe,” alisema makamu mwenyekiti huyo na kuongeza kwamba madaktari hawana
imani na tume hiyo.
Awali alisema madaktari
wanahasira kwa kitendo cha kinyama alichofanyiwa mwenzao hali inayowafanya
waishi kwa hofu huku wengine wakiandika barua za kuacha kazi na wengine
wakiendeleza mgomo.
Bunge lachafuka, kupigwa Ulimboka
Katika
hatua isiyokuwa ya kawaida, hali ndani ya bunge jana jioni ilichafuka, baada ya
mwenyekiti wa bunge, kushishwa kabisa kuongoza kikao hicho kufuatia kuzuka kwa
malumbano makali baada ya Mkuu wa mkoa wa Iringa, Stella Manyanya kukituhumu
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuwa vinara wa mgomo wa madaktari.
Manyanya
alisema kuwa, chadema wamebainika kuchochea mgogoro huo, hali iliyomfanya
Mbunge wa Ubungo kusimama na kuomba mwongozo akimtaka Manyanya kuthibitisha ama
kukanusha tuhuma hizo.
Lakini
katika hali ya kushangaza, Mbunge wa Iramba mashariki Mwigulu Mchemba alisimama
na kunukuu hotuba ya kambi ya upinzani, ambayo ilitamka bayana kuwa inaunga
mkono madai ya watumishi wa serikali, na kwamba kwa kauli hiyo inadhihirisha
bayana kuwa ndio wakuu wa mgomo huo.
Badala
ya kutoa mwongozo, Mabumba hakumtaka Manyanya kukanusha ama kuthibitisha tuhuma
hizo nzito, badala yake alimruhusu Mchemba kuendelea kurusha makombora mazito
dhidi ya Chadema, safari hii akidai kuwa ni vimbelembele kutoa matamshi ya
kulaani kupigwa kwa Ulimboka huku, wakimwacha mmoja wa viongozi wake bila
kumhudumia wala kumjulia hali.
Katika
kujichanganya kwa wabunge hao wa CCM, wakati Mchemba akidai kuwa Chadema ndio
wachocheaji wakubwa wa mgogoro huo kwa kuwatumia madaktari, mwenzake Manyanya
alitoa hoja asafari hii akidai kuwa, ndio waliohusika na tukio la kumvamia na
kumteka na kisha kumpiga Dk Ulimboka.
Hata
pale Mnyika aliposimama na kuomba tena mwongozo wa mwenyekiti, huku akiweka
bayana jinsi inavyoelezwa ushiriki wa maafisa wa polisi, na hata Dk Ulimboka
mwenyewe kuwataja wengine kwa majina, alimtaka mchangiaji kuthibitisha ushiriki
wa Chadema kumjeruhi ama sivyo afute kauli yake.
Lakini
kwa mara nyingine tena, Mabumba hakumtaka Manyanya wala Mchemba kuthibitisha kauli
ama kufuta kama inavyofanywa kwa wabunge wa
upinzani, badala yake alimruhusu mkuu huyo wa mkoa wa Iringa kuendelea na
mchango wake bila kufuta kauli wala kuithibitisha.
Kushindwa
huko kwa waziwazi kwa Mwwenyekiti wa kikao hicho cha bunge, kuliwachefua
wabunge wengi wa upinzani, huku wale wa CCM wakionekana kufurahia jambo hilo .
Vigogo wa Jeshi kortini
Na Happiness Katabazi
MKURUGENZI wa Shirika Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) Kanali
Ayoub Mwakang’ata na maofisa wenzake sita wa jeshi hilo jana walifikishwa
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam wakikabiliwa na mashitaka
saba ya kula njama na matumizi mabaya ya madaraka.
Mbali na Kanali Mwakang’ta washitakiwa wengine ni Luteni kanali
Mkohi Kichogo,Luteni Kanali Paul Mayavi, Meja Peter Lushika,
Sajenti John lazier,Meja Yohana Nyichi na Mkurugenzi wa Miradi ya
Matrekta wa SUMA JKT-Luteni Kanali Felex Samillan.
Mawakili toka ofisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa(TAKUKURU),
Dominsian Kessy na Ben Lincoln walidai mbele ya Hakimu Mkazi Alocye Katemana
katika kosa la kwanza maafisa hao wote wanashitakiwa kwa matumizi mabaya ya
madaraka kinyume na kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
ya mwaka 2007.
Wakili Kessy alidai kuwa Machi 5 mwaka 2009 katika chumba cha
mikutano cha ofisi ya SUMA JKT Dar es salaam,wakiwa ni wajumbe wa
bodi na Bodi ya Tenda ya SUMA JKT kwa makusudi walitumia madaraka yao
vibaya kwa kutoa maamuzi ya bodi hiyo ambayo yalionesha yametolewa na
TAKOPA kwa madhumuni ya kununua magari na vifaa vya ujenzi bila
kupata idhini ya Bodi ya ya Wakurugenzi ya TAKOPA.
Wakili Kessy alidai kosa la pili pia ni la matumizi mabaya ya
madaraka ambalo linawakabiliwa washitakiwa wote kuwa Machi 12 mwaka 2012
,washitakiwa hao wakiwa ni wajumbe wa bodi ya Tenda ya SUMA JKT walitumia
madaraka yao vibaya kupitishia maazimio ya kununuliwa kwa magari na vifaa
vya ujenzi ambavyo vilikuwa vimeishatumika kinyume na kifungu cha 58( 3)
cha Sheria ya Mamunuzi ya Umma ya mwaka 2005.
Aidha shitaka la tatu ni la matumizi mabaya ya madaraka linalomkabili
mshitakiwa wa pili na wa saba (Kichogo, Samillan) ambapo Machi 16 mwaka
2009 wakiwa wajumbe wa bodi ya Tenda ya SUMA JKT wanadaiwa
kuhamisha Sh Bilioni 2,744,432,545 kupitia hundi Na.000010 kutoka
akaunti ya TAKOPA Na.011103031753 kwa SUMA JKT akaunti
Na.01110307094 ambazo zote zipo Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) kufuata
matakwa ya kifungu cha 156 cha Sheria ya Fedha ya Umma na Kanuni zake ya
mwaka 2001.
Shitaka la nne alidai linalowakabili washitakiwa wa pili na
watatu ambalo pia ni la matumuzi mabaya ya madaraka wanalodaiwa kulitenda
Aprili 3 mwaka 2009,wakiwa wajumbe wa bodi hiyo ambapo walihamisha
sh milioni 489,677,879.30 kupitia hundi Na.000011 kutoka TAKOPA akaunti
Na.011103031763 kwa akaunti Na. 011103017094 ya SUMA JKT bila kufuata
kanuni na matakwa ya kifungu cha 156 cha Sheria ya Fedha za Umma ya mwaka
2001.
Shitaka la tano ambalo linawakabili tena washitakiwa hao wawili ni
matumizi mabaya ya madaraka ambapo inadaiwa Aprili 4 mwaka 2009 wakiwa ni
wajumbe wa bodi hiyo walihamisha Sh milioni 269,519,093.60 kupitia
hundi Na.000012 kutoka akaunti ya TAKOPA Na.011103031753 kwa SUMA
JKT akaunti Na.011103017094 bila kuzingatia masharti ya kifungu cha 156 cha
Sheria ya Fedha za umma na kanuni zake ya mwaka 2001.
Katika shitaka la sita linlowakabili washitakiwa hao wawili tena pia
ni la matumizi mabaya ya madaraka ambapo Mei 4 mwaka 2009 wakiwa ni
wajumbe wa bodi hiyo,walihamisha shilingi 350,000,000,000 kupitia hundi
Na.000015 kutoka akaunti ya TAKOPA Na.011103031753 kwa SUMA JKT akaunti Na.
011103017094 bila kufuata matakwa ya kifungu hicho cha sheria ya Fedha za
umma.
Hata hivyo alidai shitaka la saba linawakabili washitakiwa wote
ambalo ni la kula njama kinyume na kifungu cha 32 cha Sheria ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007, ikidaiwa kuwa kati ya Machi na Mei mwaka
2009 wakiwa wajumbe wa bodi hiyo jijini Dar es Salaam, walikula njama na
kuamisha mradi kutoka akaunti ya TAKOPA Na. 011103017094 bila kufuata
matakwa ya kifungu cha 156 cha Sheria ya Fedha ya umma na kanuni zake ya mwaka
2001.
Hata hivyo washitakiwa wote walikana na Hakimu Katema
aliwaachia kwa dhamana baada ya kila mmoja kutimiza masharti ya kuwa na
wadhamini wawili wa kuaminika ambao watasaini bondi ya sh milioni 25 kila
mmoja. Kesi imeahirishwa hadi Agosti Mosi huu, itakapotajwa tena.
Na Mwandishi Wetu,
ATHARI za wabunge walioteuliwa kuwa mikoa na wakuu wa wilaya, zimeanza kuonekana Bungeni jana baada ya kuzuiwa kuuliza maswali kwa madai kuwa ni sehemu ya Serikali.
Wabunge
waliokumbwa na kisanga hicho ni Martha Umbulla ambaye kwa sasa ni mkuu wa
wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara na mkuu wa Wilaya ya Muheza mkoani Tanga,
Subira Mgalu.
Mwenyekiti
wa Bunge, Jenister Mhagama ambaye pia ni Mbunge wa Peramiho, aliwazuia wabunge
hao wakati waliposimama kutaka kuuliza swali.
Mhagama
alilazimika kusimama na kutumia kanuni ya kudumu ya Bunge ya 2(2) ambayo
inasema “iwapo jambo au shughuli yoyote haikuwekewa masharti katika kanuni
hizi, Spika ataamua utaratibu wa kufuata katika jambo au
shughuli hiyo.
shughuli hiyo.
“Kwa
kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni
nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya maspika wa bunge pamoja na mila na desturi za uendeshaji bora wa shughuli za bunge na uamuzi huo utaingizwa katika kitabu cha Maamuzi ili kuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa shughuli za bunge.”
nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya maspika wa bunge pamoja na mila na desturi za uendeshaji bora wa shughuli za bunge na uamuzi huo utaingizwa katika kitabu cha Maamuzi ili kuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa shughuli za bunge.”
Baada
ya kusoma kanuni hiyo, Mhagama alisema wabunge hao ambao wamekuwa wakuu wa
wilaya ni sehemu ya serikali, na kutokana na sheria hiyo, alizuia kuulizwa kwa maswali
yao yaliyokuwa
yamepangwa katika orodha ya shughuli za bunge jana katika swali namba 113 na
114.
Swali
namba 113 lilikuwa liulizwe na Subira Mgalu
likielekezwa katika Wizara ya Viwanda na Biashara ambapo alitaka kujua viwanda vingapi vimejengwa na ni kiasi gani cha fedha kimetumika kuwekeza kwenye viwanda hivyo kutokana na ahadi ya Rais katika kipindi cha kampeini ya
uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 hadi leo.
likielekezwa katika Wizara ya Viwanda na Biashara ambapo alitaka kujua viwanda vingapi vimejengwa na ni kiasi gani cha fedha kimetumika kuwekeza kwenye viwanda hivyo kutokana na ahadi ya Rais katika kipindi cha kampeini ya
uchaguzi mkuu wa mwaka 2005 hadi leo.
Martha
Umbulla, pia alielekeza swali lake
Wizara hiyo hiyo akitaka
kujua serikali ina mpango gani wa kujenga viwanda vya kusindika mazao ya kilimo
ili kukuza soko la ndani na kuwezesha kilimo chenye tija kwa wananchi”.
Mbunge
mwingine ambaye pia ni mkuu wa wilaya ni Lucy
Mayenga (Uyuhi, Tabora). Wabunge viti maalum ambao ni wakuu wa mikoa ni Injinia Stella Manyanya, (Rukwa) na Christina Ishengoma (Iringa).
Mayenga (Uyuhi, Tabora). Wabunge viti maalum ambao ni wakuu wa mikoa ni Injinia Stella Manyanya, (Rukwa) na Christina Ishengoma (Iringa).
Wakati
huo huo, Spika Bunge, Anna Makinda hataendsha shughuli za bunge kwa siku kadhaa
kutokana na kufiwa na mlezi wake, Zena Stephano.
JK: Hatuwalipi
·
Asema
wasiotaka waondoke
·
Madaktari
nao wamgomea
·
Mnyika
naye amjia juu
Na Mwandishi
Wetu
HATIMAYE Rais Jakaya Kikwete amewataka
madaktari wote wanaoona hawawezi kufanya kazi serikalini hadi walipwe kiasi cha
sh milioni 3.5, waache kazi na kutafuta sehemu nyingine itakayowalipa vizuri.
Aidha, Kikwete ameweka bayana kuwa
serikali haitaweza kulipa kima hicho cha chini cha mshahara na nyongeza za
posho zitakazomfanya daktari wa ngazi ya chini kulipwa jumla ya sh milioni 7.7
kwa mwezi.
Wakati Rais Kikwete
akitoa tamko hilo , Katibu wa Jumuiya ya
Madaktari nchini, Dk. Edwin Chitage, ameweka bayana msimamo wao wa kutorejea
kazini na kuitaka serikali kuwaleta haraka madaktari kutoka nje kujaza nafasi
zao, kama ilivyotangazwa juzi.
Katika hotuba
yake kwa taifa jana, Kikwete alisema kuwa haoni sababu ya madaktari hao kugoma
na kugombana na mwajiri ili ashinikize kulipwa mshahara huo, badala yake
amewataka kuondoa usumbufu huo wa kuondolewa kwa nguvu, kwa wao kuacha kazi kwa
amani, na kutafuta sehemu itakayokubali kulipa kiasi hicho.
Rais Kikwete
amedai katika tamko hilo la kwanza tangu kuanza
kwa mgomo huo wa madaktari wiki iliyopita, kwamba hakukuwa na haja ya madaktari
hao kufikia uamuzi wa kugoma, hivyo kuleta madhara makubwa yakiwamo ya vifo kwa
wagonjwa hata baada ya serikali kujitahidi kutimiza matakwa yao kwa kiwango kikubwa.
Kikwete ambaye
alitumia kigezo cha nyongeza ya mshahara katika hotuba yake kuitetea serikali
katika mgogoro huo, alisema itakuwa kuwadanganya madaktari hao na Watanzania kuwa
inao uwezo wa kulipa kiasi hicho cha mshahara kutoka kima cha chini cha sh
957,700 cha sasa hadi sh milioni 3.5
“Mwaka
2004/2005, mshahara wa kuanzia wa daktari ulikuwa shilingi 178,700, mwaka
2005/2006 tuliupandisha na kuwa shilingi 403,120. Tuliendelea kuupandisha mwaka
hadi mwaka mpaka kufikia shilingi 957,700 wanazolipwa sasa.
“Kiasi hicho ni mara mbili ya mishahara ya
watumishi wa taaluma nyingine wenye shahada ya kwanza wanaoanza kazi ambao kwa
wastani hupata shilingi 446,100.
“Kwa
sasa hatuwezi kuwaahidi kuwa tunao uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa
shilingi 3,500,000 na posho zote zile. Tukifanya hivyo malipo ya daktari
anayeanza kazi yatakuwa shilingi 7,700,000.
Kwa hakika kiasi hicho hatutakiweza. Si vyema kutoa ahadi hewa kwa watu
tunaowaheshimu na kuwathamini kama walivyo
madaktari,” alisema Kikwete.
Kikwete alisema
Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi Machi, 8, 2012, kwa mujibu wa Sheria ya
Mahusiano Kazini, Namba 6 ya mwaka 2004 ilitoa zuio la mgomo pamoja na kuagiza
kuwepo mazungumzo baina ya pande mbili.
Aliongeza kuwa
kati ya Aprili, 10, 2012 na 30 Mei, 30, 2012, vilifanyika vikao sita vya
majadiliano kati ya Serikali na Chama cha Madaktari, kujadili madai 12 ya
madaktari, ikiwa ni nyongeza ya mshahara kutoka kima cha sasa hadi sh 3.5 milioni.
Posho ya kuitwa kazini (on call allowance) asilimia 10 ya mshahara.
Madai mengine ya
madaktari yalikuwa kulipwa posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi
(Risk allowance) asilimia 30 ya mshahara, madaktari wapatiwe nyumba daraja A au
posho ya makazi ya asilimia 30 ya mshahara, na posho ya kufanya kazi katika
mazingira magumu nayo asilimia 40 ya mshahara.
Kikwete alisema madai mengine ya madaktari
ni posho ya usafiri ya asilimia 10 ya mshahara au wakopeshwe magari, madaktari
wapatiwe Green Card za Bima ya Afya, kuondolewa kwa watendaji wakuu wa Wizara
ya Afya na Ustawi wa Jamii, viongozi wa kisiasa kulazimisha kupewa rufaa nje, madaktari
waliofukuzwa warudishwe kazini, kuboresha huduma za afya na posho ya uchunguzi
wa maiti iongezwe.
Alisema hadi sasa serikali imekubali
kutoa Green Card za Bima ya Afya, kuchukuliwa hatua za kinidhamu dhidi ya watendaji
wakuu wa Wizara ya Afya.
“ Lakini, jambo la kustaajabisha hata
Waziri mpya wa Afya alipowataka waonane kuzungumzia hoja walikataa
kumuona. Kwanza
walisema hawaoni sababu kwa vile wameyazungumza na kamati yake kwa miezi mitatu
bila ya mafanikio.
“ Kuhusu viongozi kulazimisha kupewa
rufaa ya kutibiwa nje, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwataka wazingatie maadili
ya kazi zao na kukataa kutoa rufaa kwa mtu asiyestahili, awe kiongozi au asiwe
kiongozi. Pili, walikubaliana kuwa
hospitali zilizopo ziboreshwe ili viongozi watibiwe hapa nchini. Ukweli ni kwamba kufanya hivyo ndiyo sera ya
Serikali,” alisema.
Aliongeza kuwa serikali pia ilikubali
madaktari waliofukuzwa, na wale Interns
waliokuwa wamerudishwa wizarani kutoka Muhimbili na kupangiwa hospitali za
Temeke, Ilala, Mwananyamala na Lugalo.
Aidha, alisema pande zote
walilokubaliana ni kuhusu kuongeza posho ya uchunguzi wa maiti.
“Hili ni jambo jipya halikuwepo
mwazoni. Hata hivyo, serikali
imelikubali na posho hiyo imeongezwa kutoka shilingi 10,000 hadi kufikia
shilingi 100,000 kwa daktari na shilingi 50,000 kwa wasaidizi wake,” alisema.
Serikali iliwaeleza kuwa watumishi wa
kada zote za afya watapatiwa chanjo dhidi ya maambukizi ya Hepatitis B na fedha zimetengwa katika bajeti ya 2012/13.
“Serikali imeeleza dhamira ya kurudisha
posho ya mazingira hatarishi kwa watumishi wa umma wanaostahili. Utekelezaji wake utafanyika baada ya
uchambuzi wa kina wa kubainisha mazingira hatarishi ni yepi, viwango stahiki
viwe vipi na nani hasa wahusika.
Madaktari wamekataa hili la kufanya uchambuzi, wanataka kiwango kiwe kama wanavyotaka wao, yaani asilimia 30 ya mshahara na
kianze mara moja,” alisema.
Mambo
yaliyoshindikana
Hata hivyo, Kikwete alikiri kuwa kuna
mambo mawili hayakufikiwa muafaka kabisa kati ya pande zetu mbili, nayo ni
posho ya kuitwa kazini (on call allowance).
“ Kwanza sina budi kueleza kuwa serikali
imekubali kuongeza posho hiyo. Tangu
Februari, 2012 posho iliongezwa kutoka shilingi 10,000 hadi shilingi 25,000 kwa
daktari bingwa (specialist), shilingi 20,000 kwa dakari mwenye usajili wa
kudumu (Registrars) na shilingi 15,000 kwa madaktari waliohitimu ambao wapo
katika kipindi cha mafunzo kazini (Interns). Viwango hivyo vya posho vinatumika
hivi sasa.
“Madaktari kwa upande wao hawakukubali
uamuzi huo wa serikali na kusisitiza walipwe asilimia 10 ya mshahara.
Ugumu wa kukubali pendekezo la madakari ni kuwa sharti la malipo haya ni
mtu kuitwa kazini. Ukitaka ilipwe
kiwango cha mshahara ina maana kuwa hata kama daktari hakupangwa kuitwa au
alipangwa na hakutokea aendelee kulipwa.
Hili haliwezi kuwa sahihi kufanya.
Linaweza kuwafanya baadhi ya madaktari kutokutimiza wajibu wao kwa vile
wana hakika mwisho wa mwezi malipo yako pale pale,” alisema.
Alidai jambo la pili ambalo muafaka haukufikiwa
baina ya serikali na madaktari ni kuhusu mshahara wa kuanzia kazi wa daktari,
ambao wanataka uwe shilingi 3,500,000 wakati serikali imesema kiasi hicho hawakiwezi,
badala yake ipo tayari kuongeza mshahara kwa kati ya asilimia 15 mpaka 20 kama
ambavyo itafanya kwa watumishi wote wa umma katika mwaka huu wa fedha.
“Kwa kiwango cha
sasa cha mshahara wao, daktari ataanzia kati ya shilingi 1,100,000 na 1,200,000
kutegemea kiwango kipi hatimaye kitaamuliwa.
Madaktari wamekataa katakata na wameng’ang’ania shilingi 3,500,000,”
alisema.
Jumuiya yashupalia mgomo
Wakati hali ya wasiwasi
ikiwa hivyo, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Edwin Chitage ameitaka
serikali kuwaleta haraka madaktari kutoka nje huku akisisitiza kwamba hawapo
tayari kurejea kazini.
Dk. Chitage alisema iwapo
serikali itaendelea kupuuza madai yao hawatarudi kazini licha ya kupewa siku ya
mwisho kuwa leo wawe wamerejea kazini.
Kwa mujibu wa katibu
huyo, uamuzi wa serikali kutaka kutumia sh bilioni 200 kuwaleta madaktari
kutoka nje ya nchi kabla ya kuboresha mazingira ya utoaji wa huduma ni jambo la
kuhuzunisha.
“Wakitaka wawalete hao
madaktari hata leo lakini sisi msimamo wetu upo palepale… tunataka madai yetu
yafanyiwe kazi kwanza,” alisisitiza Dk. Chitage.
Madaktari bingwa nao juzi
walitangaza mgomo huku wakisisitiza kuungana kwa mabingwa wa hospitali za
Muhimbili, MOU, MUHAS na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road.
MAT waukana mgomo
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Namala Mkopi, alisema
katiba ya chama chao hairuhusu mgomo hivyo tamko la serikali kuwataka waliogoma
kurejea kazini haliwahusu.
Akizungumza kwa kifupi
sana, Dk. Mkopi alisema MAT haijawahi kuitisha mgomo na kwamba madaktari
waliogoma wanafanya hivyo kwa sababu zao.
“MAT haijawahi kugoma kwa
sababu katiba ya chama haituruhusu kufanya hivyo sasa kama kuna daktari
aliyegoma ebu muulize.
TUCTA yahoji bil. 200/-
Katibu wa Shirikisho la
Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Nicholous Mgaya, aliitaka serikali kutafakari
upya uamuzi wa kutumia sh bilioni 200 kuwaleta madaktari kwa sababu unaathiri
wataalamu wa sekta nyingine.
Alisema lazima wananchi
waelezwe fedha hizo zinatoka wapi kwa sababu hazipo kwenye bajeti iliyosomwa
hivi karibuni na Waziri wa Fedha, William Mgimwa.
“Hivi wameshindwaje
kutumia japo nusu ya fedha hizo kutatua sehemu ya matatizo ya madaktari? Hao watakaokuja watakaa kwa kipindi gani? Kwa
nini wameshindwa kuwatimizia madai madaktari wetu?” alihoji.
TEC yanena
Baraza la Maaskofu Katoliki
Tanzania (TEC), limeitaka serikali kukaa meza moja na madaktari ili kumaliza
tatizo hilo.
Rais wa baraza hilo anayemaliza
muda wake, Askofu Mkuu Yuda Thaddeus Ruwaichi, alisema mgomo huo wa madaktari
hauna matokeo mema kwa wananchi ambao ni
waathirika wakubwa katika jambo hilo.
Mnyika amkosoa JK
Naye
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, amekosoa hotuba hiyo, akidai Rais Kikwete hakueleza
kabisa mchango wa serikali katika kusababisha hali hiyo.
“Hivyo, kwa kuwa pande zote mbili zinachangia
katika athari zinazoikumba nchi na wananchi kutokana na mgomo; ni muhimu chombo
cha tatu kikaingilia kati kuwezesha ufumbuzi kupatikana na chombo hicho ni
bunge ambalo ndilo lenye wajibu wa kuisimamia serikali.
“Jitihada za kuwalazimisha madaktari kurejea
kazini bila majadiliano ya pande mbili mbele ya chombo cha kuisimamia serikali
kushughulikia chanzo cha mgogoro huo zinaweza kuleta ufumbuzi wa muda mfupi na
athari za muda mrefu,” alisema.
Alisema hata madaktari wakisitisha mgomo wa
wazi kutokana na amri ya mahakama na agizo la rais, migogoro katika ya serikali
na watumishi wa umma wenye kusababisha migomo baridi ya chinichini ina madhara
ya muda mrefu kwa taifa.
“Mathalani, kutokana na migomo baridi na
huduma mbovu katika sekta ya afya wananchi wa kawaida wamekuwa wakifa kutokana
na magonjwa yanayotibika. Migomo ya chini kwa chini ya walimu na mazingira
mabovu yamekuwa yakisababisha kudidimia kwa elimu katika shule za umma;
mwanafunzi aliyehitimu masomo yake bila kujua kusoma na kuandika hana tofauti
na mgonjwa anayekufa kwa kukosa huduma.
“Hali hii ya kugoma kusiko kwa wazi imeanza
kujipenyeza mpaka kwa askari wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuachia mianya
ya ufisadi na kushindwa kusimamia utawala wa sheria kama ivyodhihirika kwa
kuongezeka kwa vitendo vya biashara haramu katika taifa letu’ alisema Mnyika.
Awashauri
madaktari
Hata hivyo, Mnyika alikwenda mbali zaidi na
kuwaomba Madaktari kuueleza umma msingi wa madai yao na kwa kiwango gani
walikuwa tayari kushuka kutoka katika madai yao ya awali, kinyume na hayo
itaonekana kwamba waliingia katika majadiliano wakiwa na msimamo wa kutaka
madai yao pekee ndiyo yakubaliwe wakati ufumbuzi wa mgogoro wa pande mbili
hupatikana kwa usawa.
“Ni vizuri ikafahamika kwamba katika
majadiliano, pande zote mbili huwa na mapendekezo yake; hivyo upo
uwezekano kwamba yapo madai ambayo madaktari wameyatoa ambayo serikali haina
uwezo wa kuyatimiza kwa kiwango walivyopendekeza na yapo ambayo serikali
imeyakataa wakati ambao ina uwezo wa kuyatekeleza hata ikiwa kwa kiwango
pungufu ya kile kilichopendekezwa na madaktari,: alisema.
UJUMBE WA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA KWA
WAAMINI WAKATOLIKI NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA
Sisi Maaskofu wa
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania
tumekutana katika Mkutano wetu Mkuu wa 65 wa kawaida tangu tarehe 23 – 30 Juni
2012 uliowajumuisha Wakuu wa Mashirika ya Kitawa, wakuu wa Idara, Tume na
Taasisi za Baraza pamoja na wawakilishi Walei.
Lengo la Mkutano huu lilikuwa kutathmini shughuli na kazi zetu za
Kichungaji na za huduma za jamii kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita
(2009-2012) na vile vile kupanga mikakati ya kuboresha shughuli hizo za
Kichungaji na za huduma za Jamii katika Nyanja za Afya, Elimu, Maji, misaada
kwa wasiojiweza, utetezi na ushawishi, kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo
(2012-2015).
Pamoja na kufanya
tathmini ya kina ya utendaji wa Baraza letu katika kipindi hicho kilichopita,
na kupanga mipango kabambe kwa ajili ya utendaji wa Baraza kwa kipindi cha
miaka mitatu ijayo, Mkutano wetu Mkuu
umekuwa fursa ya kujadiliana na kushirikishana baadhi ya matukio/mambo ambayo,
kwa hakika, yameitikisa jamii yetu ya Watanzania na kuidhalilisha mbele ya Jumuiya ya kimataifa.
Kwa namna ya pekee
kabisa, tumetafakari juu ya vuguru za kidini za hivi karibuni zilizotokea
katika Visiwa vya Zanzibar kuanzia 26-28 Mei,
2012 na kupelekea kuchomwa moto kwa baadhi ya Makanisa Visiwani humo pamoja na
uharibifu mkubwa wa mali
na uvunjifu wa amani. Bila kupenda kurudia matamko ya Wadau mbali mbali
waliyoyatoa katika nyakati tofauti kulaani bila kusita hali hiyo ya kutisha na
kusikitisha iliyojitokeza Visiwani humo, tunaunga mkono kwa nguvu zote kauli na
jitihada za wale wote wenye mapenzi mema walioguswa na vitendo hivyo na hivyo kuvilaani.
Tunatoa pole na kueleza mshikamano wetu wa kindugu kwa wale wote walioathirika
kwa namna moja au nyingine na vitendo hivyo vya vurugu ambavyo vimefanya sehemu
ya jamii ya wakazi wa Visiwani humo, hasa Wakristo, kuishi kwa wasi wasi mkubwa
kutokana na vitisho vinavyoendelea kutolewa na baadhi ya vikundi pamoja na hali
ya kutopewa ulinzi wa kutosha na vyombo husika.
Tunaendelea kuwaahidi Sala na mshikamano wetu katika kipindi hiki
kigumu.
Pamoja na hayo,
tunapenda kuwakumbusha Watanzania wenzetu, hasa mamlaka husika kutafakari na
kuzingatia busara ya wahenga waliosema kwamba “mwanzo wa makubwa ni madogo” na kwamba “mdharau mwiba mguu huota tende”. Kumbu kumbu zinatwambia kwamba,
chuki za wazi za kidini zilianza kuinyemelea nchi yetu miaka ya 1990, pale mihadhara
ya kashfa za kidini ilipoanza kuruhusiwa.
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, kwa kuongozwa na busara ya
kichungaji, kwa nyakati tofauti, liliandika barua kuziomba na kuzihimiza Mamlaka
husika kuingilia kati na kuhakikisha kwamba mihadhara kama hiyo haipati nafasi
ya kuendelea katika nchi yetu kwani kamwe haiwezi kuwa na tija isipokuwa kuamsha hisia kali za kidini, jazba na kujenga chuki
miongoni mwa waamini wa dini tofauti. Kwa bahati mbaya, ushauri huo wa Baraza
la Maaskofu ulipuuzwa na mamlaka husika.
Hivi karibuni,
kumekuwa na ongezeko kubwa la vyombo vya habari ambavyo vimeanzishwa na ambavyo
badala ya kuzingatia malengo mazuri ya vyombo vya habari ya kuhabarisha, kuelimisha
na kuburudisha, vimeonyesha malengo ya wazi ya kueneza uzushi, kashfa, chuki na
uchochezi. Bado kuna CD/DVD na Kanda chungu
nzima zilizozagaa mitaani zenye malengo kama hayo ambapo, kwa mshangao mkubwa
wa raia wema wa nchi hii, licha ya wahusika kufahamika na kuonekana wazi wazi,
hakuna hatua za kisheria zinazochukuliwa dhidi yao. Tunachelea hata kudhani kwamba mamlaka
za dola zinawakingia kifua wadau wa harakati hizo.
Mkusanyiko wa
mambo yote haya ndio uliotufikisha hapa tulipo.
Kwa upendo tulio nao kwa nchi yetu na kwa kuzingatia historia ya
mlolongo wa matukio yaliyotufikisha hapa tulipo, tunahofu, lakini kwa uwazi
tunapenda kuziambia mamlaka husika, watu wote wenye mapenzi mema na Watanzania
wote kwa ujumla kwamba, iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa mara moja ili
kurekebisha hali hii, baada ya miaka michache,
hakika kwamba nchi yetu inaweza kuingia katika machafuko makubwa ya
kidini. Ili
kuepuka hali hiyo isitokee, kwa moyo wa unyenyekevu kabisa, tunapendekeza hatua
zifuatazo zichukuliwe:-
· Sisi Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania
tutaendelea kusali ili kuiombea nchi yetu amani. Licha ya sala na maombi ya kawaida kwa ajili
ya lengo hilo,
Mkutano Mkuu umeamua kwamba, tutakuwa na siku moja ya kusali kitaifa kwa ajili
ya kuomba amani;
· Tutaendelea
kutumia sauti yetu ya kinabii kuonya, kukemea na kukaripia vitendo vyote vile
vinavyoashiria kueneza chuki miongoni mwa watu wa dini mbali mbali;
· Kwa kutumia Tume
na Idara zetu, tutaendelea kujenga na kueneza mazungumzano na Waamini wa dini
mbali mbali tukiheshimu tofauti zilizopo. Hii ni kwa sababu tunaamini kwamba,
suala la dini ni wito na hiari ya mtu na hakuna mtu yeyote aliye na haki ya
kumlazimisha mwingine ajiunge na dini yake.
Kwa
upande wa wadau wengine na hasa kwa Serikali yetu pamoja na vyombo vyake vya
usalama tunapendekeza yafuatayo:-
· Mihadhara,
makongamano na mikutano yenye lengo la
kutoa kashfa na kuchochea chuki miongoni mwa dini mbalimbali ipigwe marufuku;
· Vyombo vya habari
vinavyoeneza uzushi, kashfa na uchochezi vidhibitiwe kwa kuchukuliwa hatua za
kisheria ikiwa ni pamoja na kufungiwa;
· Uzushi na uongo
unaoenezwa na vyombo vya habari na watu wenye lengo la kuwachonganisha Watanzania
na waamini wa dini mbali mbali utolewe ufafanuzi mara moja na Wizara na vyombo
vingine vinavyohusika;
· Kuweko na mpango
kabambe wa kutoa elimu ya uraia yenye kina na upana katika nafasi zote,
itakayowawezesha vijana wetu kuwa wazalendo kwa nchi yao na kuepuka propaganda za kuwagawa Watanzania
kwa misingi ya kidini;
· Suala la ukosefu
wa ajira, hasa miongoni mwa vijana, liangaliwe kwa makini kwani linaweza kuwa
moja ya sababu zinazowafanya vijana wengi kujiingiza katika vikundi vya kidini vinavyojenga
chuki na kutoa matumaini ya uongo;
· Lakini, zaidi ya
yote, iwapo Serikali yetu na mamlaka husika inataka kuwa na imani mbele ya
jamii kwamba ina nia thabiti ya kuhakikisha kwamba vurugu za kidini hazipati
nafasi katika Nchi yetu, wale wote wanaohusika na vurugu hizo wachukuliwe hatua
za kisheria mara moja! Ni vigumu kuamini kwamba katika kipindi cha kuanzia
mwaka 2001 mpaka sasa, Makanisa 25 yamekwisha chomwa moto Visiwani Zanzibar
lakini hakuna aliyekamatwa na kuchuliwa
hatua za kisheria!
Tumefanya
mkutano wetu katika mazingira ya kuwepo mvutano kati ya madaktari na serikali na
kwa bahati mbaya sana, kama
tulivyokwisha kutamka huko nyuma, mvutano huu unaleta athari kubwa kwa raia
wasio na hatia, athari ambayo haiwezi kurudishwa. Uhai wa raia wa Tanzania
unaangamia kwa kukosa ulinzi wa tiba.
Katika hili tunapenda kukumbusha kuwa kila mmoja ni mdau. Hakuna hata mmoja anayeweza kulikwepa
hili. Tunapenda kurudia himizo letu la awali
kwamba ni bora ikapatikana njia nyingine iliyo mwafaka zaidi ya kudai haki na mazingira
yanayofaa ya kazi bila kuleta madhara ya kupoteza uhai ambao ni haki msingi ya
kila mwanadamu.
Tunaiasa
Serikali yetu ikae tena pamoja na madaktari na kuchambua hoja zitakazowekwa
mbele yao. Uwazi na ukweli vikitawala hakuna pande
itakayokataa kuridhia eti kwa sababu ya kukataa tu bila hoja. Taifa letu limejipatia aibu mbele ya macho ya
ulimwengu ya jinsi tunavyoshindwa kuishi kile tunachosema kwenye majukwaa.
Mwisho,
tunaendelea kuwaalika Watanzania wenzetu, hasa viongozi wa dini mbalimbali
kuwahamasisha waamini wao wawe raia wema wa nchi hii kwa kuungana pamoja
kuhamasisha upendo, haki, amani na maridhiano miongoni mwa Watanzania wote.
Licha ya tofauti zetu, tuzingatie hasa yale yanayotuunganisha: ubinadamu wetu
na uraia wetu wa nchi yetu Tukufu ya Tanzania ambamo tutake tusitake, ni
lazima wote tuishi! Tuepe ushindani ambao hauna tija isipokuwa kutupeleka
katika kujenga chuki na hali ya kudhaniana vibaya miongoni mwa Waamini
wetu. Iwapo kuna sababu ya kushindana,
tushindane katika kubuni mbinu za kujenga Upendo na Amani miongoni mwa
Watanzania katika kutafuta njia za kuwaletea maendeleo yatakayowatoa kutoka
katika Umaskini, Ujinga na Maradhi ambao ndio adui wetu sote.
Tunaiombea
Nchi yetu Amani na Usalama.
+Jude
Thaddaeus Ruwai’chi
RAIS: BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA/
ASKOFU MKUU JIMBO LA MWANZA
Hali ya Dk Ulimboka tete
HALI ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Madaktari nchini Dk. Steven Ulimboka juzi usiku ilibadilika na kuwa tete kiasi
cha kuwatia wasiwasi madaktari wanaomtibu.
Baadhi ya madaktari wanaomhudumia
mwenyekiti huyo wameliambia Tanzania Daima jana kuwa, Dk Ulimboka hali yake
ilibadilika ghafla juzi usiku, na hivyo kulazimika kumfanyia uchunguzi mpya na kumwongezea
uangalizi.
Akizungumza na waandishi wa habari nje
ya jengo la Kitengo cha Mifupa (MOI) cha hospitali ya Taifa Muhimbili kiongozi
wa jopo la madaktari wanaomtibu Ulimboka, Profesa Joseph Kihamba alisema
uchunguzi mpya umebaini matatizo mengine makubwa ya kiafya.
Alisema vipimo imebaini kuwa kiongozi
huyo ameumizwa zaidi sehemu za shingo, taya, mbavu, hivyo, kukiri kwamba huyo
ameumizwa sehemu kubwa ya mwili.
“Kuna vipimo vinahitajika ninachoweza
kusema ni kwamba tumegundua ameumia sana kwenye singo, taya, ubongo wake, mbavu…
kwa kifupi naweza kusema amejeruhiwa sehemu kubwa ya mwili wake,” alisema
Profesa Kihamba.
Kutokana na mabadiliko hayo, sasa
madaktari wameanzisha mchakato wa kukusanya fedha za kumsafirisha nje ya nchi
kutokana na kukosekana kwa kipimo maalum ambacho kitaweza kugundua madhara
mengine.
Maktari bingwa nao wagoma
Mgomo huo sasa umechukua sura nyingine
baada ya madaktari bingwa kutangaza kujiunga nao huku wakiwataka madaktari
wengine kote nchini kushiriki.
Akitoa tamko la madaktari hao waliokuwepo
kwenye kikao kwa zaidi ya saa nane ndani ya majengo ya MOI, Dk. Catherine
Mng’ong’o alisema uamuzi wa kikao hicho unatokana na ukatili aliofanyiwa Dk.
Ulimboka.
Kwa mujibu wa Dk. Mg’ong’o mgomo huo wa
mabingwa utahusisha hospitali za MOI, Muhimbili, Taasisi ya Saratani ya Ocean Road
na MUHAS zote za jijini Dar es Salaam.
Kabla ya kutoa tamko hilo alisema
madaktari wote nchini wamefadhaishwa na kupata hofu kuhusu usalama wa maisha
yao hivyo kuitaka serikali iweke bayana mustakabali wa wataalam wa sekta hiyo
muhimu.
“Madaktari tumefadhaishwa,
tumesikitishwa pia tumepata hofu kuhusu usalama wa maisha yetu tunaiomba
serikali itamke mustakabali wa usalama wetu.
“Tunalaani ukatili aliofanyiwa Dk.
Ulimboka ambaye hali yake inazidi kuwa mbaya… tunalaani juhudi zinazofanywa na
wadhalimu wanaoitendea mabaya sekta ya afya kwa kutudhuru,” alisema Dk.
Mg’ong’o.
Aidha mabingwa hao wameiomba serikali
kuwarejesha kazini madaktari waliosimamishwa kazi na kunyimwa mshahara wao wa
mwezi wa sita kwa sababu kufanya hivyo ni kuwadhalilisha wataalam hao.
“Hakuna mahali waliposema hoja za mgomo
sio za msingi sasa kwa nini wawasimamishe kazi na kuwanyima mshahara wao wakati
suala hili lipo mahakamani,” alisema kwa niaba ya timu ya madaktari bingwa huku
akisisitiza kwamba huduma kwenye hispitali zilizotajwa zimesitishwa.
Polisi watishia kukamata
madaktari
Jeshi la polisi nchini limetishia
kuwakamata na kufikisha katika vyombo vya sheria madaktari watakaoendelea
kukaidi amri halali ya Mahakama ya kusitisha mgomo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Kamishina
wa Operesheni nchini, Paul Chagoja kwa wandishi wa habari, akisema hawatakuwa
tayari kuona yeyote akitendewewa kinyume na matakwa ya sheria hivyo aliwataka
madaktari kuheshimu viapo vyao vya kazi vinavyosisitiza kwamba udaktari ni
wito.
Alisema ikiwa madaktari hawakuridhishwa
na mwenendo wa mahakama wangefuata sheria kwa kukata rufaa mahakama za juu
kuliko kuchukua uamuzi wa kibabe wa kugoma na kusababisha wagonjwa kukosa
huduma za afya na kusababisha wengine kupoteza maisha.
Akizungumzia kuhusu Jeshi la polisi
kuhusishwa katika tukio la kutekwa na kujeruhiwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Madaktari, Dk. Steven Ulimboka alikana chombo hicho cha usalama kuhusishwa kwa
namna yoyote na tukio hilo kwa sababu wanatambua suluhu ya mgomo kamwe hauwezi
kutatuliwa kwa kumuondoa Daktari huyo bali njia pekee ni ya mazungumzo.
Aliwaonya wale wanaosambaza uvumi wa
kulihusisha jeshi la polisi na tukio la kujeruhi kwake anayachukulia kama
maneno ya kuwakatisha tamaa ili washindwe kufanya uchunguzi wao kikamilifu.
Chagonja pia aliwataka wananchi na
madaktari kuwa na imani na jopo la wapelelezi walioteuliwa kufuatilia suala
hilo, na kwamba watafanya uchunguzi kwa
kina na kwa haki.
Kumetokea sintofahamu baina ya polisi
na watu wa kada mbalimbali kutokana na kuwepo kwa tuhuma zinazolihusisha jeshi
hilo na tukio la kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa vibaya kwa Dk Ulimboka.
Aidha, kutokana na hali hiyo, watu
wengi wamependekeza kuundwa kwa chombo huru kitakachofanya uchunguzi wa haki
kwa sababu tayari jeshi hilo, limekwishachafuka kwa kuhusishwa na tuhuma hizo.
Mwisho
Uchunguzi
ufisadi wa bilioni 300 za gesi
waanza
*Pinda atangaza neema Mtwara, Lindi, Bajeti yake yapita
Serikali imeanza uchunguzi wa tuhuma za mafisadi wanaodaiwa kupora sh bilioni 300 za miradi ya gesi, madini na petrol na kuzihifadhi kwenye akaunti nchini Uswizi.
Akizunguza wakati wa kufanya majumuisho ya hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema kuwa tayari Serikali imeanza uchunguzi wa tuhuma hizo.
"Taarifa hizi tumezipata kupitia vyombo vya habari
na tumeshafanya mawasiliano na vyombo vya dola kwa ajili ya uchunguzi, wakibainika wataenda mahakamani," alisema Pinda.
Taarifa za ufisadi huo uliibuliwa mwishoni mwa wiki ambapo inadaiwa kuwa Watanzania sita wamepokea hongo kutoka makampuni yanayotafiti gesi, madini na petrol na kuweka pesa zao Uswizi.
Akizungumzia ugunduzi wa gesi katika mikoa ya Lindi na Mtwara, Pinda alisema mikoa hiyo itanufaika zaidi na fursa hiyo.
"Niwaambie tu kwamba sasa Lindi, Mtwara kumekuja. Wajipange kwa fursa hiyo na serikali tumejipanga kuhakikisha wananufaika na gesi," alisema.
Akizungumzia posho za madiwani, Pinda alisema wameongezewa kutoka sh 120000 hadi 250000 na posho hiyo itaendelea kuongezeka kadri ya uwezo wa serikali itakavyokuwa.
Bunge limepitisha Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2012/2013 ambapo aliomba kuidhinishiwa sh trilioni 3.2
Kati ya fedha hizo, sh trilioni 2.7 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh bilioni 544.1 kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
Katika Bajeti hiyo, aliomba kuidhinishiwa sh bilioni 176.7 kwa ajili ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake.
Kati ya fedha hizo, sh 68,522,866,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh 108,271,972,000 kwa ajili ya Mpango wa Maendeleo.
Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Asasi zake ziliombewa na kupitishiwa sh.186,891,598,000, kati ya hizo, sh.164,614,726,000) ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na sh 22,276,872,000 kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo.
Ofisi za Wakuu wa Mikoa ziliombewa na kupishiwa sh 173,276,761,000), kati ya hizo, sh.146,552,262,000 kwa matumizi ya kawaida na sh bilioni 26,724,499,000 kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
Ends
waanza
*Pinda atangaza neema Mtwara, Lindi, Bajeti yake yapita
Serikali imeanza uchunguzi wa tuhuma za mafisadi wanaodaiwa kupora sh bilioni 300 za miradi ya gesi, madini na petrol na kuzihifadhi kwenye akaunti nchini Uswizi.
Akizunguza wakati wa kufanya majumuisho ya hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema kuwa tayari Serikali imeanza uchunguzi wa tuhuma hizo.
"Taarifa hizi tumezipata kupitia vyombo vya habari
na tumeshafanya mawasiliano na vyombo vya dola kwa ajili ya uchunguzi, wakibainika wataenda mahakamani," alisema Pinda.
Taarifa za ufisadi huo uliibuliwa mwishoni mwa wiki ambapo inadaiwa kuwa Watanzania sita wamepokea hongo kutoka makampuni yanayotafiti gesi, madini na petrol na kuweka pesa zao Uswizi.
Akizungumzia ugunduzi wa gesi katika mikoa ya Lindi na Mtwara, Pinda alisema mikoa hiyo itanufaika zaidi na fursa hiyo.
"Niwaambie tu kwamba sasa Lindi, Mtwara kumekuja. Wajipange kwa fursa hiyo na serikali tumejipanga kuhakikisha wananufaika na gesi," alisema.
Akizungumzia posho za madiwani, Pinda alisema wameongezewa kutoka sh 120000 hadi 250000 na posho hiyo itaendelea kuongezeka kadri ya uwezo wa serikali itakavyokuwa.
Bunge limepitisha Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka 2012/2013 ambapo aliomba kuidhinishiwa sh trilioni 3.2
Kati ya fedha hizo, sh trilioni 2.7 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh bilioni 544.1 kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
Katika Bajeti hiyo, aliomba kuidhinishiwa sh bilioni 176.7 kwa ajili ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi zake.
Kati ya fedha hizo, sh 68,522,866,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh 108,271,972,000 kwa ajili ya Mpango wa Maendeleo.
Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Asasi zake ziliombewa na kupitishiwa sh.186,891,598,000, kati ya hizo, sh.164,614,726,000) ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na sh 22,276,872,000 kwa ajili ya Matumizi ya Maendeleo.
Ofisi za Wakuu wa Mikoa ziliombewa na kupishiwa sh 173,276,761,000), kati ya hizo, sh.146,552,262,000 kwa matumizi ya kawaida na sh bilioni 26,724,499,000 kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.
Ends
Pinda ayumba tena
* Akwama kutoa kauli ya serikali
* Akwama kutoa kauli ya serikali
* Atakiwa kujiuzulu, yeye
ang’aka
* Kipigo cha Ulimboka
chamtesa
Na Martin Malera,Dodoma
Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa mara nyingine tena jana katika hali isiyotarajiwa na wengi, aliyumba na kushindwa kutoa tamko zito kuhusu mgomo wa madaktari kinyume na alivyokuwa ameahidi mbele ya bunge juzi mjiniDodoma .
Pamoja na kushindwa kwake, Pinda pia alijikuta katika wakati mgumu kuelezea ukweli wa kile kinachodaiwa kuhusika kwa serikali katika tukio la kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa vibaya kwa kiongozi wa jumuiya ya madaktari nchini, Steven Ulimboka.
Akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (Chadema) katika kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu, ambaye alitaka kujua hatua ya serikali ya kutotoa tamko wakati juzi alitoa kauli nzito ya ‘liwalo na liwe’ kuhusu mgomo wa madaktari na kuibua hofu kubwa kwa wananchi, Serikali inalieleza nini taifa kuhusu hali hiyo na inafanya nini kumaliza mgomo huo.
Akijibu swalihilo , Pinda kwanza alikiri kuahidi
kutoa tamko la Serikali akitumia neno la “liwalo na liwe’, lakini akadai kuwa
serikali haitaweza kutoa tamko hilo tena baada
ya kupata ushauri wa kisheria kwa kuwa jambo hilo liko mahakamani.
"Kwa bahati mbayasana
kauli yangu ya 'Liwalo na Liwe' imetafsiriwa kwa namna tofauti. Hata dada yangu
Halima Mdee nilimsikia akitilia shaka kauli hiyo na kuhusisha na tukio la
kutekwa kwa Dk. Ulimboka.
"Nilichoaminisha ni kwamba hili jambo liko mahakamani, lakini tungetolea tamko la Serikali bila kujali kwamba sualahilo
liko mahakamani ndo maana nikasema Liwalo na Liwe"
Alisema baada ya mashauriano na wataalamu wa serikali jana usiku waliona si vyema kuendelea na tamkohilo
hadi kesi iliyopo mahakama itakapomalizika.
Kuhusu tukio la kutekwa, kupigwa kwa Ulimboka, Waziri Mkuu Pinda alisema Serikali imeguswa na kushitushwa na tukiohilo ,
na akadai kuwa amesikitishwa na kuwepo kwa taarifa zinazoituhumu serikali
kuhusika na unyama huo.
Na Martin Malera,
Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa mara nyingine tena jana katika hali isiyotarajiwa na wengi, aliyumba na kushindwa kutoa tamko zito kuhusu mgomo wa madaktari kinyume na alivyokuwa ameahidi mbele ya bunge juzi mjini
Pamoja na kushindwa kwake, Pinda pia alijikuta katika wakati mgumu kuelezea ukweli wa kile kinachodaiwa kuhusika kwa serikali katika tukio la kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa vibaya kwa kiongozi wa jumuiya ya madaktari nchini, Steven Ulimboka.
Akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (Chadema) katika kipindi cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu, ambaye alitaka kujua hatua ya serikali ya kutotoa tamko wakati juzi alitoa kauli nzito ya ‘liwalo na liwe’ kuhusu mgomo wa madaktari na kuibua hofu kubwa kwa wananchi, Serikali inalieleza nini taifa kuhusu hali hiyo na inafanya nini kumaliza mgomo huo.
Akijibu swali
"Kwa bahati mbaya
"Nilichoaminisha ni kwamba hili jambo liko mahakamani, lakini tungetolea tamko la Serikali bila kujali kwamba suala
Alisema baada ya mashauriano na wataalamu wa serikali jana usiku waliona si vyema kuendelea na tamko
Kuhusu tukio la kutekwa, kupigwa kwa Ulimboka, Waziri Mkuu Pinda alisema Serikali imeguswa na kushitushwa na tukio
Waziri Mkuu aliliambia bunge kuwa madai hayo ya kuituhumu
serikali yanashangaza kwa sababu, yeye mwenyewe alipata taarifa ya kufanyiwa
vitendo hivyo akiwa bungeni na hata wakati alipoahidi kutoa tamko la
Serikali hakuwa anajua chochote.
"Dk. Ulimboka tumekuwa naye kwenye vikao vya ndani vya majadiliano, tuko naye mahakamani. Leo Serikali ihusike kumteka, kumpiga na kumtesa kwa kiasi kile ili iweje,?"
Alisema Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi ameshatoa kauli juu ya tukiohilo , hivyo
alisisitiza kuwa Serikali itafanya uchunguzi wa kina kuwanasa waliohusika.
Akijibu swali la nyongeza la Mbowe aliyetaka kujua hatua za dharula zilizochukuliwa na Serikali kumaliza mgomo huo hasa baada ya kusitisha tamkolake Bungeni ,
Pinda alisema Serikali itaendelea na majadiliano na madaktari hao ili kufikia
muafaka.
"Hatua nyingi ya dharura tuliyochukua Serikali ni kuzungumza na hospitali ya Lugalo na zingine ndogo kubeba jukumuhilo kwa sasa,
pia tumeagiza madaktari wastaafu wote warejee kazini katika kipindi hiki cha
mgomo," alisema Pinda.
Lissu amtaka ajiuzulu
"Dk. Ulimboka tumekuwa naye kwenye vikao vya ndani vya majadiliano, tuko naye mahakamani. Leo Serikali ihusike kumteka, kumpiga na kumtesa kwa kiasi kile ili iweje,?"
Alisema Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi ameshatoa kauli juu ya tukio
Akijibu swali la nyongeza la Mbowe aliyetaka kujua hatua za dharula zilizochukuliwa na Serikali kumaliza mgomo huo hasa baada ya kusitisha tamko
"Hatua nyingi ya dharura tuliyochukua Serikali ni kuzungumza na hospitali ya Lugalo na zingine ndogo kubeba jukumu
Lissu amtaka ajiuzulu
Majibu ya Pinda
yalimkoroga Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyesimama na kumuuliza
sababu gani zinazomfanya aendelee kushikilia wadhifa wake huku akitambua kuwa
ameshindwa kumaliza mgogoro huo.
"Mheshimiwa Waziri Mkuu, Februali mwaka huu wakati wa mgomo wa madaktari uliahidi kwamba mgomo huo hautatokea tena, leo mgomo umerudi tena, je, kwanini usijiuzulu?" Alihoji Lissu.
"Mheshimiwa Waziri Mkuu, Februali mwaka huu wakati wa mgomo wa madaktari uliahidi kwamba mgomo huo hautatokea tena, leo mgomo umerudi tena, je, kwanini usijiuzulu?" Alihoji Lissu.
Pinda alidai kuwa tangu
kuanza kwa mgogoro huo, amefanya jitihada za kutosha kujaribu kunusuru mgomo
huo, na kwamba anaamini amefanya kazi kubwa kuufikisha hapo ulipo.
Hata hivyo, Lissu
alisimama na kumwambia waziri mkuu, kwamba hapo alipoufikisha ni pabaya zaidi
na haoni sababu ya yeye kuendelea kuwepo madarakani, kauli iliyoonekana kumkera
Pinda ambaye alidai kuwa yapo mambo ambayo yanaweza kumfanya akajiuzulu, lakini
sio katika sakata la mgomo wa madaktari.
"Mheshimiwa Lissu hii sio lugha nzuri ya kusema, nakuheshimusana ," alisema Pinda na kuzima swali hilo .
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Martha Mlacha (CCM), alihoji endapo serikali inajuakama kuna kikundi cha watu kinachochochea mgomo huo kwa kuwapa fedha. Akijibu hoja
hiyo, Pinda alikiri kupata taarifa hizo na akadai kuwa serikali inafanya
uchunguzi kubaini ukweli, ikiwa ni kweli wahusika watachukuliwa hatua.
Juzi Pinda aliahidi kutoa kauli ya Serikali wakati akijibu mwongozo Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Dhambi (CCM) aliyetaka kujua msimamo kuhusu mgomo wa madaktari.
"Mheshimiwa Lissu hii sio lugha nzuri ya kusema, nakuheshimu
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Martha Mlacha (CCM), alihoji endapo serikali inajua
Juzi Pinda aliahidi kutoa kauli ya Serikali wakati akijibu mwongozo Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Dhambi (CCM) aliyetaka kujua msimamo kuhusu mgomo wa madaktari.
Madaktari waikataa tume ya polisi
Jumuiya ya Madaktari
nchini imesema haina imani na tume iliyoundwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya
kuchunguza unyama aliofanyiwa Dk. Ulimboka huku wakisisitiza kuwepo kwa chombo
huru zaidi.
Licha ya kutaka tume
huru, madaktari hao wamesema wataendelea na msimamo wao wa kuhakikisha
wanatetea maslai yao
pamoja na mazingira magumu ya kufanyia kazi yanayowakabili kwa sasa.
Akizungumza na waandishi
wa habari nje ya jengo la MOI Katibu wa Jumuiya hiyo Dk. Edwin Chitage alisema
madaktari nchini wanahitaji chombo kilichohuru kitakachochunguza tukio hilo kwa undani zaidi
kuliko jeshi la polisi.
Alisema hawana imani na
tume hiyo kwa sababu si huru kitakachopatikana kwa utaratibu unaoeleweka,
kuliko polisi tu hasa wakizingatia
mazingira ya kutekwa na kupigwa kwa mwenzao ingawa hawawezi kusema kama jeshi la polisi linahusika.
“Tutaendelea kupigania
masuala ya mazingira bora ya kazi kwani hatufurahii kuona msongamano wa
wagonjwa wodini, mgonjwa akilala chini, watoto wachanga kulala zaidi ya watano
kitanda kimoja na kukosekana kwa dawa na vifaatiba,” alisema.
Awali aliwataka madaktari
wote nchini kuwa watulivu hasa katika kipindi hiki kigumu na kusisitiza kwamba
tukio hilo
limewaimarisha na kuwazidishia mshikamano.
Afya ya Ulimboka yaimarika
Hali ya afya ya
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini Dk. Steven Ulimboka inaendelea kuimarika
licha ya maumivu makali yanayomkabili.
Akizungumza kwa tabu na
waandishi wa habari kwenye chumba cha wagonjwa mahututi kwenye Kitengo cha
Mifupa (MOI) Dk. Ulimboka alisema; “Namshukuru Mungu naendelea vizuri tofauti
na nilivyofikishwa hapa jana…bado nina maumivu makali naomba kama
kuna watu wanataka kuja kuniona wasije ili nipumzike,” alisema.
Awali Ofisa Uhusiano wa
MOI Jumaa Almas alisema hali ya Dk. Ulimboka inaendelea vizuri tofauti na
alivyoletwa juzi asubuhi kwa kuwa sasa ana uwezo wa kutambua watu wanaofika
kumjulia hali na kuzungumza kidogo.
“Kwa sasa hali yake ni
nzuri na yupo chini ya uangalizi wa jopo la madaktari linaloongozwa na Profesa
Joseph Kahamba,” alisema.
Kuhusu mgomo katika
kitengo hicho Almas
alisema ni huduma za dharura pekee zinazotolewa huku zile za kawaida zikiwa
hazifanyiki kabisa.
Dk. Ulimboka alifikishwa
hospitalini hapo baada ya kutekwa na watu wasiojulikana kisha kumpiga,
kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kutupwa kwenye msitu wa Pande,
nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mwenyekiti huyo ambaye
amekua akiratibu mgomo ya madaktari unaoendelea, aliokotwa na msamaria mwema
akiwa amefungwa mikono akiwa amejeruhiwa
vibaya.
Vyama vyaendelea kulaani
Kutoka Mkoani Mwanza, Sitta Tumma anaripoti kuwa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU), Kanda ya Ziwa kimelaani vikali kitendo cha kinyama cha kupigwa na kuumizwa vibaya, alichofanyiwa Dk. Steven Ulimboka, na kuelekeza tuhuma hizo kwa Serikali.
RAAWU imesema, ushahidi wa mazingira unaonesha dhahiri kwamba Serikali imehusika kwa namna moja au nyingine kumdhuru kiongozi huyo wa madaktari nchini, ikiwa ni lengo la kutaka kuzima mgomo wa madaktari unaoendelea katika kudai maslahi na huduma bora ya matibabu kwa Watanzania.
Katibu wa RAAWU Kanda ya Ziwa, Ramadhani Mwendwa, ameliambia Tanzania Daima ofisini kwake kuwa kuna haja ya serikali kujisafisha kwa sababu mazingiora ya tukio hilo inaiweka katika hali ya kutuhumiwa
Mwendwa ambaye pia ni Katibu wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Mkoa wa Mwanza, alizidi kudai kuwa, manyanyaso na ukandamizwaji mkubwa unaofanywa na Serikali inaonesha wazi kwamba viongozi wa Tanzania wanawapeleka wananchi wao katika machafuko.
"Tusifike hukokama nchi nyingine
zinavyopigana. Viongozi wa wafanyakazi tuweni wamoja na wafanyakazi wote katika
kutetea maslahi ya taifa. Tusirudi nyuma", alisema Mwendwa.
CUF, Chadema wanena
Kutoka Mkoani Mwanza, Sitta Tumma anaripoti kuwa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Habari na Utafiti nchini (RAAWU), Kanda ya Ziwa kimelaani vikali kitendo cha kinyama cha kupigwa na kuumizwa vibaya, alichofanyiwa Dk. Steven Ulimboka, na kuelekeza tuhuma hizo kwa Serikali.
RAAWU imesema, ushahidi wa mazingira unaonesha dhahiri kwamba Serikali imehusika kwa namna moja au nyingine kumdhuru kiongozi huyo wa madaktari nchini, ikiwa ni lengo la kutaka kuzima mgomo wa madaktari unaoendelea katika kudai maslahi na huduma bora ya matibabu kwa Watanzania.
Katibu wa RAAWU Kanda ya Ziwa, Ramadhani Mwendwa, ameliambia Tanzania Daima ofisini kwake kuwa kuna haja ya serikali kujisafisha kwa sababu mazingiora ya tukio hilo inaiweka katika hali ya kutuhumiwa
Mwendwa ambaye pia ni Katibu wa Shirikisho la vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Mkoa wa Mwanza, alizidi kudai kuwa, manyanyaso na ukandamizwaji mkubwa unaofanywa na Serikali inaonesha wazi kwamba viongozi wa Tanzania wanawapeleka wananchi wao katika machafuko.
"Tusifike huko
CUF, Chadema wanena
VYAMA vya CUF na
Chadema, vimelaani kitendo cha kutekwa na kupigwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Madaktari, Dk. Stephen Ulimboka, huku vikiitaka serikali kuunda tume huru ya
uchunguzi.
Mkurugenzi wa Mafunzo
na Oganizesheni wa Chadema, Benson Kigaila, alisema kuwa kitendo hicho jitihada
za serikali kuwanyamazisha watetezi wa maslahi ya umma.
Akizungumza jijini
Dar esSalaam jana, alisema hizo ni dalili za wazi za serikali ya CCM kushindwa
kuhimili demokrasia ya wengine.
“Tumeshuhudia hali
hii ikiwakumba wengi, kumbukeni tukio la mhariri wa Mwanahalisi Sued Kubenea
kumwagiwa tindikali, mauaji ya Masudi Mbwana kule Igunga na hata kuuawa kwa
mwenyekiti wa Chadema kule Arumeru ni katika njia za kutaka kuwanyamazisha na
kuwatisha wengine,”alisema Kigaila
Alisema katika mgomo
wa kwanza wa madaktari Rais Jakaya Kikwete aliuhakikishia umma kuwa
watayashughulikia matataizo ya madaktari na kwamba suala la mgomo kwao litakuwa
ni ndoto.
Kwa upande wao CUF,
Naibu Mkurugenzi wa Itikadi na Uenezi,
Abdul Kambaya, alilitaka jeshi la polisi kuacha kuchunguza tukio hilo kutokana kutolitilia
maanani tangu awali walipopewa taarifa.
Akizungumza jana
na Tanzania Daima, alisema kuwa
kitendo alichofanyiwa Dk.Ulimboka
ni aibu kwa
taifa kwa kushindwa
kufanya ulinzi wa viongozi watu
wake.
Alisema
uchunguzi huo wa tukio unatakiwa kufanywa na taasisi zingine huru ili kutoa kutoa majibu sahihi
kwa wananchi lakini si jeshi la
polisi.
“Serikali
haiwezi kujitoa katika tukio hili
la kinyama alilofanyiwa Dk.Ulimboka hasa ukizingatia ni katika kipindi kifupi
ambacho madaktari wako kwenye mgomo na huyu ni kiongozi wao,” alisema Kambaya.
MBUNGE AMWAGA CHOZI MAUAJI YA ALBINO
MBUNGE wa Viti Maalum, Alshaymaa Kweigir (CCM) jana aliangua kilio Bungeni na kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kupinga Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa mwaka huu wa Fedham
Mbunge huyo alipinga Bajeti hiyo kwa madai kuwa Waziri Mkuu ameshindwa kukabiliana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na kwamba haungi mkono hoja.
Mbunge huyo alisema anasikitishwa na Serikali kutochukua hatua dhidi ya watu wanaowaua albino bila hatia.
Alisema idadi ya vifo vya albino nchini imeongezeka na kufikia 80 katika kipindi ambacho hakufafanua.
Alisema Albino wengi wamepoteza maisha, lakini wauaji wa watu hao wapo lakini hawakamatwi.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu wewe ndio mtu wakutusaidia sisi walemavu wa ngozi lakini umekaa kimya, hivi karibuni aliuwawa Faru ambaye alikuwa anaitwa George na mtu aliyehusika na mauaji hayo alikamatwa kwanini wauaji wa albino hawakamatwi,"
"Hivi karbibuni kauwawa albino huko Arumeru na walemavu hawa wamekuwa wakiuwawa kwakukatwa viungo vyao mbalimbali vya mwili vikiwemo viungo vya sehemu za siri kwa kweli napata uchungu siungi mkono hoja," alisema Mbunge huyo na baadaye
akaanza kulia.
Wakati akiendelea kulia, Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Adam Malima aliinuka kwenye kiti chake na kwenda kumchukua na kumtoa nje ya ukumbi wa Bunge huku akimbembeleza.
Awali akichangia bajeti hiyo Mbunge huyo aliishauri Serikali kuweka alama za barabarani ambazo ni maalum kwa ajili ya walemavu wasioona, wasiosikia na walemavu wa viungo ili kuwasaidia wakati wa kuvuka.
Mbunge huyo alifafanua kuwa walemavu hao wamekuwa wakipata taabu mara wanapotaka kuvuka barabara hivyo ni vyema Serikali ikaliangalia suala hilo kwa kina.
Aidha alisema kumekuwa na alama za barabarani ambazo ni maalum kwa ajili ya walemavu lakini hazitumiki.
Kiongozi wa madaktari atekwa, aumizwa
- Aokotwa Mabwe
Pande akiwa mahututi
- Madaktari wazusha
vurugu kubwa Muhimbili
- Chadema waishukia
serikali, wataka maelezo
- Waziri Mkuu Pinda
kutoa msimamo mzito leo
WATU wasiojulikana, juzi usiku
walimteka kisha kumpiga na kumjeruhi vibaya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari
Dk. Steven Ulimboka.
Ulimboka ambaye amelzwa katika
hospitali ya taifa ya Muhimbili akiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi inadaiwa
alitekwa na watu hao akiwa na daktari mwenzake aliyetajwa kwa jina la Deo, eneo
la kinondoni baada ya kupigiwa simu na watu hao.
Kiongozi huyo ameng’olewa meno na kucha
na watu ambao haijajulikana, huku baadhi wakidai ni watumishi wa Idara ya
Usalama wa Taifa, huku wengine wakisema ni majambazi.
Ulimboka alifikishwa Muhimbili majira
ya saa 04:54 asubuhi na kupelekwa moja kwa moja katika Kitengo Cha Mifupa (Moi)
na kupokelewa na Dk Cuthbert Mcharo.
“Tumempokea Dk Ulimboka ambaye hali
yake si nzuri tumempeleka katika chumba cha dharura ili kumfanyia vipimo na
uchunguzi,” alisema Dk Mcharo.
Baadhi ya madaktari walishindwa
kuhimili na kuangua vilio vilivyoongeza simanzi huku wengine wakisema kauli ya
liwalo na liwe iliyotolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda imeanza kutekelezwa.
Ulimboka anena
Akizungumza kwa taabu baada ya
kufikishwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, Dk. Ulimboka alisema akiwa
na rafiki zake alipigiwa simu na mtu anayemfahamu na ambaye walishawahi
kukutana akimtaka wakutane.
Ulimboka alisema mara baada ya mtu huyo
kufika walipokuwa, walianza mazungumzo, lakini wakiwa katikati yule mtu
aliwasiliana kwa njia ya simu na watu asiowafahamu, na baada ya muda mfupi
kabla ya kuagana liliwasili gari moja lenye rangi nyeusi likiwa halina namba.
“Wakashuka watu kama watano hivi wakiwa
na bunduki wakawaambia wale wenzangu na yule niliyekuwa naongea nae kuwa wako
free (huru), wakaniingiza kwenye gari
lao kwa nguvu” alisema Dk. Ulimboka
Naye Katibu wa Jumuiya ya Madaktari Dk Godwin
Chitage alisema juzi wakiwa na Dk. Ulimboka walipigiwa simu na mtu wa usalama
wa taifa (jina limehifadhiwa) akamtaka wakutane usiku huo.
“Walitoka Ulimboka na Dk. Deo wakaenda
maeneo ya Kinondoni Sterio walipokutana naye akaanza kupiga simu likaja gari
jeusi, wakashuka watu wanne wakiwa na silaha, na kumtaka Dk. Deo aondoke, ndipo
yakaanza malumbano kabla ya kumzidi nguvu na kumwingiza kwenye gari kisha
kuondoka naye”
“Tulipopata taarifa kutoka kwa Deo
tukaanza kupiga simu ya Dk. Ulimboka ikawa haipatikani tena.Tulienda Oysterbay
polisi kutoa taarifa lakini hatukupata ushirikiano wa kutosha tukaenda
‘Central’ (kituo cha Kati) tukaambiwa tusubiri hadi kesho hapo ilikua saa saba
tangu saa tano walipomteka.
Alisema asubuhi walipata taarifa kutoka
kwa msamaria mwema kwamba Ulimboka amepigwa sana na ametelekezwa kwenye msitu
wa Pande, na walifuatilia ingawa anadai walikosa ushirikiano kwenye kituo cha
polisi Bunju.
“Kitendo alichofanyiwa mwenyekiti wetu
kimetufanya kuwa imara zaidi katika kupigania haki zetu. Tutasimama kwa pamoja
kwa gharama yoyote hata kama ni kutoa uhai wetu.
“Nawaomba watanzania wote wanaoitakia
amani Tanzania walaani kitendo hiki, tunawalaani wote waliofanya juhudi za
kumchelewesha Dk. Ulimboka kufika hospitali ili lengo lao la kumtoa uhai
litimie,” alisema Dk. Chitage.
Kauli ya MAT
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT)
kimelaani kitendo alichofanyiwa Dk. Ulimboka na kusema kimewafadhaisha na
kimewavunja moyo katika utendaji kati yao na serikali.
Akizungumza na waandishi wa habari nje
ya jengo la MOI alikolazwa Dk. Ulimboka, Mwenyekiti wa MAT Dk. Namala Mkopi
alisema wamesikitishwa zaidi na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliyoitoa
bungeni jana baada ya kuulizwa kuhusu mgomo huo akisema liwalo na liwe.
“Kazi ya MAT ni kulinda na kutetea haki
za watumishi wa sekta ya afya hususan madaktari kuhakikisha wanakuwa na
mazingira bora ya kazi kwa manufaa ya wananchi.
Mkuu wa Polisi Salenda
apigwa
Katika tukio lisilo la kawaida mtu
mmoja anayedaiwa kuwa mkuu wa kituo kidogo cha polisi daraja la Salenda alipata
kipigo kikali kutoka kwa kundi la madaktari, baada ya kuhisiwa kuwa ni mmoja wa
watu waliohusika na kumtekaji nyara Dk Ulimboka.
Inadaiwa polisi huyo ambaye alihisiwa
kuwa mtumishi wa usalama wa taifa, alichepuka baada ya kumwona Ulimboka na
kisha akasikika akizungumza na wenzake kwa njia ya simu kwamba,
alikuwa(ulimboka) hajafa.
Afisa huyo aliokolewa askari wanaolinda
hospitali hiyo na kupelekwa kwenye chumba kidogo kilichopo jirani na lango la
kuingilia hospitalini hapo, ambapo baada ya muda askari polisi zaidi waliwasili
wakiwa katika gari lenye namba za usajili T226 AMV wakiingia na kutoka katika
chumba hicho.
Majira ya saa 05:20 asubuhi gari aina ya
Toyota lenye namba za usajili T716 BKZ ililiwasili na kumchukua afisa huyo ambaye
alidai kupoteza “Redio call” na bastola yake katika shambulio hilo.
Kova aunda Tume ya
Uchunguzi
Katika hatua nyingine, kamanda wa
polisi wa Kanda Maalum ya dare s Salaam, Seelema Kova ameunda tume maalum ya
wataalam wa jeshi hilo, kuchunguza kwa makini tukio zima la kushambuliwa kwa
kiongozi huyo wa madaktari nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari
jana, Kova alisema tume hiyo itaongozwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Polisi, Ahmed Msangi, na kwamba wahusika watakaokamatwa watafikishwa mahakamani
bila kujali ni akina nani.
Akizungumzia kupigwa kwa polisi Muhimbili,
Kova alisema waliohusika walitenda kosa baada ya kudhani kuwa ni mmoja wa watu
waliohusika kumpiga Ulimboka.
“Huyu alikuwa katika kazi ya operesheni
kuwasaka waliohusika na tukio hilo. Na alifika pale kuhakikisha kama kweli
amepatikana na ndio maana akachepuka pembeni kutuarifu kuwa alikuwa Ulimboka.
Sasa wao wakachukua sheria mkononi na kuanza kumshambulia” alisema Kova
Pinda kutoa tamko leo
KIPIGO alichokipata kiongozi wa madaktari, Dk. Ulimboka na kauli nzito aliyoitoa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu mgomo wa madaktari, kimelivuruga Bunge.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), ndiye aliyechafua hali ya hewa jana baada ya kutilia shaka kauli ya Waziri Mkuu Pinda na kipigo cha daktari huyo.
Jana asubuhi wakati Waziri Mkuu akijibu mwongozo wa Mbozi Mashariki, Godfrey Dhambi (CCM), aliyetaka kujua msimamo wa serikali kuhusu mgomo huo, alisema leo Serikali itatoa uamuzi mzito kuhusu mgomo wa madaktari na 'Liwalo na Liwe'
Mbunge huyo alisema wakati madaktari walipotoa tishio la mgomo wiki mbili zilizopita, Waziri wa Afya, Dk. Hussein Mwinyi alitoa kauli ya Serikali Juni 22 kwamba Serikali imetekeleza madai ya madaktari na kuongeza posho.
Kwa mujibu wa Zambi licha ya kauli hiyo, madaktari katika baadhi ya hospitali ikiwemo Muhimbili walianza mgomo.
"Mheshimiwa Spika, leo nimepigiwa simu kutoka Mbeya,
Akijibu mwongozo huo, waziri mkuu Pinda alikiri kuwa kweli Serikali imeenda mahakamani kupinga mgomo huo na mahakama iliwazuia madaktari kugoma na kuwataka watangaze kwenye vyombo kwamba wamesitisha mgomo.
Kwa mujibu wa Pinda, madaktari walikaidi amri hiyo na jana Serikali ilikimbilia tena mahakamani na mahakama ilikazia uamuzi wake wa awali.
"Tunafikiri sio vizuri kuingilia kazi ya mahakama lakini pia tulidhani madakatari wataheshimu amri ya mahakama.
"Kesho (leo) serikali itatangaza hatua za kuchukua. Maana wakati mwingine waswahili wanasema ' Litakalo na Liwe,' alisema Pinda na kushangiliwa na wabunge wote.
Chadema yataka tamko
Hata hivyo, kauli ya Pinda imeleta tafrani baada ya wabunge wawili wa Chadema, Halima Mdee ambaye ni mbunge wa Kawe na Mbunge wa Ubungo John Mnyika kutaka maelezo yakinifu kuhusiana na mambo ya kutatanisha katika mgogoro huo.
Hata hivyo, kauli ya Pinda imeleta tafrani baada ya wabunge wawili wa Chadema, Halima Mdee ambaye ni mbunge wa Kawe na Mbunge wa Ubungo John Mnyika kutaka maelezo yakinifu kuhusiana na mambo ya kutatanisha katika mgogoro huo.
Mdee
alimtaka Waziri Mkuu Pinda kutoa maelezo ya serikali kuhusiana na tukio la
kuvamiwa, kutekwa na kisha kupigwa vibaya kwa Ulimboka, akitiliwa mashaka kauli
ya kiongozi huyo mkuu wa shughuli za serikali bungeni aliyedai kuwa sasa
‘liwalo na liwe’.
Mbunge
huyo alidai kuwa kauli ya Pinda inaleta mashaka na hisia kuwa serikali
inahusika na tukio la kinyama alilofanyiwa Dakta Ulimboka.
Naye Mnyika kukamatwa na
kushambuliwa kwa kiongozi wa madaktari Ulimboka Steven utachochea zaidi mgogoro
kati ya madaktari na serikali
“Udhaifu wa serikali
kuharakisha kwenda mahakamani kabla ya bunge kupewa fursa ya kujadili madai ya
madaktari na kuisimamia serikali umelifikisha taifa hapa tulipo” alisema.
Mbunge huyo aliliambia
Bunge kuwa serikali inajikanyaga katika sakata hilo kwa sababu imekishitaki Chama cha Madaktari
nchini (MAT), lakini iliyotangaza mgomo ni Jumuiya ya Madaktari.
Pia Mnyika aliomba Bunge liruhusiwe haraka kujadili hoja za madai ya madaktari ili kuisimamia serikali kwa mujibu wa ibara ya 63 (2) ilio kupitisha maazimio kupata suluhu wa mgogoro huo.
Pia Mnyika aliomba Bunge liruhusiwe haraka kujadili hoja za madai ya madaktari ili kuisimamia serikali kwa mujibu wa ibara ya 63 (2) ilio kupitisha maazimio kupata suluhu wa mgogoro huo.
“Waziri
Mkuu Mizengo Pinda ametoa maelezo bungeni kuwa kesho tarehe 28 Juni 2012
Serikali itatoa kauli bungeni kuhusu suala la mgomo wa madaktari, hata hivyo
kauli hiyo itatolewa kwa mujibu wa kanuni ya 49 (1) hivyo bunge halitaruhusiwa
kujadili kauli husika na hivyo kukoseshwa fursa ya kuisimamia serikali kwa niaba
ya wananchi.
Alisema bunge
linakoseshwa fursa ya kusikiliza upande wa pili wa madaktari na wahudumu
wengine wa afya ambao walipewa nafasi ya kuwasilisha maelezo na vielelezo vya
upande wao kwenye kamati ya bunge ya huduma za jamii.
Mnyika alidai kumeshangaa
Naibu Spika Job Ndugai kudai kuwa tayari kamati ya huduma za jamii imewasilisha
taarifa bungeni wakati wabunge hawajapewa nakala husika na wala haijawasilishwa
kwenye bunge kwa ajili ya kujadiliwa
“Ikumbukwe kwamba jana
tarehe 26 Juni 2012 niliomba muongozo kuhusu kauli za mawaziri kwa mujibu wa
kanuni ya 49 (2) na 116, hata hivyo niliruhusiwa kuomba kutoa maelezo kuhusu
kauli ya serikali juu ya utekelezaji wa madai ya madaktari na uboreshaji wa
maslahi ya madaktari.
Mnyika alisema kuzembea
ama kupuuza kuchukua hatua dhidi ya udhaifu uliojitokeza kutaleta madhara zaidi
kwa kuwa hata serikali ikichukua hatua za kudhibiti mgomo kwa kutumia vyombo
vya dola, madaktari na watumishi wa afya wataendelea na mgomo wa chini kwa
chini, hivyo afya na maisha ya wananchi yataendelea kuathirika kwa muda mrefu
zaidi.
“Ikiwa wabunge tutaelezwa
ukweli na kupewa taarifa kamili tutaweza kuisimamia serikali na kuwaeleza
ukweli madaktari kipi kinawezekana na kipi hakiwezekani na nichukue fursa hii
kuwaomba madaktari kufanya kila kinachowezekana kuokoa uhai wa wagonjwa katika
kipindi hiki kigumu” alisema Mnyika
Zitto: sitaki kuamini Tanzania tumefika huko
Naye Naibu Katibu Mkuu wa
Chadema, Zitto Kabwe ameeleza kuchukizwa kwake na tukio la kutekwa, kupigwa na
kuumizwa vibaya kwa Dk Ulimboka, akidai mambo kama
hayo yanatokea kwenye nchi za kidikteta na kuongozwa kiimla
“Sitaki kuamini kwamba Tanzania
imefikia huko.
Serikali kama mlinzi wa usalama
kwa raia ina wajibu kueleza tena kwa haraka ni nini kimetokea kwa kijana huyu
msomi na kiongozi wa wataalamu wenzake.
“Nimemuomba Waziri kivuli wa Afya
wa Chadema kufuatilia suala hili kwa karibu sana ili kuhakikisha kwamba ukweli wote
unafahamika. Kamwe hatuwezi kuacha Mtanzania yeyote aonewe, anyanyaswe au
akandamizwe eti kwa sababu ya kudai haki yake na za wenzake” alisema Zitto.
Nchimbi asema serikali haihusiki
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa serikali haihusiki na wala haijatoa maelekezo ya kumshambulia Ulimboka.
Aliahidi kuwa itafanya uchunguzi wa nguvu kuwanasa wahusika na kuwafikisha katika mikono ya dola.
Alisema daktari huyo alitekwa na watu wasiojulikana hadi katika msitu wa pande ambako alipigwa hadi kupoteza fahamu na baadaye kuokolewa na msamari
Nchimbi asema serikali haihusiki
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi amesema kuwa serikali haihusiki na wala haijatoa maelekezo ya kumshambulia Ulimboka.
Aliahidi kuwa itafanya uchunguzi wa nguvu kuwanasa wahusika na kuwafikisha katika mikono ya dola.
Alisema daktari huyo alitekwa na watu wasiojulikana hadi katika msitu wa pande ambako alipigwa hadi kupoteza fahamu na baadaye kuokolewa na msamari
‘Madudu’ Wizara ya Fedha
*Katibu Mtendaji PPAA akalia
ofisi miaka 8 kinyume
Na Edson Kamukara
KATIBU Mtendaji wa
Mamlaka ya Rufaa za Zabuni za Umma (PPAA), Bertha Grace Malambugi, anatumikia
wadhifa huo kwa uteuzi batili kwa mujibu wa sheria za Manunuzi ya Umma, uchunguzi
wa Tanzani Daima imebaini.
Malambungi ambaye alikuwa
Mhadhiri wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IMF) jijini Dar es Salaam, alianza
kuongoza chombo hicho tangu mwaka 2001 na kasha kupandishwa cheo na kuteuliwa
kuwa Katibu Mtendaji wa Mamlaka hiyo mwaka 2004.
Uchungizi wa Tanzania
Daima ulibaini kuwa Malambugi aliteuliwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya
Fedha kwa wakati huo, Gray Mgonja kwa barua yenye kumb: Na. C/JA 26/425/01 ya
Novemba 2, 2004.
Hata hivyo, uteuzi wake
huo ulikiuka sheria ya mamlaka hiyo ya mwaka 2004 kifungu cha 2 (c) na
marekebisho yake ya mwaka 2011 kifungu 89 (1) kwa vile Sheria ya Ununuzi wa
Umma ya mwaka 2001, ilifutwa sheria ya ununuzi wa umma ya mwaka 2004 ambayo
ilianza kutumika mwaka 2005.
Kabla ya mabadiliko hayo,
mamlaka ya uteuzi wa Katibu wa PPAA yalikuwa kwa Waziri wa Fedha lakini baada
ya hapo alipewa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,
hivyo Malambugi ameendelea kushikilia wadhifa huo bila uteuzi wake
kuthibitishwa na Rais kama sheria inavyosema.
Vyanzo vyetu vya habari vinabainisha
kuwa watendaji wenzake katika taasisi zilizoanzishwa chini ya sheria ya ununuzi
wa umma ya mwaka 2004 kama vile Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi
wa Umma (PPRA), walifanya jitihada kuhakikisha uteuzi uliofanywa kwa sheria ya
mwaka 2001 unapata baraka na kuhalalishwa na Rais.
Alipotakiwa kufafanua
utata wa uteuzi wake, Malambugi alisema kuwa habari hizo ziko kwa Katibu Mkuu
wa Wizara ya Fedha, kwani ndiye mwenye mamlaka ya kujua kama
una shida au hapana.
“Hata kama uteuzi wangu
una utata mimi ningefanyaje, siwezi kuhoji mamlaka ya uteuzi, wewe kama unaona kuna makosa yalifanyika watafute wahusika
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na wengine waliopelekewa nakala za barua yangu,”
alisema Malambungi.
Tanzania Daima ilimtafuta
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhan Khijja, ambaye alikiri utata wa uteuzi
wa Katibu Mtendaji huyo na kusema kuwa wanaliangalia jambo hilo ili kupata ushauri wa kisheria.
“Nimezungumza naye nikiwa
Dodoma baada ya wewe kumpigia simu, hivyo jambo hilo tunaliangalia kupata ushauri wa wanasherika maana alianza
kabla ya sheria kubadilishwa sasa tunasubiri tuone watasemaje kama jina lake lipelekwe
kwa Rais au namna gani.
Khijja alifafanua kuwa
kwa vile sheria ilikuja ikakuta tayari Malambugi ameteuliwa, hivyo kisheria
yeye kama katibu mkuu hawezi kulitolea uamzi,
hivyo wanasubiri kuona Mwanasheria Mkuu atasemaje.
PPAA ilianzishwa kwa
sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2001 (sheria Na 3) chini ya Wizara ya Fedha
kama chombo huru cha kusikiliza malalamiko
kutoka kwa wazabuni.
Mramba, Yona kujibu mashitaka
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imewaona aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba,
Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu mkuu wa zamani wa
Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja wana kesi ya kujibu katika shauri la
matumuzi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya
sh bilioni 11.7
Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Sam Rumanyika anayesaidiwa
na Jaji John Utamwa na Saul Kinemela alisema jopo lao
baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi 12 walioletwa na upande wa Jamhuri
uliokuwa ukiwakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali marehemu Stanslaus Boniface,
Ben Lincoln wa Takukuru na vielelezo17 mahakama imewaona washitakiwa wote wana
kesi kujibu.
Jaji Rumanyika alisema kutoka na uamuzi wao washitakiwa wote
sasa watapata fursa ya kujitetea ili mahakama nayo isikie utetezi wao.
Jaji Rumanyika aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 22,mwaka huu, ambapo
siku hiyo washitakiwa wote wataanza kujitetea.
Siri vifo vya Wahabeshi 42 yajulikana
Na Martin Malera, Dodoma
SIRI ya vifo vya raia wa Ethiopia 42 waliofariki dunia kwa kukosa hewa kwenye roli la mizigo wakisafiria kwenda nchini Malawi, imejulikana.
Habari ambazo gazeti hili imezipata kutoka kwa majeruhi wa tukio hilo, zilisema kuwa waliopoteza maisha walikosa chakula baada ya kukaa kwenye gari kwa miezi mitatu mfululizo.
Mmoja wa majeruhi 72 walionusurika, aliliambia gazeti hili kuwa tangu walipoanza safari hadi siku waliyokutwa kwenye roli wilayani Kongwa, Dodoma walikuwa wamemaliza miezi mitatu wakiwa wameishiwa chakula walichohifadhi.
Alisema wametumia muda huo kwani walikuwa wakisafiri kwa kutumia njia za polini ambazo haziwezi kulifanya gari likimbie.
"Tulikuwa tunapita porini, hakuna barabara na mara nyingi tulisafiri usiku na mchana tunaegesha gari kusubiri giza ndo maana hadi jana tulipokamatwa tulikuwa na miezi mitatu," alisema.
Habari zaidi kutoka katika hospitali ya mkoa wa Dodoma zilikohifadhiwa maiti hizo, zilisema kuwa miili yao imeanza kuharibika kutokana na uwingi wa maiti ambao hauendani na uwezo wa kuhifadhi.
Kwa sasa vyombo vya usalama vina msaka wakala anayehusika na biashara ya kuwasafirisha wahamiaji haramu ambaye anadaiwa kuwa yupo nchini Kenya.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk. Emmanuel Nchimbi alisema kuwa serikali inafanya mawasiliano na ofisi ya ubalozi wa Ethiopia nchini Kenya kwani hapa nchini hawana ofisi.
Taratibu za mazishi ziko chini ya ubalozi wa Ethiopia na serikali inaendelea kufanya mawasiliano kupatia ufumbuzi suala hili
Raia 45 wa Ethiopia walikutwa wamekufa na wengine 72 kuwa taabani baada ya kukosa hewa katika lori walilokuwa wakisafiria kwenda Malawi.
Maiti za watu hao na wenzao ambao wako katika hali mbaya, waligundulika juzi asubuhi katika msitu wa Chitego wilayani Kongwa, Dodoma.
Usafirisha watu hao umekuwa mchezo wa kawaida kwani Watanzania wanadaiwa kuwa ndio wanaosaidia kuwasafirisha.
Polisi Tarime iache
kuvuruga wananchi
KATIKA ukurasa wa mbele wa gazeti hili, kuna habari
ya vurugu zilizozushwa jana na Jeshi la Polisi kwenye Kanda Maalumu ya Tarime
na Rorya mkoani Mara.
Chanzo cha vurugu hizo kilielezwa kuwa ni baada ya
jeshi hilo kutumia nguvu na kuwatisha kwa silaha wananchi waliokuwa
wakiomboleza msiba wa Mgosi Magasi Chacha, aliyeuawa na askari kwa kupigwa
risasi juzi katika mgodi wa North Mara.
Kwamba polisi hao waliokuwa wamejazana kwenye
magari wakiwa na silaha, walizingira hospitali ya wilaya hiyo wakitaka
kuuchukua kwa nguvu mwili wa Chacha ili kwenda kuuzika.
Licha ya ndugu wa marehemu wakiongozana na mkewe na
wananchi wengine, kujaribu kuwazuia askari hao wasiuchukue mwili huo, wakitaka
taratibu za kisheria zifuatwe juhudi zao ziligonga mwamba.
Tunawapa pole ndugu wa marehemu Chacha pamoja na
wafiwa wote walioguswa na msiba huo, lakini tunalaani vikali hatua ya Jeshi la
Polisi kutumia mabavu kuuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuuzika wakati
ndugu zake wapo.
Tunasema hivyo tukiwa bado na kumbukumbu za jeshi
hilo mwishoni mwa mwaka jana kuwaua kwa kuwapiga risasi raia watano na kisha
kuvamia hospitali wakitaka kuchukua miili ya marehemu kwa madai ya kwenda
kuizika.
Hata hivyo, miili hiyo baadaye ilikutwa
imetelekezwa vichakani ikiwa kwenye majeneza, jambo ambalo lilizidisha hasira,
simanzi kwa wafiwa na hivyo vurugu kubwa kuzuka.
Sisi tunahoji ni lini Jeshi la Polisi limepata
jukumu la kuwaua wahalifu na kuwazika kwa nguvu wakati familia zao ziko tayari
kuwachukua na kuwazika kwa heshima?
Matukio haya yameanza kujirudia mkoani Mara pasipo
viongozi wakuu kutoa kauli za kuyakemea, hatua inayoashiria kuwa wanakubaliana
nayo.
Maana inashangaza kuona askari wanampiga risasi na
kumuua mtuhumiwa wa wizi halafu hao hao kabla ya hata uchunguzi kufanyika
kuthibitisha kama aliyeuawa alikuwa mwizi kweli, wanakimbilia kumzika kwa
nguvu. Je, huku si kutaka kuficha ukweli?
Na hata katika mila na tamaduni zetu za Kiafrika,
maiti huwa inazikwa kwa heshima zote kulingana na taratibu za jamii husika,
ndiyo maana wanafamilia wanaachiwa kusimamia jukumu hilo. Sasa ubabe huu wa
polisi mkoni Mara unalenga kuwataka wananchi hao wafanyeje?
Maana lazima ieleweke kuwa hata kama aliyeuawa
alikuwa mwizi, bado ndugu zake wana haki zote za kuchukua mwili wake na
kuhifadhi tayari kwa mazishi vyovyote vile watakavyo.
Tunaamini kuwa Jeshi la Polisi mkoani Mara na
uongozi wa kitaifa watajitathimini na kujirekebisha, na hivyo kujiepusha na
vurugu zisizo za lazima, zinazotokana na ubabe wao wa kuzingira hospitali kwa
nia ya kuwapora wafiwa maiti za ndugu zao ili wakazizike kwa nguvu.
Mwisho
Shinikizo la POAC lamrejesha Mbajo
Na Betty Kangonga
MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za
Mashirika ya Umma (POAC), Zitto Kabwe amesema kuwa kamati hiyo iliamua
kutopitia taarifa za hesabu ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) hadi
pale Mkurugenzi wake, Methusela Mbajo, atakaporudishwa katika nafasi yake.
Mbajo
alisimamishwa mwishoni mwa mwaka jana kupisha uchunguzi ndani ya CHC ulitokana
na maombi ya Bodi ya shirika hilo
baada ya kuwapo tuhuma kwamba menejimenti yake ilihusika na vitendo vya
ufisadi.
Akizungumza na waandishi wa habario jana jijini
Dar es Salaam, Zitto alisema kuwa kamati ililazimika kutopitia na kujadili
taarifa za CHC hadi pale Mbajo atakaporudishwa kazini kutokana na uchunguzi wa
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kutomkuta na makosa.
“Tulikubaliana kama kamati kwanza Mbajo
arudishwe katika nafasi yake...wakitekeleza hilo
ndipo sasa warudi kwa ajili ya kupitia taarifa yao ,” alisema.
Zitto ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini,
alisema kuwa CHC wameweza kutekeleza agizo hilo na jana wamemrejesha kazini mkurugenzi
huyo.
Alisema ripoti ya hiyo inatarajiwa kujadiliwa Juni
6 mwaka huu, kabla ya kuanza kwa kikao
cha Bunge.
Katika mkutano wa nne wa Bunge ambao ulishuhudia
mvutano, Zitto aliapa kuwa kama ingebainika alihongwa yeye au wajumbe wake wa
POAC, angejiuzulu na kumtaka aliyekuwa Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo naye ale
kiapo kama hicho, lakini aligoma.
Mkapa asema niacheni
Na Grace
Macha, Arusha
RAIS
Mstaafu Benjamin Mkapa, jana alisema kwa sasa hataki kusumbuliwa kwa namna
yoyote, badala yake ameomba aachwe huru ili ashughulikie matatizo aliyonayo.
Bila
kutaja aina ya matatizo hayo, Mkapa alikataa kuzungumza na waandishi wa habari
akidai kuwa hataki kuongeza matatizo mengine, kwa vile aliyonayo kwa sasa
yanamtosha.
Mkapa
alitoa kauli hiyo baada ya kuombwa na kundi la waandishi wa habari mara baada ya
kutoka kwenye mjadala maalum kuhusu uboreshaji wa mazingira ya uwekezaji barani
Afrika, ulioandaliwa na Taasisi ya Uwezeshaji na Uwekezaji (ICF).
Waandishi
walitaka kufanya mahojiano na Rais huyo mstaafu kuhusiana na mambo kadhaa yakiwemo
aliyozungumza katika mkutano huo, ambayo yalikuwa mazito na ‘mwiba’ kwa watawala
wengi wa serikali barani Afrika.
“
Niacheni , nina matatizo yangu ya kunitosha, sitaki kuongea kwa sasa” alisema na
kisha akaondoka.
Rais
Mstaafu Mkapa amekuwa akishambuliwa na viongozi mbalimbali wa siasa kwa madai
ya kuuza mashirika ya umma, kutumia wadhifa wake na kujimilikisha kampuni ya
uchimbaji madini, akishirikiana na baadhi ya waliyokuwa mawaziri katika
serikali yake.
Baadhi
ya wanasiasa wamekuwa wakipendekeza rais huyo wa zamani akamatwe kwa kuhusika
na tuhuma za ufisadi, kama ilivyofanywa kwa
baadhi ya mawaziri wake wa zamani kwa tuhuma za ubadhilifu.
Mkapa
aliingia hivi karibuni katika mzozo mzito na familia ya Baba wa Taifa Mwalimu
Julius Nyerere, baada ya kukaririwa akisema Mbunge wa Musoma, Vicent Nyerere
(Chadema) hakuwa mtoto wa Mwalimu, kauli aliyoitoa wakati wa kampeni ya
uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wakati akimnadi mgombea wa CCM,
Sioi Sumari
Mapema
akizungumza katika mjadala uliohudhuriwa na washiriki toka makampuni na taasisi
mbalimbali za bara la Afrika, Mkapa alisema alifanikiwa wakati wa utawala wake
kutokana na sera yake ya uwazi na ukweli, na pia kujikita katika utekelezaji wa
mipango.
Alisema
sio vema kwa viongozi wa nchi za Afrika
kuzungumzia mipango na mikakati ya maendeleo kila kukicha, badala yake
waingie kwenye utekelezaji.
Alisema
kuwa sera yake ya uwazi na ukweli ilisaidia kuwapa wananchi taarifa sahihi
kuhusu hali ya uchumi, fedha na changamoto zote zilizoikabili Serikali na wao
kupata fursa ya kushiriki kuzitafutia ufumbuzi.
Mkapa
alisisitiza umuhimu wa serikali za Afrika kuwawezesha kiuchumi wanawake na
vijana waweze kujiajiri kwa kuwa hayo ndio makundi makubwa kuliko makundi
mengine katika jamii hivyo itaziwezesha nchi hizo kupiga hatua za kimaendeleo
kwa haraka na kukabiliana na tatizo la umaskini wa kipato.
Alisema
kuwa tatizo la ajira limesababisha vijana wengi kughiribiwa na wanasiasa ambao
huwapa matumani hewa ya mafanikio, na wengi kuamini kuwa njia sahihi ya
kujinanusa ni kujiingiza katika siasa
Kwa upande wake, Mtendaji
Mkuu wa ICF, Omary Issa alisema taasisi hiyo imefanikiwa kuboresha mifumo mbalimbali inayopunguza usumbufu kwa
wafanyabiashara na wawekezaji huku akitolea mfano wa mpango kuboresha mfumo wa
usafirishaji mizigo kutoka bandarini mpaka nchi jirani wanaoutekeleza kwa
pamoja na mamlaka ya mapato nchini TRA na Jeshi la polisi ambao utawezesha
kuondoa vizuizi vyote vya kodi barabarani.
Alisema kuwa ICF
imesaidia kuboresha mfumo wa usajili wa makampuni nchini Rwanda ambapo
kwa sasa huchukua siku 2 kusajili biashara tofauti na awali ambapo ilikuwa
mpaka siku 16 huku gharama zikipungua kutoka dola za Marekani 433 mpaka 25.
Issa alisema kuwa taasisi
yake katika kuhakikisha shughuli za biashara zinafanyika kwa urahisi na ufanisi
zaidi imesaidia kuboresha mfumo wa mahakama nchini Zambia kwenye mahakama 3 na
kutoa mafunzo kwa majaji wapya 14 huku nchini Sierra Leone wakifanikiwa
kuboresha mfumo wa mahakama ambapo kwa sasa huchukua miezi miwili tokea
kufungua kesi za biashara na kupata uamuzi ambapo awali ilikuwa inatumia mpaka
miaka sita.
Chadema yaiumbua CUF
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimegeuza mashambulizi yake na safari hii kimekishutumu Chama cha wananchi (CUF) kwa kile walichosema kuwahadaa watanzania kiasi cha kuaminika kuwa ni wapinzani wa kweli.
Mbowe akifungua tawi la chadema katika eneo la Mihuta
wilayani Tandahimba alisema mwanzoni walidhani CUF kilikuwa na dhamira ya kweli
ya kuwakomboa wananchi na ndiyo maana waliwaachia mikoa ya kusini kwa ajili ya
kuendeleza kazi hiyo.
Aliongeza kuwa dalili za wazi za CUF kushindwa kuwatumikia watu wa kusini zimeonekana wazi baada ya kuamua kufunga ndoa ya mkeka baina yake na ccm.
“Ninachoweza kuwaambia wana Mihuta ni kwamba Chadema, CUF na CCM si baba yenu wala mama yenu nakama mtaona vyama hivi
haviwasemei achaneni navyo, na kwa kuwa Cuf na CCM mlishawapa dhamana hiyo
wakashindwa mviache sasa”alisema.
Aliongeza kuwa dalili za wazi za CUF kushindwa kuwatumikia watu wa kusini zimeonekana wazi baada ya kuamua kufunga ndoa ya mkeka baina yake na ccm.
“Ninachoweza kuwaambia wana Mihuta ni kwamba Chadema, CUF na CCM si baba yenu wala mama yenu na
Mbowe, amewataka wananchi wa wilaya ya Tandahimba
kuihukumu serikali ya CCM kwa vile haitetei maslahi ya watanzania hususan
wakazi wa Tandahimba na sasa inatumia mabavu kuwatisha hata katika haki
zao za msingi hususan pale wanapodai kulipwa kulingana na nguvu zao
zilizotumika
“Jamani Tanzania inasifika kwa kutajwa kuwa nchi inayofuata haki na sheria za binadamu lakini leo wanatandahimba mnapigwa mabomu na askari
wanaotumia kodi zenu kwa ajili ya kudai fedha za korosho ambazo kwa makusudi serikali imeamua kuwakopa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani” alisema Mbowe
Alibainisha kuwa hakuna haja ya wakazi wa Tandahimba na Mtwara kwa ujumla kwa kulazimishwa mazao yao kuuzwa kupitia stakabadhi ghalani wakati mikoa mingine haifanyiwi hivyo na wanauza mazao kwa matajiri wanaowataka na bei wanayoitaka
Dk Slaa atoboa siri ya CUF
“Jamani Tanzania inasifika kwa kutajwa kuwa nchi inayofuata haki na sheria za binadamu lakini leo wanatandahimba mnapigwa mabomu na askari
wanaotumia kodi zenu kwa ajili ya kudai fedha za korosho ambazo kwa makusudi serikali imeamua kuwakopa kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani” alisema Mbowe
Alibainisha kuwa hakuna haja ya wakazi wa Tandahimba na Mtwara kwa ujumla kwa kulazimishwa mazao yao kuuzwa kupitia stakabadhi ghalani wakati mikoa mingine haifanyiwi hivyo na wanauza mazao kwa matajiri wanaowataka na bei wanayoitaka
Dk Slaa atoboa siri ya CUF
Naye Dk Slaa alitoboa siri ya namna CUF kilivyoamua kuwa
sehemu ya utawala, baada ya kufichua barua mbili zikiomba fedha kwa ajili ya
kuhudumia chama na safari za kifamilia za Makamu wa Kwanza
wa Rais Zanzibar.
Alisema barua ya kwanza ya Katibu Mkuu wa Cuf Maalimu Seif kwenda serikalini inaomba kuwezeshwa kufanyika kwa mkutano wao chama kwa siku tatu katika eneo la Bagamoyo kwa gharama za sh. milioni 34.
Dk Slaa alisema barua ya pili ni ile inayoomba dola za kimarekani 10,000 kwa ajili ya nauli ya kwenda Nairobi Kenya kwa mke wa Maalim Seif kwa safari ya
kifamilia, ikiwa ni sawa na dola 1,000 kwa siku.
Aidha Dk Slaa alisema katika taarifa hiyo inaonyesha pia kuna fedha za dharura kwa ajili ya matumizi ya makamu wa Rais ambayo ni dola 3000 na kudai kuwa huo ni ufisadi usioweza kuvumiliwa na wapenda haki.
Alisema kwa mfumo huo wa CUF kutegemezi hata katika mikutano yake ya chama fedha za serikali, ni ushahidi wa wazi wazi kuwa inafanya kila kitu kwa kuongozwa na
serikali ya ccm.
Alisema barua ya kwanza ya Katibu Mkuu wa Cuf Maalimu Seif kwenda serikalini inaomba kuwezeshwa kufanyika kwa mkutano wao chama kwa siku tatu katika eneo la Bagamoyo kwa gharama za sh. milioni 34.
Dk Slaa alisema barua ya pili ni ile inayoomba dola za kimarekani 10,000 kwa ajili ya nauli ya kwenda Nairobi Kenya kwa mke wa Maalim Seif kwa safari ya
kifamilia, ikiwa ni sawa na dola 1,000 kwa siku.
Aidha Dk Slaa alisema katika taarifa hiyo inaonyesha pia kuna fedha za dharura kwa ajili ya matumizi ya makamu wa Rais ambayo ni dola 3000 na kudai kuwa huo ni ufisadi usioweza kuvumiliwa na wapenda haki.
Alisema kwa mfumo huo wa CUF kutegemezi hata katika mikutano yake ya chama fedha za serikali, ni ushahidi wa wazi wazi kuwa inafanya kila kitu kwa kuongozwa na
serikali ya ccm.
Mgeja awashukia wasomi
Na
Mwandishi wetu, Kahama
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Shinyanga na
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicvho, Hamis Mngeja amewashukia wasomi hapa
Nchini kwa kuendekeza mambo ya semina, makongamano,warsha pamoja na tafiti
mbalimbli huku wakiicha nchi ikiendelea kudidimia kiuchumi.
Mngeja
ambaye pia ni Kaimu Mwenyekiti wa Shirika lisilo la Kiserikali la Mzalendo
Foundation, aliliambia Tanzania Daima kuwa baadhi wasomi wameshindwa kutumia utaalamu wao kulisaidia
taifa hususan kuinua maisha ya wakulima ambao sasa wanakandamizwa.
Alisema
mfumo wa bei za mazao ya wakulima katika masoko hauelweki na kusababisha
kuyumba kwa bei ya mazao kila wakati na kusababisha mkulima badala ya kunufaika
na bei inamdidimiza.
Mgeja
alimwomba Waziri wa Kilimo Christopher Chiza kusikia kilio cha wakulima
wa mazao hususan yale ya Biashara ambayo yamekumbwa na mtikisiko wa kuporomoka
kwa bei mara kwa mara.
Aliitaka
Serikali kujielekeza katika kulinda viwanda
na kutumia malighafi za ndani badala ya kupeleka nje ya nchi jambo
linalowanufaisha mataifa mengine.
Alisema
kuwa ikiwa taifa litawekeza kwa wingi katika viwanda vya ndani uchumi wa nchi
utakuwa imara na thamani ya kilimo itapanda na kupendwa na kila mtu kwa sababu
ndio njia pekee anayoamini itawasaidia wananchi kuondokana na umasikini
walionao.
Mwisho
Kesi ya mauji ya mtoto wa Fundikila yaiva
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Juni 4-8
itaanza kusikiliza kesi ya mauji ya mtoto wa Chifu Abdallah Fundikila, Swetu
Fundikila inayowakabili MT 1900 Sajenti Roda Robert(42) wa Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT) Kikosi cha Mbweni na wenzake.
Kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya uendeshaji wa
kesi za Mahakama Kuu ambayo gazeti hili imeiona nakala yake, kesi hiyo
imepangwa kusikilizwa na Jaji Zainabu Mruke na jumla ya mashahidi tisa wa
upande wa jamhuri watoa ushahidi katika kesi hiyo.
Mbali na Dorisi washtakiwa wengine ni MT
75854 Koplo Ally Ngumbe (37) wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Kikosi cha Kunduchi na
MT 85067 Koplo Mohamed Rashid wa JKT Mbweni.
Wakili wa serikili Dionisia Saiga awali alidai
mahakamani hapo kuwa Januari
23 mwaka 2010 kuanzia majira ya saa 6 usiku, kuwa marehemu akiwa na
wenzake wawili wakitumia gari aina ya Toyota Corolla, wakitoka Mwananyamala
walikutana na washtakiwa wakiwa kwenye gari lao wakitokea kwenye maegesho ya magari
ya Baa ya Mango Garden .
Wakili
Saiga alidai kuwa mshtakiwa wa kwanza alimwamuru dereva wa gari alilokuwemo
marehemu, arudi nyuma na kwamba dereva huyo alitii.Alidai kuwa washtakiwa
walilifuata gari hilo na kusimama pembeni na baadaye mshtakiwa wa kwanza
alishuka na kumfuata dereva na kumuonya kuwa siku nyingine asipowaheshimu
viongozi wa nchi atapata shida.
Aliendelea kudai kuwa baada ya hapo marehemu na wenzake waliondoka lakini walipofika kwenye makutano ya Barabara ya Kawawa na MwinyiJuma, walikutana tena na washtakiwa ndipo mshtakiwa wa kwanza akawatukana.
Alidai kuwa marehemu aliuliza sababu ya kuwatukana bila kosa, lakini mshtakiwa wa kwanza alimpiga dereva, jambo lililomlazimisha marehemu kuingilia kati kuamlia.
Aliendelea kudai kuwa baada ya hapo marehemu na wenzake waliondoka lakini walipofika kwenye makutano ya Barabara ya Kawawa na MwinyiJuma, walikutana tena na washtakiwa ndipo mshtakiwa wa kwanza akawatukana.
Alidai kuwa marehemu aliuliza sababu ya kuwatukana bila kosa, lakini mshtakiwa wa kwanza alimpiga dereva, jambo lililomlazimisha marehemu kuingilia kati kuamlia.
mwisho
Vurugu Z’ bar zina mkono wa vigogo
Betty Kangonga na Asha Bani
KANISA la Pentekoste Tanzania limedai kuwa vurugu zilizotokea
visiwani Zanzibar na kusababisha uharibifu
mkubwa wa mali ,
zina msukumo wa baadhi ya viongozi wa siasa na dini.
Kiongozi mkuu wa Kanisa hilo , William Mwamalanga
aliliambia Tanzania Daima jana kuwa baadhi ya viongozi wa siasa wanaouchukia
Muungano, na wale wenye malengo ya kidini waliwatumia vijana kufanya vurugu
hizo.
‘Kuna siri nzito iliyojificha katika vurugu hizo. Wapo baadhi ya viongozi nyuma ya vurugu hizo kwani muungano umetumiwakama
kigezo.
‘Kuna siri nzito iliyojificha katika vurugu hizo. Wapo baadhi ya viongozi nyuma ya vurugu hizo kwani muungano umetumiwa
‘Chokochoko za muungano
hazijaanza leo wala jana maana tunafahamu wazi kuwa wapo baadhi ya viongozi
ambao wamekuwa wakiupinga muungano huo ndani ya Bunge na hata nje hivyo imefika
wakati kwa watawala wetu kuwa wakweli juu ya suala hilo ,’ alisema.
Mchungaji huyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya kupambana na dawa za kulevya, alisema kuwa kauli za baadhi ya viongozi zinazotolewa juu ya sualahilo zimekuwa chachu za
vurugu hizo.
Alidai kuwa anaamini matatizo ya muungano haytamalizwa kwa kupatikana katiba Mpya bali kinachopaswa ni viongozi wanaofahamu umuhimu wa sualahilo kuweka wazi kwa
wananchi ili waweze kuujua kwa undani.
‘Watawala wawaeleze vijana umuhimu wa sualahilo
hata kama kuna mchakato wa katiba mpya bado
itakuwa shida kwa kuwa vijana hawaelewi ulazima wa ushirikiano huo,’
alifafanua.
Alisema watawala wanapaswa waandae kipindi maalum ili kuujadili muungano huo na sio maana kwa sasa sualahilo limevuka mipaka na
kutumiwa kama kigezo cha uhalifu na uvunjifu
wa amani.
Hata hivyo alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema kupata muda na kukutana na wazee wa visiwa hivyo pamoja na viongozi wa kisiasa ili kutafuta suluhu ya kudumu juu ya sualahilo .
Mchungaji huyo ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya kupambana na dawa za kulevya, alisema kuwa kauli za baadhi ya viongozi zinazotolewa juu ya suala
Alidai kuwa anaamini matatizo ya muungano haytamalizwa kwa kupatikana katiba Mpya bali kinachopaswa ni viongozi wanaofahamu umuhimu wa suala
‘Watawala wawaeleze vijana umuhimu wa suala
Alisema watawala wanapaswa waandae kipindi maalum ili kuujadili muungano huo na sio maana kwa sasa suala
Hata hivyo alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Said Mwema kupata muda na kukutana na wazee wa visiwa hivyo pamoja na viongozi wa kisiasa ili kutafuta suluhu ya kudumu juu ya suala
Utalii haujavurugwa
Katika
hatua nyingine, serikali imesema vurugu zilizotokea Zanzibar
haikuathiri soko la utalii kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari vya Kenya
na katika mitandao ya kijamii.
Akizungumza
na Waandishi wa Habari jana, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro
Nyalandu, alisema mitandao na vyombo hivyo vinalenga havikusema ukweli na
vinalengo la kuichafua Tanzania .
Alisema
hali ya amani katika mji Mkongwe imetulia
na kwamba hakuna taarifa zozote za uharibifu wa maeneo ya vivutio vya
utalii wala kuchmwa kwa hoteli yeyote ya kitalii mjini humo.
“Serikali
inawahakikishia wananchi na jumuiya ya kimataifa kuwa hayo yalikuwa matukio ya
kipekee nay a kupita na hatua zimechukuliwa na Jeshi la Polisi kuongeza usalama
kwa wakazi na watalii,”alisema Nyalandu.
Hata
hivyo alikiri kuwepo kwa matukio ya kuporwa kwa watalii na vibaka ambapo hivi
karibuni watalii wanne wamefanyiwa vitendo hivyo katika maeneo ya Masaki jijini
Dar es Salaam
ambao yamefanywa na watu waliotumia magari na pikipiki.
Hivi
karibuni katika mji wa Zanzibar
kumetokea na vurugu zilizopelekea kuchomwa kwa makanisa pamoja na shule jambo
ambalo viongozi mbalimbali wa serikali na wa kidini wametoa tamko.
Mwisho.
Slaa amlipua Waziri Ghasia
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema (Chadema) Dk Willbroad
Slaa amemtaka Mbunge wa Mtwara vijijini Hawa Ghasia kuacha kutisha na kuwakamata wananchi wanaomuuliza maswali katika mikutano ya hadhara akidai amekashifiwa.
akihutubia umati wa wananchi katika Kata ya Mtimbwilimbwi na Nanyamba, Slaa alisema ni uvunjaji wa sheria na ubabe kukamata wananchi waliowapigia kura.
Slaa
alisema hayo baada ya wananchi kumwelezea kuwa wamekuwa wakikamatwa na viongozi
wa Serikali na CCM wanapouliza maswali, ndio maana wameingiwa woga.
Alisema Waziri Ghasia anafanya vitendo hivyo kwa kuwa ana uhakika wa kutogombea tena ubunge katika jimbo la Mtwara vijijini baada ya kutambua kuwa hawezi tena kushinda
Alisema Waziri Ghasia anafanya vitendo hivyo kwa kuwa ana uhakika wa kutogombea tena ubunge katika jimbo la Mtwara vijijini baada ya kutambua kuwa hawezi tena kushinda
Slaa
alisema maisha ya wakazi wa Mtwara vijijini na umasikini unaowazunguka ni aibu kwa
uongozi katika miaka 50 ya uhuru, ambapo akina mama wajawazito wanalazimika
kwenda hospitali wakiwa na vifaa.
“Enzi za Mwalimu Nyerere hakukuwa na sualahilo leo hata mtoto mdogo anajua kuwa mama
yake anakaribia kujifungua kwa kuwa ni lazima atakuwa anahangaika kutafuta
vifaa vya kujifungulia.”alisema Dk Slaa
Alibainisha kuwa jimbo la Karatu ambalo wananchi wake hawakuwahi kuwa na waziri kwa miaka 15 sasa wanafikiria kuingiza maji ndani ya nyumba zao wakati Mtwara vijijini ambayo Mbunge wake ni waziri wananchi wanatafuta maji umbali wa zaidi ya kilometa 10 kufuata maji.
Katika hatua iliyoonesha kukithiri kwa umasikini, Dk Slaa alilishwa supu ya ngozi ya ng’ombekama kitoweo, ambapo walidai
wamefanya hivyo kwa kuwa hawana uwezo wa kununua nyama.
walisema hata hizo ngozi ni lazima aende mtu kuzifuata Mtwara mjini na siku inapokosekana wanajihesabiakama wamekosa
nyama halisi
Kufuatia hali hiyo Dk Slaa aliwataka wananchi wa Mtwara mjini
kujiepusha na kuuza uhuru wao kwa gharama ya shilingi elfu tano na badala yake wasimamie ukombozi wa kweli
“Enzi za Mwalimu Nyerere hakukuwa na suala
Alibainisha kuwa jimbo la Karatu ambalo wananchi wake hawakuwahi kuwa na waziri kwa miaka 15 sasa wanafikiria kuingiza maji ndani ya nyumba zao wakati Mtwara vijijini ambayo Mbunge wake ni waziri wananchi wanatafuta maji umbali wa zaidi ya kilometa 10 kufuata maji.
Katika hatua iliyoonesha kukithiri kwa umasikini, Dk Slaa alilishwa supu ya ngozi ya ng’ombe
walisema hata hizo ngozi ni lazima aende mtu kuzifuata Mtwara mjini na siku inapokosekana wanajihesabia
Kufuatia hali hiyo Dk Slaa aliwataka wananchi wa Mtwara mjini
kujiepusha na kuuza uhuru wao kwa gharama ya shilingi elfu tano na badala yake wasimamie ukombozi wa kweli
Mbowe kumbana Waziri Mkuu
Akizungumza
katika mkutano aliyoifanya katika kata za Madimba na Tangazo, Mwenyekiti wa
Taifa wa Chadema Freeman Mbowe amesema kuanzia sasa atakuwa msemaji wa wakazi
wa mkoa wa Mtwara kwa kuwa hawana msemaji wa shida zao hususan zao la korosho
na gesi.
Alisema akifika bungeni swali lake la kwanza kwa waziri mkuu ni kumuuliza serikali ya CCM inatumia sera gani kuchimba gesi katika mkoa wa Mtwara.
Mbowe alishangazwa na kitendo cha serikali kuweka nguzo za umeme katika maeneo yenye nyumba za nyasi, na kukiitakama dharau,
na kwamba ilipaswa kwanza kuhakikisha wananchi wake wana nyumba bora.
Wenje amvaa Mbatia
Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje (Chadema) amemshambulia Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha Nccr Mageuzi, James Mbatia akidai amefungishwa ndoa ya mkeka na CCMapinduzi, kwa kupewa ubunge
wa Viti Maalum na Rais Jakaya Kikwete ili kumsaidia kutekekeza ilani isiyotekelezeka.
Akizungumza na wananchi wa kata ya Majengo katikati ya mji wa Mtwara juzi,Wenje alisema kitendo cha Mbatia kukubali ubunge wa viti maalum
kimeonyesha udhaifu wake mkubwa kwamba sio mpinzani wa kweli wa kupinga ufisadi na ubadhirifu unaofanywa na Serikali ya CCM.
Hatua hiyo ya Wenje kumuita mbatia mbunge wa viti maalum iliibua mvutano katika mkutano huo baada ya makundi ya watu kutofautiana wengine wakisema hata Chadema kuna wabunge wa viti maalum
Kutokana na mabishano hayo ilimlazimu Wenje mwisho wa mkutano kutoa ufafanuzi jinsi wabunge wa viti maalumu wa chama wanavyopoatika na wabunge wanaoteuliwa na rais kwa mujibu wa mamlaka ya ibara ya 66 (1)
(a) ya katiba ya nchi.
“Ndugu zangu hakuna sababu ya kubishana hapa, wapo wabunge wa viti maalum wa chama husika wanaotokana na idadi ya wabunge halali waliochaguliwa kwa kura za wananchi, na wapo wabunge wa kuteuliwa na Rais kwa mujibu wa kifungu hicho,wote ni wabunge lakini tofauti yao ni huyu ni wa Rais na huyu ni wa wabunge.
Alisema akifika bungeni swali lake la kwanza kwa waziri mkuu ni kumuuliza serikali ya CCM inatumia sera gani kuchimba gesi katika mkoa wa Mtwara.
Mbowe alishangazwa na kitendo cha serikali kuweka nguzo za umeme katika maeneo yenye nyumba za nyasi, na kukiita
Wenje amvaa Mbatia
Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje (Chadema) amemshambulia Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha Nccr Mageuzi, James Mbatia akidai amefungishwa ndoa ya mkeka na CCMapinduzi, kwa kupewa ubunge
wa Viti Maalum na Rais Jakaya Kikwete ili kumsaidia kutekekeza ilani isiyotekelezeka.
Akizungumza na wananchi wa kata ya Majengo katikati ya mji wa Mtwara juzi,Wenje alisema kitendo cha Mbatia kukubali ubunge wa viti maalum
kimeonyesha udhaifu wake mkubwa kwamba sio mpinzani wa kweli wa kupinga ufisadi na ubadhirifu unaofanywa na Serikali ya CCM.
Hatua hiyo ya Wenje kumuita mbatia mbunge wa viti maalum iliibua mvutano katika mkutano huo baada ya makundi ya watu kutofautiana wengine wakisema hata Chadema kuna wabunge wa viti maalum
Kutokana na mabishano hayo ilimlazimu Wenje mwisho wa mkutano kutoa ufafanuzi jinsi wabunge wa viti maalumu wa chama wanavyopoatika na wabunge wanaoteuliwa na rais kwa mujibu wa mamlaka ya ibara ya 66 (1)
(a) ya katiba ya nchi.
“Ndugu zangu hakuna sababu ya kubishana hapa, wapo wabunge wa viti maalum wa chama husika wanaotokana na idadi ya wabunge halali waliochaguliwa kwa kura za wananchi, na wapo wabunge wa kuteuliwa na Rais kwa mujibu wa kifungu hicho,wote ni wabunge lakini tofauti yao ni huyu ni wa Rais na huyu ni wa wabunge.
JK Tumepwaya
afichua kisa cha kuachwa Ma-DC
RAIS
Jakaya kikwete amekiri kuwa watanzania wengi wamekosa imani na serikali yake
kwa kile alichodai kuwa kimechangiwa na utendaji mbovu wa baadhi ya watumishi.
Kikwete
ametamka hayo jana, alipokuwa akifunga semina ya mafunzo kwa wakuu wa mikoa na
wilaya iliyokuwa ikifanyika mjini hapa, na kudai kuwa utendaji mbovu wa baadhi
ya watendaji wa serikali yake, umewafikisha wananchi wengi kuichukia serikali
ya Chama Cha Mapinduzi.
Alisema
taifa limekosa kukosa maendeleo kutokana na tabia ya baadhi ya watendaji,
kujihusisha na rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma na uonevu, mambo
ambayo yamewakatisha tamaa wananchi.
Aidha
aliongeza kuwa tabia ya viongozi kuchelewesha maamuzi katika kutatua kero za
watu, zimekuwa zikiwakasirisha wananchi, na kutoboa kuwa ndizo zilizomfanya
kuwaacha baadhi ya waliokuwa wakuu wa wilaya.
Ameongeza
kuwa baadhi ya wakuu hao wa wilaya, waliiuka maadili ya ya utumishi ikiwa ni
pamoja na ulevi uliokithiri.
Kutokana
na hali hiyo, Kikwete aliwaagiza viongozi hao kufanya kazi zao kwa uangalifu,
kutotumia ubabe na kuheshimu mipaka na mgawanyiko wa majukumu yao ya kila siku.
Katika
hatua nyingine, Rais Kikwete amewataka viongozi na watendaji wa serikali
kujiuzulu na kuwaachia vijana wasomi
nafasi hizo ili waweze kutumia elimu yao
kujenga taifa.
Alisema
kuwa ni wakati muafaka kwa wazee kuwapisha vijana, watumie nguvu na elimu yao , na wao wabaki pembeni
wakiwa washauri katika mambo mbalimbali, badala ya kunga’ang’ania madaraka hata
katika umri huo mkubwa.
Semina
hiyo ilikuwa na lengo la kutoa mafunzo kwa wakuu wa mikoa na wilaya, kabla ya
kuanza rasmi kazi zao, kufuatia kuteuliwa kwao na Rais Kikwete hivi karibuni.
Nchimbi aonya vurugu Z’bar
·
30 wapandishwa kizimbani
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi,
ameliagiza jeshi la polisi nchini kumkamata mtu yeyote atakayechochea fujo na
vurugu visiwani hapa bila kujali wadhifa wake.
Akizungumza
na viongozi viongozi mbalimbali wakiwemo wanajumuia za maimamu (Jumaza) pamoja
na mwakilishi wa mabalozi katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani Kilimani,
katika mkutano uliohudhuriwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema.
Nchimbi alisema, watanzania wanahitaji amani ambayo inatakiwa kulindwa na kila
mtanzania.
Nchimbi
ambaye alidai kuridhishwa na kurejea kwa utulivu katika viunga vya mji huu,
alisema serikali haiwezi kamwe kunyamaza na kuwaachia watu wachache wakivuruga
amani na kuhatarisha usalama wa wengi.
Bila
kutafuna maneno, waziri huyo alikiri kutofurahishwa kwake na mwenendo mzima wa
kikundi cha uamsho kinachotuhumiwa kushiriki vurugu kubwa zilizozuka kwa siku
mbili zilizopita.
Alisema
jumuia hiyo, ambayo kwa karibu mwaka mzima wamekuwa wakiitwa na kuonya na polisi
dhidi ya matamshi mbalimbali yaliyolenga kuwagawa watanzania, lakini mara tu
wanapotoka katika meza ya mazungumzo hurejea tena kuhubiri yaleyale, jambo
alilosema sio la kiungwana.
“Hata
katika mikutano na maandamano ya juzi walikuwa na haki ya kufanya maandamano,
na walitakiwa kuomba kibali na kupatiwa ulinzi, jambo ambalo hawakulifanya”
alisema.
Aliwaomba
viongozi wa serikali kushirikiana na kuona wananchio wanarudi katika hali nyao
za zamani na kusisitiza jeshi kutosita kuchukua hatua kwa yeyote akateyevunja
sheria.
Nsaye
sheikh kutoka msikiti wa Amir Tajo, Omar Mohamed Ali , alimtaka waziri huyo
kuangalia kanda za jumuia za uamsho na kuona kama kuna uvunjifu wa amani, na
kudai kuwa juzi walifanya matembezi ya hiyari bila kudhuru mtu, ambapo polisi
walikuwa na habari ya matembezi hayo na badala yake, walimchukua sheikh wao kwa
njia ya kumteka nyara hali iliyozua hisia tofauti kwa wananchi.
Katika
hatua nyingine watu 30 wakiwemo viongozi watatu wa jumuiya ya Uamsho
akiwemo Mussa juma Issa wamepandishwa
kizimbani katika mahakama ya wilaya ya Mwanakwerekwe wakikabiliwa na tuhuma
kukusanyika na kuandamana bila kibali na kufanya fujo
Viongozi
na watu hao hata hivyo, wameachiwa kwa dhamana ambapo upelekezi wa kesi hiyo
bado unaendelea.
Vurugu
kubwa zilizuka juzi mjini hapa ambapo, kundi la watu wanaoaminika kuwa wafuasi
wa Uamsho walifanya ghasia kubwa ikiwemo
kuchoma magari, kushambulia nyumba ambapo kanisa moja la T.A.G Kariako
lilichomwa moto na kuharibiwa vibaya kwa magari ya watu.
Aidha,
katika vurugu hizo, inadaiwa kwamba watu wasiofahamika walianza kusaka nyumba
wanazoishi watu kutoka Tanzania
bara wakitishia kuwauwa.
Marekani yahuzunika
Balozi wa
Marekani nchini, Alfonso Lenhardt, ameeleza kusikitishwa kwake na vurugu
zilizozuka mjini hapa, na amewataka viongozi wa makundi yote kuhakikisha kuwa
wanasimamia amani na utulivu kwa nguvu zote.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya
habari jana, Balozi huyo alisema vurugu hizo zimetia doa amani, umoja na
mshikamano ambao umekuwepo tangu uchaguzi mkuu uliyopita, na kuundwa kwa
serikali ya umoja wa kitaifa.
Amesema ni vema kuchukuliwa kwa hatua madhubuti
kulinda amani kwa kuwa ghasia hizo zitaleta athari kwa uchumi wa nchi na
kuwagopesha watalii na wawekezaji wa kigeni kuingia nchini.
Uamsho yakana kuchoma kanisa
Katika
hatua nyingine, Taasisi za Kiislamu na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya
Kiislamu Zanzibar (JUMIKI), imepinga kuhusika kuhamasisha kufanya machafuko
yaliyotokea mji wa Zanzibar usiku wa Mei 26 na kusababisha kuchomwa moto kanisa
la Tanzania Assemblies of God (TAG) la Kariakoo ikiwa ni pamoja na kuharibu
magari, miundo mbinu na mali nyingine.
Katika
taarifa yake kwa vyombo vya habari imesema; “kama alivyosema Mtume (S.A.W)
katika Hijatul Wadaa, kwamba ni haramu kumwaga damu zenu, kuharibiana mali
zenu, kuvunjiana heshima zenu ila kwa haki ya Uislamu (maana yake pale mtu
anapofanya kosa na likathibitika atahukumiwa kwa hukumu ya Kiislamu). Vile vile
Uislamu unaheshimu nyumba za ibada (Makanisa, Mahekalu na sehemu nyingine za
ibada) zisivunjwe wala zisiharibiwe”.
Jumuia
hiyo ilitoa wito kwa Waislamu na Wazanzibari wote kuendelea kudumisha amani na
utulivu wa nchi na kutoharibu mali za Serikali, mali za Wananchi, Taasisi za
dini zenye imani tofauti, kwani kufanya hivyo ni kwenda kinyume na mafundisho
ya dini ya Kiislamu.
Taarifa
hiyo ilibainisha kwamba matukio hayo wanayachukulia kama njama za makusudi za
wale wasioipendelea amani ya nchi hii, pamoja na kutaka kuipaka matope jumuiya
na kutaka kuzuia lengo la Wazanzibari kudai nchi yao .
“Tunatoa
wito kwa Jeshi la Polisi na vyombo vyote vya Dola wafanye kazi zao kama
wanavyotakiwa kwa mujibu wa muongozo wa haki za binadamu kwa Polisi na vikosi
vingine kwani wana jukumu la kutunza amani na utulivu na jukumu la kutoingilia
haki za watu,” ilisema taarifa hiyo.
Mwisho.
- Makanisa, magari yachomwa moto
- Vita ya mabomu, mawe yalindima
- Raia wa Bara wawindwa, wapigwa
- Kisa ni suala la kuwepo kwa Muungano
Na
Waandishi wetu, Zanzibar
Machafuko
makubwa yameukumbuka mji wa Zanzibar
juzi na jana, ambapo Kanisa moja limelipuliwa na kitu kinachoaminika kuwa bomu
la kurusha kwa mkono, huku kukiwa na madai kuwa watanzania wenye asili ya Bara wanaoishi
na kufanya kazi visiwani hapa wakishambuli.
Mashuhuda
wameliambia Tanzania Daima kwamba, watu ambao hadi sasa hawajajulikana lakini
wakiaminika kuwa ni wafuasi wa kundi la kidini la uamsho, walilishammbulia na
kulilipua Kanisa la Tanzania Assemblies Of God la Kariakoo, kuharibu magari,
miundombinu na mali nyingine.
Taarifa hizo
zilizothobitishwa na jeshi la polisi, zimesema kuwa wafuasi wa kundi hilo walianza vurugu hizo
wakipinga kitendo cha kukamatwa kwa kiongozi wao, Mussa Juma kwa kosa la
kufanya maandamano bila kibali cha polisi.
Habari
zimedai kuwa baada ya kukamatwa kwa kiongozi huyo, wafuasi wake walianza
kuhamasishana kwenda kituo cha polisi Madema, kilichoko wilaya ya Mjini
Magharibi wakiwa na silaha za mawe, jambo lililowafanya polisi kutumia mabomu ya
machozi kuwatawanya.
Hata hivyo,
habari zinadai kuwa baada ya kutawanyika majira ya saa mbili usiku wafuasi hao
walianza kuziba barabara kwa mawe na magogo makubwa, kuchoma matairi katika
maeneo ya michenzani, kabla ya kuyashambulia na kuharibu vibaya magari kadhaa.
Aidhaa
mashuhuda wamedai kuwa baadhi ya wafuasi hao walianza kuzisaka nyumba za ibada
na ndipo walipokwenda lilipo kanisa hilo ,
na kuanza kulishambulia kwa mawe, kabla ya kulilipua kwa kitu kinachoaminika
kuwa bomu
Kadhalika,
kuna madai kuwa wafuasi wengine wa kundi hilo ,
walijigawa na kuanza kuzifuatilia nyumba wanamoishi wafanyabiashara na
wafanyakazi wanaotoka Tanzania Bara na kuzishambuli kwa mawe, huku wakitoa
maneno ya vitisho.
Mmoja wa
watanzania hao anayefanya kazi katika hoteli moja ya kitalii (jina
linahifadhiwa) alikiri nyumba yao
kushambuliwa vikali, na jana alilazimika kuhamia kwa rafiki zake ambao ni
wenyeji wa visiwa hivi.
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Kamishna Musa Ali katika taarifa yake
jana kwa vyombo vya habari, amekiri kuharibiwa kwa kanisa hilo na kwamba hadi
jana mchana watu saba walikuwa wakishikiliwa na jeshi hilo.
Kamishina
Ali alisema, kundi hilo Mei 26 katika mwendelezo wake wa kufanya mikusanyiko kwa ajili ya makongamano,
mihadhara, dua na itkafu wakiwa katika viwanja vya Lumumba majira vya asubuhi
kwa dhamira ya kusasababisha watu wauchukie
Muungano na kuitaka serikali iitishe kura ya maoni kuhusu kuendelea, au kutoendelea
kwa Muungano na serikali zake.
Alisema
pamoja na kufanya matendo mengine ya uvunjifu wa amani kinyume na lengo la kuanzishwa kwa
jumuia hiyo na katiba yao , majira ya saa za
mchana viongozi wao waliwahamasisha watu waliokuwa watu katika kongamanao hilo kufanya maandamano
bila kuarifu polisi.
Kamishna
Ali alidai, kutokana na historia ya nyuma ya kundi hilo , polisi walilazimika kuyavunjwa kwa vile
katika siku za karibuni jumuiya hiyo ilikwishaonesha dalili za uvunjifu wa
amani kwa kuyfanya matendo mbalimbali ikiwemo kutoa lugha ya matusi kwa
viongozi wa serikali na wananchi ambao hawakuwaunga mkono.
Alisema
kundi hilo limekuwa likifunga barabara bila
sababu, kutembea na ving’ora isivyo halali, kuwashambulia watu kwa silaha zenye
ncha kali, kuharibu mali za
watu kama magari, na vingine vya aina hiyo.
Kutokana
na tukio hilo ,
Polisi wametangaza msako mkali wa kuwasaka viongozi na wanaokiwafadhili kikundi
hicho kwa gharama yoyote waliohusika na furugu hizo na kwamba watakaopatikana
watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka.
Kamishna
huyo amesema polisi na vikosi vya usalama wameimarisha ulinzi kuhakikisha kuwa
usalama wa maisha ya watu na mali
za unadumishwa kwa gharama yoyote.
Chadema wailaumu
Serikali
Jijini Dar es Salaam, Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema Rais Jakaya Kikwete, Serikali ya
Umoja wa Kitaifa Zanzibar na CCM wamesababisha
mivutano na vurugu Zanzibar kwa kutaka kudhibiti mjadala kuhusu muundo wa muungano na uhuru wa nchi katika mchakato wa
katiba mpya kwenye suala hilo tete na tata.
Kauli hiyo ilitolewa jana
jijini Dar es Salaa, Mkurugenzi wa habari wa Uenezi wa chama hicho, John Mnyika
ambaye alisema mivutano na virugu zinazoendelea Zanzibar ni matokeo ya serikali
ya Muungano na ya Mapinduzi Zanzibar kutokuzingatia mapendekezo ya chama hicho
kuhusu umuhimu wa uhuru wa mjadala kuhusu muundo wa muungamo katika mchakato wa
katiba mpya.
Aidha, alisema mvutano huo
umeshika kasi baada ya maamuzi ya NEC ya CCM bila ya maoni ya wanachama wake wa
Zanzibar na bara kuminya mjadala kuhusu suala hilo .
“Maamuzi hayo ya NEC
yaliyotanguliwa na kauli ya Rais Kikwete kudhibiti mjadala kuhusu hatma ya
muungano. Jana na leo pamekuwapo na vurugu Zanzibar kati ya wafuasi wa kikundi cha
uamsho na vyombo vya dola, kukamtwa ni matokeo tu,” alisema Mnyika
mwisho
AJALI:
habari za kuaminika zinasema kuwa Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, Chadema, amepata ajali mbaya ambayo imesababisha kifo cha mama yake mzazi, Gloria Shao na wengine wawili.
ajali hiyo imetokea majira ya saa 12.45 jioni ya leo, katika eneo la Boma Ng'ombe wilayani Hai, mkoa wa Kilimanjaro wakati alipojaribu kumkwepa mwendesha pikipiki na ndipo gari lake likaacha njia na kupinduka.
Selesini akiongea nami kwa shida kutoka katika hospitali ya wilaya ya hai, alisema kuwa anajisikia maumivu makali kifuani na alikuwa hajui hali ya mama, mke wake na wengine
-->
Na Happiness Katabazi
HATIMAYE
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemtangaza Mbunge wa Jimbo la Ubungo,John
Mnyika (Chadema) kuwa ndiye mbunge halali wa jimbo hilo na matokeo ya uchaguzi
ya jimbo hilo yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi Novemba mwaka
2010,yalikidhi matakwa ya kisheria.
Uamuzi huo ulisababisha jiji la Dar es
salaam kuzizima kwa shangwe na nderemo na baadhi ya barabara zikifungwa kwa
muda kutokana na umati mkubwa wa wafuasi na
wanachama wa Chadema waliokuwa wakishangilia ushindi wa mbunge huyo.
Akisoma hukumu hiyo iliyokuwa
ikisubiriwa kwa shauku kubwa ndani na nje ya jiji la Dar es Salaam, na
kuhudhuriwa na maelfu ya wafuasi wa vyama hivyo, Jaji Upendo Msuya alitupilia
mbali hoja moja baada ya nyingine, kabla ya kuhitimisha na kufutilia mbali
pingamizi lililowekwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ng’umbi.
Akichambua dai la kwanza, la kwamba
mdaiwa wa pili(Mnyika) aliingiza Laptop binafsi
katika chumba cha kujumlishia kura ambazo zilimuongezea kura hewa14,857
ambazo hazikuhesabiwa, jaji huyo alisema mashahidi wa tatu wa mlalamikaji
walishindwa kuthibitisha dai hilo katika ushahidi wao.
“Hoja katika dai hili ni je Laptop hizo
zilitumika kuongezea kura au la..lakini mahakama baada ya kupitia ushahidi wa
pande zote mbili umeona Ng’umbi ameshindwa kutoa vielezo au kuleta ushahidi wa
kuunga mkono dai lake kwamba kompyuta hizo mali ya Mnyika ambazo kisheria
hazikupaswa kutumika kujumlishia kula, zilitumika na kwa sababu hiyo mahakama
hii inatupilia mbali dai hilo”alisema Jaji Msuya.
kuhusu hoja ya kura 14,857 zinazodaiwa kuwa
hewa, jaji huyo alisema amelazimika kuzifanyia mahesabu idadi za kura
walizopata ambapo alisema Mnyika alipata kura 66,742, Ng’umbi 50,554 jumla ya
kura hizo ni 117,286 na wagombea wengine 14 toka vyma vingine walipa kura
15,210 kwa hiyo jumla ya kura zote
walizopigiwa wagombea wote 16 ilikuwa ni 132,496.
“Kura 14,857 zinazobishaniwa na
mdaiwa zinaweza kuhesabiwa kwa jumla ya wagombea 16 ambao walipata 132,496 ambapo kura halali zilizopigwa ni
117,639 ,kura zilizoaribika ni 2,184
unapata jumla kura 14,857.
Alisema baada ya kufanya hesabu ya kura
hizo alibaini kuwepo kwa tofauti ya kura 353 sawa na asilimi 0.3 ya jumla ya
kura halali zilizopigwa.
“Katika akili yangu nimetafakari dai
hili ,pia nimezingatia mazingira ya kujumlishia kura yaliyoelezwa na pande zote katika kesi hii, nimezingatia
muda wa kazi na kielelezo kilicholetwa na upande wa utetezi ni sahihi na dosari
ya kura 14,857 haikuweza kufanywa na laptop hizo na Mnyika hakupinga kuingia nazo
kwaajili ya kuhakiki kura ambazo zilishahesabiwa na maofisa wa NEC .
“Kwa maelezo hayo hapo juu mahakama hii
inasema hata sheria haikatazi wakala wa
mgombea kuingia na laptop kwenye chumba cha kujumlishia kura na pia
Ng’umbi ameshindwa kuleta wataalamu wa kompyuta waje kutoa ushahidi ambao
ungeonyesha laptop hizo zilitumika kujumlishia kura na kwa maana hiyo ombi hilo
nimelikataa ”alisema Jaji Msuya.
Kuhusu dai kuwa Mnyika aliingiza watu zaidi ya nane ambao hawakustahili katika
chumba cha kujumlishia kura, jaji huyo alisema Ng’umbi ameshindwa kutoa
ushahidi na hata kama waliingia waliathiri vipi taratibu na kanuni za uchaguzi
wa jimbo hilo.
Kuhusu
dai la Mnyika kwamba alimkashifu Ng’umbi katika mkutano wake wa hadhara
alioufanya Septemba mwaka 2010 na kudaiwa alimuita ni fisadi kwasababu aliuza
nyumba za UWT ,alisema pia mlalamikaji huyo ameshindwa kuthibitisha dai hilo
kwani lilijikita katika misingi ya ushahidi wa kusikia ambao hautakiwi
mahakamani.
“Kwa kuitimisha mahakama hii imetupilia
mbali madai yote ya mlalamikaji na kwa kauli moja inamtangaza Mnyika kuwa ndiye
mbunge halali wa jimbo la Ubungo na kwamba taratibu zote za uchaguzi zilifuatwa
“alimaliza Jaji Msuya na kusababisha kulipuka kwa nderemo na vifijo toka kwa
wafuasi wa Chadema.
Ng’umbi
aondoka kwa huzuni
Muda mfupi
mara baada ya kutolewa kwa hukumu, malalamikaji katika kesi hiyo, Hawa Ng’umbi,
aliondoka mahakamani hapo kwa huzuni huku akisindikizwa na baadhi ya wanachama
wa CCM waliofika hapo kusikiliza kesi hiyo.
Akizungumzia
juu ya kama ana nia ya kukata rufaa, Ng’umbi alisema bado anatafakari ili aweze
kupata majibu kama atakata rufaa ya kupinga hukumu hiyo.
Alisema atakaa na uongozi wa juu wa chama chake kwa ajili
ya kuangalia kama kutakuwa na uwezokano wa kufanya hivyo, haraka iwezekanavyo.
”Hadi sasa siwezi nikasema lolote juu ya kukata rufaa,
lakini nitatolea ufafanuzi juu ya hilo pindi nitakapokaa na uongozi wa juu na
kulijadili suala hilo,”alisema Ng’umbi.
Katika kesi hiyo Ng’umbi alitetewa na wakili wa kujitegemea
Issa Maige, wakati Mwanasheria Mkuu wa Serikali alitetewa na wakili Kiongozi wa
serikali Justus Mulokoz. Mnyika alitetewa na Edson Mbogoro.
Chadema yafanya kufuru
Baada ya kumalizika kusomwa kwa hukumu
hiyo, maelfu ya wanachama wa Chadema
walimbeba juu juu Mnyika na kumtoa nje ya viwanja vya mahakama kwa shangwe.
Wabunge wawili wa chama hicho, Ezekiel
Wenje wa jimbo la Ilemela na Mchungaji Peter Msigwa wa Iringa mjini waliungana
na umati huo na ndipo ukaanza msafara wa kuelekea katika ofisi za jimbo la
ubungo huku wakiimba nyimbo mbali mbali za kusifu hukumu hiyo
Msafara ulipitia barabara ya Maktab,
Bibi Titi, morogoro ambapo polisi waliokuwa wametanda kila eneo la mji,
walijaribu kumzuia Mnyika wakitaka apande gari kuepusha msongamano, lakini wananchi
waligoma na kutishia kufanya fujo hali iliyowalazimu askari kuusindikiza kwa
amani.
Idadi ya watu ilikuwa ikiongezeka kila
baada ya muda, na baadhi ya wafanyakazi na wenye biashara zao waliacha kwa kwa
muda na kuungana na wafuasi hao kushangilia.
Katika eneo la magomeni magomeni mwembe
chai wanafunzi wa shule ya Msingi Dk Omar waliungana na msafara huo sambamba na
wanafunzi wengine wa shule mbali mbali za sekondari, na katika eneo la soko la
Big
Brother wafanyabiashara walionekana wakiwa wamejipanga barabarani na kupunga mikono juu huku wakiwa wameshika bendera za Chadema.
Brother wafanyabiashara walionekana wakiwa wamejipanga barabarani na kupunga mikono juu huku wakiwa wameshika bendera za Chadema.
Hata hivyo, mamia ya watu katika eneo
la Kituo Kikuu cha Mabasi walimzuia Mnyika wakitaka aingie ndani ya stendi hiyo
kuhutubia jambo ambalo lilipingwa na viongozi wa Chama hicho kwa kuhofia
uvunjifu wa amni.
Mnyika auhutubia
Akiwa katika eneo la ofisi za Chadema, Ubungo, Mbunge huyo alilazimika kuhutubia umati wa watu, ambapo alisema hukumu hiyo ni ushindi wa wananchi wote dhidi
ya ufisadi unaofanywa na serikali ya CCM.
Akiwa katika eneo la ofisi za Chadema, Ubungo, Mbunge huyo alilazimika kuhutubia umati wa watu, ambapo alisema hukumu hiyo ni ushindi wa wananchi wote dhidi
ya ufisadi unaofanywa na serikali ya CCM.
“Kwa sababu ya mfumo wa serikali yetu
nilijua leo (jana) ingekuwa ni mwisho wa ndoto yangu ya kuwatumikia wananchi,
lakini kwa sala zenu tumeshinda na sasa ni fursa nyingine ya kuwatumikia ninyi
mlioniyuma pasipo kuwa na kizuizi chochote”alisema Mnyika na kushangiliwa.
Alisema mazingira ya kazi awali
yalikuwa magumu kutokana na muda mwingi kufuatilia kesi mahakamani na kwamba
sasa ana uhakika wa kuongeza nguvu juu ya kuzisemea shida za wananchi
bungeni na hata kuzitatua.
Aliitaka Taasisi ya Kupambana na Rushwa
(TAKUKURA) iwaeleze wananchi hatua waliyofikia baada ya aliyekuwa mshindani
wake Hawa Ng’umbi kuwahi kukamatwa na taasisi hiyo kwa makosa ya rushwa.
Alisisitiza kuwa ni wakati wa wananchi kujua
nini kinaendelea dhidi ya kesi hiyo na kwamba wasimuonee aibu kwa kuwa anatoka
chama kinachotawala.
Akizungumzia masuala ya kitaifa Mnyika alisema anazo nyarak zinazoonyesha matumizi mabaya ya fedha katika benki kuu huku akisema hali hiyo inaiweka nchi katika hatari ya kukwama kiuchumi kutokana na ufisadi unaofanyika.
Akizungumzia masuala ya kitaifa Mnyika alisema anazo nyarak zinazoonyesha matumizi mabaya ya fedha katika benki kuu huku akisema hali hiyo inaiweka nchi katika hatari ya kukwama kiuchumi kutokana na ufisadi unaofanyika.
“Ninazo nyaraka za siri za benki kuu na
ninatarajia kuziweka hewani muda wowote kuanzia sasa pale panafanyika ufisadi
wa kutisha hali inayofanya mfumuko wa bei kuongezeka kila siku”alisema Mnyika
Kuhusu tatizo la maji katika jimbo la Ubungo
na madudu ya wizara hiyo, alisema ataenda kupambana nae bungeni baada ya
kuonyesha kiburi cha kutosikia kilio cha wananchi huku akisisitiza suala la
Machinga kulifikisha bungeni
Mbowe: ni ushindi wa
watanzania
Naye
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, amesema ushindi wa Mnyika ni wa Wananchi
wa jimbo la Ubungo, Wanachama na Watanzania kwa ujumla.
Akizungumza
na waandishi wa habari mara baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Mbowe alisema
kesi za uchaguzi zinagharimu kiasi kikubwa cha fedha ambazo zingetumika kwa
ajili ya shughuli zingine za maendeleo, hivyo suala hilo litawasilishwa bungeni
kujadiliwa.
Mbowe
alisema pesa za uchaguzi zinazopotea zingeweza kutumika kwa ajili ya kununua
dawa hospitali, vitanda, madawati kwa ajili ya maendeleo ya nchi.
“Wananchi
kama mlivyoona wenzetu walikuwa na mashitaka matano, ambayo yametupiliwa mbali
na Jaji kutokana na kukosa uthibitisho, hatua ya kukimbilia mahakamani
kunakofanywa na baadhi ya Wabunge huku wakikosa vielelezo, sio nzuri”alifafanua
Alisema
kama Mnyika angepoteza Ubunge huo, ni wazi kwamba Wananchi wasingepata
mwakilishi mwenye uwezo kama wake.
Mawaziri, wabunge wengi wanaishi
na VVU
Na Nasra
Abdallah
Baraza
la watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Nchini (TACOPHA) limedai kuwa wapo mawaziri
na wabunge wanaoishi na virusi vya ugonjwa huo, na limewataka wasiogope kujitangaza
hadharani ikiwa ni pamoja na kuunda mtandao wao.
Mwenyekiti
wa Baraza hilo,Vitalis Makagula, alitoa kauli hiyo wakati wa semina ya siku
mbili ya waandishi wa habari kuhusu vvu/Ukimwi, Sheria na Haki za Binadamu, iliyoandaliwa
na Chama cha Waandishi wanaoandika habari za Ukimwi(AJAAT), na kufanyika jijini
Dar es Salaam.
Makagula
alisema kujitangaza kwa viongozi hao kutasaidia kuondoa woga kwa wananchi
wengine ambao wanaogopa kujitokeza hadharani na kujitangaza, kwa vile watakuwa
wameonesha mfano.
Mwenyekiti
alidai kushangazwa na ukimya wa viongozi hao hata pale wanapolazimika
kuzungumzia ugonjwa huo katika majukwaa yao
ya kisiasa, husema kwa dakika chache na kurukia mambo mengine.
“Tunajua
vema wapo mawaziri wanaoishi na ugonjwa huu. sasa badala ya kujificha na
kuongea tu kwa maneno, ifike mahali viongozi wetu wafanye suala hili kwa
vitendo,”alisema.
Alisema
hadi sasa, makundi machache ndio yameonesha nia yakuwa na mtandao wa watu
wanaoishi na ugonjwa huo wakiwemo,walimu waandishi na wananchi wa kawaida huku
wataalam katika fani mbalimbali wakibaki nyuma jambo analosema bado jitihada za
makusudi zinatakiwa kufanyika.
Naye Mwanasheria
wa Taasisi ya Kudhibiti Ugonjwa wa Ukimwi (TACAIDS) Sam Komba, alisema pamoja
na Ukimwi kuwa na mahusiano ya karibu na haki za binadamu, lakini bado wagonjwa
wanakabiliana na unyanyapaa, na wengine wakilazimishwa kupimwa bila hiari yao kama
vile akina mama wajawazito.
Awali
akifungua semina hiyo,Mwenyekiti wa AJAAT,Simon Kivamwo,alisema lengo la semina
hiyo ni kuwajengea uwezo waandishi katika kuandika habari za Ukimwi.
Kivamwo
alisema katika semina hiyo waandishi wataweza kupitia sheria ya Ukimwi na kujua
watu ambao wapo katika mazingira hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa huo.
mwisho.
Kagasheki akumbana na madudu Maliasili
·
Maofisa wake wafuja mamilioni ya fedha
·
Atishwa na utoroshaji wanyama hai
Na Asha Bani
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis
Kagasheki ameelezea kushtushwa kwake na ubadhilifu wa kutisha ulioko katika
wizara hiyo, Idara ya wanyamapori unaodaiwa kufanywa na baadhi ya watendaji
wake.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya
kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wizara ya Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Jijini
Dar es Salaam, waziri huyo alisema idara
hiyo inanuka kwa uozo unaotokana na wizi na ubadhilifu mkubwa ambao umeleta
hasara kwa taifa
Kagasheki alidai idara hiyo inaongoza kwa
‘madudu’ ya kutisha, na ametangaza kuchukua hatua za haraka dhidi ya watendaji
wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhilifu huo mkubwa haraka iwezekanavyo, akidai
fedha zilizotafunwa na wajanja hao ni nyingi.
“Jamani Idara ya wanyamapori ina fedha nyingi lakini
zinaliwa na watu kwa maslahi binafsi na kama fedha hizo zingekuwa zinapelekwa serikalini
kama inavyohitajika nchi hii kwa sasa ingefika mbali, mimi naogopa hata kutaja
kiasi cha fedha hapa hadharani,”alisema Kagasheki.
Mbali na ufujaji huo, Balozi Kagasheki amekiri kuwa usafirishaji wanyamapori
nje ni mkubwa mno licha ya serikali kusitisha kuuzaji huo.
Alisema uchunguzi wa haraka umebaini kuwa
biashara ya kusafirisha wanyama pori inafanywa kati ya wanfanyabiashara wa
ndani na baadhi ya watendaji ambao hawajali na wanaonekana kutumia kila mbinu
kufanikisha biashara hiyo.
Hata hivyo, katika hali iliyotarajiwa, Balozi
Kagasheki alionesha hofu yake ya kukabiliana na wafanyabiashara na baadhi ya
maafisa wa wizara hiyo, kiasi cha kuomba msaada kutoka taasisi nyingine
vikiwemo vyombo vya habari kusaidia kupambana na ‘genge’ la wabadhilifu hao
“Katika idara kunahitaji usaidizi maana hapa ni
vita na hata ninyi waandishi nafikiri mnaweza tukasaidiana kwa kuwa najua
mtakuwa mnawajua sana wafujaji. Kuwaondoa hawa ni kutangaza vita ”alisema
Kutokana na hali hiyo, alisema atavunja uongozi
wa idara hiyo na kuunda upya haraka iwezekanavyo, ingawa ni mapema sana kufanya
hivyo.
Alisema ataagiza kufanyika kwa sensa kwa wanyama
na kuweka wazi kila kitu, ili kunusuru kumalizika kwa wanayama wote.
“Tutawajulisha wananchi waelewe, hatutachelewa
maana watu wameshajua, wasije kuwamalizia wanyama wote,”alisema Balozi
Kagasheki.
Balozi Kagasheki alibainisha pia udhaifu mkubwa
ndani ya wizara hiyo uliosababisha kushindwa kudhibiti uuzwaji wa magogo nje ya nchi.
Alisema katika usimamizi wa mazao ya misitu
mambo hayaendi vizuri lakini akadai kuyashughulikia haraka iwezekanavyo.
Akitoa hotuba yake kwa wajumbe wa bodi hiyo
alisema rasilimali za misitu zinakadiriwa kuwa hekta 33.5 milioni, ambapo kati
ya hizo hekta milioni 15.3 zimetengwa na kuhifadhiwa kisheria katika sehemu
mbalimbali za nchi huku hekta milioni 9.7 za hifadhi ya maji ardhi na bioanuai
na haziruhusiwi kuvunwa.
Alisema
kiasi cha hekta 2.3 milioni ni ya misitu ya hifadhi ya jamii, na wakala
akisimamia mashamba 15 ya miti ya kupandwa yenye takribani hekta 85,000 za
misitu iliyohifadhiwa.
Kagasheki alisema eneo la misitu takribani hekta
milioni 18.2 zilizobaki ni eneo lisilohifadhiwa kisheria. Aidha alisema
watumishi wa wakala wa huduma za misitu ni wachache ikilinganishwa na maeneo ya
misitu yanayotakiwa kusimamiwa kulingana na takwimu zilizopo.
“Kuna wataalamu 1,756 sawa na asilimia 67.5 ya
watumishi wanaohitajika ambao ni 2,600 huku wataalamu wanaosimamia na kutunza
misitu ya asili moja kwa moja ni 500 tu
sawa na asilimia 19.2 ya wanaohitajika kusimamia misitu ya taifa iliyohifadhiwa
kisheria,”alisema.
Naye
Naibu Waziri wa Wizara hiyo Lazaro Nyalandu alimtaka kila mtu kujenga utamaduni
wa kupanda miti ili nchi iwe kijani, na kuongeza kuwa kuna soko kubwa la asali duniani
linaloweza kuharibika kutokana na ufugaji wa nyuki unaofanyika karibu na kilimo
cha tumbaku unaharibu ubora wake.
Kutokana na hali hiyo aliwashauri wafugaji wa
nyuki kufanya shughuli hizo mbali na kilimo cha tumbaku.
Mwisho.
Kesi ya
Lulu yapigwa kalenda
Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es
Salaam, jana iliairisha tena kesi ya mauji inayomkabili msanii wa Filamu,
Elizabeth Michael ‘Lulu’ hadi Juni 4, mwaka huu kwa maelezo kuwa jalada la kesi
hiyo limeitwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kufanyiwa kazi.
Mei 15 mwaka huu, Lulu kupitia
mawakili wake Kenned Fungamtama, Peter Kibatara, Fulgence Masawe na Joaquine De- Melon waliwasilisha ombi Na.46/2012 chini ya hati
ya dharura iliyokithiri Mahakama Kuu wakiomba mahakama hiyo iamuru Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
kulishughulikia ombi la msanii huyo la kutaka kesi hiyo isikilizwe katika
mahakama ya watoto kwasababu mshtakiwa huyo ana umri chini ya miaka 18.
Mei 18
mwaka huu, uongozi wa Mahakama Kuu ukampangia Jaji Dk.Fauz Twaibu kusikiliza
ombi hilo
ambapo atalisikiliza Mei 28 mwaka huu mahakama hapo.
Kwa
mujibu wa ombi la Lulu, anadai kuwa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu
Augustina Mmbando Mei 7 mwaka huu, alikataa kutoa uamuzi la kutaka kesi hiyo ihamishiwe
katika mahakama ya watoto kwasababu mshitakiwa huyo ana umri chini ya miaka 18
na badala yake hakimu huyo akasema mahakama hiyo haina mamlaka na kuwashauri
mawakili hao kuwasilisha ombi hilo
Mahakama Kuu.
Kwa
mujibu wa hati hiyo ya madai, Wakili Fungamtama alidai kuwa Hakimu Mmbando
alijielekeza vibaya kwa kusema kuwa mahakama ile ilikuwa haina mamlaka ya
kusikiliza ombi lao kwa hiyo wanaiomba Mahakama Kuu imwelekeze hakimu huyo
asilikize ombi lao na alitolee maamuzi na kuwa endapo Mahakama Kuu itabaini vinginevyo
basi mahakama hiyo ya juu itoe tafsiri ya umri kuhusu ombi hilo .
mwisho
TCRA: Simu za mkononi hazina madhara
Na Sitta Tumma, Kwimba.
MAMLAKA ya Mawasiliano nchini (TCRA), imesema kwamba mionzi ya mawimbi ya mawasiliano ya simu hayaleti madhara kwa watumiaji punde wanapokuwa wanawasiliana, tofauti na inavyoelezwa na baadhi ya watu.
Imesema, katika kubaini ukweli huo imefanya utafiti kuhusiana na athari ambazo zinaweza kumkumba mtumiaji wa simu hizo, na kwamba hakuna athari zozote zinazoweza kujitokeza badala ya simu yenyewe kuchemka iwapo mtumiaji atatumia muda mrefu kuongea na mwenzake kwa wakati mmoja.
Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa, Injinia Lawi Odiero aliyasema hayo juzi wakati alipokuwa akizungumza katika siku ya Mawasiliano na Teknolojia inayofanyika Mei 17 kila mwaka, iliyofanyika kwenye shule ya sekondari ya wasichana ya Bishop Mayala Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Kwa mujibu wa Meneja huyo wa TCRA Kanda ya Ziwa, Watanzania hawana budi kuendelea kutumia mawasiliano ya simu, kwa maendeleo yao, na kwamba Mamlaka hiyo imejizatiti kuhakikisha inaboresha na kutoa huduma nzuri za mawasiliano hapa nchini.
"Mionzi ya mawasiliano ya simu hayawezi kumdhuru mtumiaji kama ambavyo imekuwa ikielezwa. Isipokuwa mtumiaji anayeongea kwa muda mrefu kwa wakati mmoja simu anayotumia hupata joto tu!.
Suala la kwamba kuna athari kubwa siyo kweli, ila ipo athari kidogo sana labda na ile ya simu kupata joto wakati wa mawasiliano. TCRA imefanya utafiti wa uhakika katika hili na ndiyo maana tunasema hakuna madhara kwa mtumiaji", alisema Meneja huyo wa TCRA Kanda ya Ziwa, Odiero.
Katika hafla hiyo, TCRA iliendesha pia maswali ya chemsha bongo, ambapo washindi waliweza kuzawadiwa TV yenye vifaa vyake vyote, Laptop mbili, kashine ya mahesabu pamoja na fedha taslimu kwa wanafunzi na walimu wa shule hiyo ya Bishop Mayala iliyopo Kijiji na Tarafa ya Ibindo Kwimba.
Kwa upande mwingine, Meneja huyo wa TCRA Kanda ya Ziwa, Odiero aliwahakikishia Watanzania kwamba, Mamlaka yake imejizatiti zaidi katika utoaji wa leseni za huduma, masafa, kuagiza bidhaa za simu na mawasiliano,leseni za kuuza vifaa hivyo vya mawasiliano nchini, pamoja na leseni ya mitandao nakadhalika.
Pamoja na mambo mengine alisema, Mamlaka hiyo imejiimarisha zaidi katika sula zima la kukuza na kulinda mawasiliano kwa maslahi ya watumiaji hapa nchini, ikiwa ni pamoja na kuendelea kutekeleza mikataba mbali mbali ya Kimataifa katika kuleta ufanisi bora wa huduma ya mawasiliani kwa Watanzania
Kwa mujibu wa Meneja huyo wa TCRA, Mamlaka hiyo ambayo ilianza kazi zake rasmi Novemba Mosi mwaka 2003, imefanikiwa pia kupiga hatua kubwa za kimaendeleo juu ya mawasiliano hapa nchini, hivyo kamwe haitarudi nyuma kuhakikisha kwamba Watanzania wengi wanapata huduma hiyo ya mawasiliano ya simu, intaneti na mawasiliano mengine yote yanayosimamiwa na TCRA.
Mwisho.
Dk. Kigoda msimamisha kazi bosi TBS
Marietha Mkoka na Happiness Mnale
WAZIRI wa Viwanda na Biashara Abdallah Kigoda amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la viwango Tanzania (TBS) Charles Ekerege kwa tuhuma za ubadhilifu.
Kusimamishwa kazi kwa Ekerege kumekuja baada ya kuwepo sintofahamu ya muda mrefu kuhusiana na kukabiliwa na tuhuma nzito za upotevu wa takairban sh bilioni 38 zinazotokana na ukaguzi wa magari nje ya nchi.
Kigoda alitangaza uamuzi huo jana, na kudai kuwa ni kwa ajili ya kutoa nafasi ya kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya tuhuma hizo, ambapo ameunda kamati maalum ya uchunguzi. Hata hivyo, waziri huyo hakutaka kuingia kwa undani kuhusiana na suala la mtendaji huyo mkuu wa TBS
Waziri huyo aliyeanzakazi wiki iliyopita, alisema ameamua kumsimamisha kazi Ekerege ili kulifanya shirika hilo lirudi katika hali yake ya kawaida ikiwemo kupisha bodi iliyoundwa kutimiza wajibu wake.
Tuhuma dhidi ya Ekerege ziliibuliwa na kamati mbili za kudumu za bunge, ya Mashirika ya Umma (POAC) na Hesabu za Serikali (PAC), ambapo wajumbe wa kamati hizo waliokwenda kufanya ukaguzi nje ya nchi walibaini madudu mengi, ikiwemo kutokuwepo kwa ofisi za ukaguzi kama ilivyodaiwa na shirika hilo, kiasi cha kusababisha upotevu wa sh bilioni 38.
Wajumbe wa kamati hizo walibaini malipo ya kampuni hewa za ukaguzi wa magari nje ya nchi.
Hatua ya kumsimamisha Ekerege, imekuja baada ya mtangulizi wake, Waziri Cyril Chami kushindwa kumchukulia hatua ikiwemo kumsimamisha, jambo ambalo pamoja na tuhuma nyingine dhidi ya mawaziri kadhaa, lililozua mzozo mkubwa bungeni kiasi cha kuwalazimisha wabunge kutishia kupiga kura ya kutokuwa na imani, na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Chami pia inadaiwa alikataa ushauri wa aliyekuwa naibu wake, Lazaro Nyarandu ambaye alitaka asimamishwe kazi kupisha uchunguzi, na akadiri kuendelea na msimamo huo hadi alipoachishwa uwaziri wa Viwanda na Biashara
Katika utetezi wake, Chami alidai kushindwa kumwondoa mkurugenzi huyo madarakani kwa kile alichodai kuwa mtendaji huyo ni mteule wa rais kama alivyo yeye. Kauli hiyo, na kubaki madarakani kwa Ekerege, kuliwashangaza wengi ambao waliamini kuwa, hakukuwa na sababu ya kutomwondoa kwa vile lengo lilikuwa kutaka tume ya uchunguzi ifanye kazi yake ikiwa huru. Aidha, inajulikana wazi kuwa kusimamishwa sio kufukuzwa, na hivyo angeweza kurudi kazini ikiwa ataonekana hana hatia.
Hata hivyo Dk. Kigoda ambaye ni Mbunge wa Handeni hakuwa tayari kuwataja wajumbe wa kamati hiyo na muda waliopewa kumchunguza Ekerege.
Katika hatua nyingine waziri huyo alisema atainua sera ya kukuza viwanda na biashara ikiwemo kuinua wafanyabiashara wadogo na ushirikiano baina ya serikali na viwanda vidogo.
“Tumepanga kuwasaidia wajasiriamali na kuangalia maeneo ambayo watu wakiwezeshwa watainua uchumi wao na kuboresha utendaji kazi,” alisema
Alisema kiwanda cha General Tyre kitahitaji kufufuliwa na viwanda vya Pamba na Korosho.
Pia alivisifu viwanda vinavyoiingizia serikali mapato kuwa ni kiwanda cha Saruji Twiga, Sigara (TCC) na viwanda vya bia kutaka viwanda vingine kuiga mfano ikiwemo kuongeza juhudi.
Akizungumzia uwekezaji katika nchi waziri huyo alisema kuwa suala la kupunguza gharama za umeme halijapata ufumbuzi hivyo juhudi zinahitajika kukabiliana na changamoto hiyo.
Mgomo mkubwa wa walimu wanukia
* Waipa serikali siku 13
Na Nasra Abdallah
CHAMA cha walimu Nchini(CWT),kimetoa siku 13 kwa Serikali kuwalipa malimbikizo ya madeni yao la sivyo wasilaumiwe kwa hatua ambayo wataichukua.
Akizungumza na waandishi wa habari,jijini Dar es Salaam,Rais wa CWT ,Gratian Mukoba, alisema madeni hayo yanayofikia sh. Bilioni 13 yanahusiana na mishahara na mengine.
Akiwa ameongozana na kamati tendaji ya CWT Mukoba alidai tamko hilo limetokana na kikao chao walichokaa Mei 14 hadi 18 mwaka huu ambapo mbali na mambo mengine ,kamati ilipokea taarifa ya ulipwaji wa madeni ya walimu yaliyohakikiwa mwaka 2011 na kubaini kuwa Desemba mwaka jana Wizara ya Fedha na Uchumi ilitoa jumla ya sh. Bilioni 22.5 kwa ajili ya kulipa madeni hayo.
Akifafanua zaidi, alisema hadi kufika Machi mwaka huu, kati ya fedha hizo zilizotengwa kuwalipa walimu,TAMISEM iIilikuwa imelipa jumla ya sh. Bilioni 16.6 na bado ilikuwa haijalipa sh. Bilioni 2.6
Hadi Aprili mwaka huu,Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufindi ilikuwa imewalipa jumla ya sh. Milioni 800 kati ya bilioni 3.2 zilizotengwa kwa kazi hiyo.
“Kamati inatoa rai kwa Serikali kutowabeza walimu kiasi hicho na inategemea kuona hatua za haraka zinachukuliwa ili kuepuka mgogoro wa kikazi kati ya walimu kupitia chama chao na serikali kama mwajiri”alisisitiza Mukoba.
Alisema serikali inapaswa kulipa madeni yote hayo ndani ya mwezi huu, kwa kuwa fedha hizo tayari zipo mikononi mwa Wizara ya Elimu na kinachofanywa sasa ni ucheleweshwaji wa makusudi.
Madai mengine chama hicho walimu wanayotaka kufanyiwa kazi mbali na madeni ni Serikali kuweka kwenye bajeti yake posho ya kufundishia asilimia 55 kwa walimu wa Sayansi na asilmia 50 kwa walimu wanaofundisha masomo ya sanaa.
Pia wameitaka Serikali iweke kwenye bajeti yake asilimia 30 ya mishahara ya walimu wanaofanya kazi kwenye mazingira magumu kama posho ya mazingira na kuongeza kuwa Wilaya zinazohusika zilishatajwa na Serikali.
DK. Kafumu amkataa Jaji
Na Mustapha Kapalata,Nzega
KATIKA hali isiyo ya kawaida jana Mbunge wa Jimbo la Igunga Dk. Peter Kafumu alimkataa Jaji Mery Nsimbo Shangali kuendelea kusikiliza kesi ya kupinga matokeo yaliyo mpatia ushindi mbunge huyo katika uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Akisoma barua ya Kafumu mbele ya mahakama hiyo, Wakili wake, Antony Kanyama alisema kuwa mteja wake hana imani na jaji huyo kwa kuwa baadhi ya maamuzi yanakwenda ndivyo sivyo.
Alisema imani na jaji huyo imetoweka kwa madai kwamba amekuwa akiwadhalilisha na kuwatukana mashahidi wa upande wa utetezi, na kutoa mfano wa shahidi(DW14), ambapo amedai alichukua nafasi ya mawakili wa mdai kwa kuwahoji maswali mashahidi wake badala ya kutaka ufafanuzi juu ya maelezo yao.
Aliitaja sababu nyingine kuwa ni tabia ya jaji huyo ya ukali pasipo sababu dhidi ya mawakili wa utetezi kila walipohoji mashahidi wa upande wa mdai.
Aliitaja sababu nyingine kuwa ni kile alichodai kuwa ni kitendo cha jaji huyo kuwanyima mawakili wa upande wa utetezi waliomba kupewa nakala ya mwenendo wa shauri hilo, mara tu usikilizaji wa kesi kwa pande zote ulipokamilika ili kuwasaidia kuandaa hoja za majumuisho.
Wakili Kanyama alidai kuwa kutokana na hali hiyo mashahidi wake muhimu wamekataa kuja kutoa ushahidi kwa kuogopa kudhalilishwa.
Hata hivyo, wakili Prof. Abdallah Safari anayemtetea mlalamikaji, Joseph Kashindye anayepinga ushindi wa Kafumu, alisema kuwa maombi hayo si ya msingi, na akatoa mifano mbalimbali ya kesi kama hizo na kuongeza kuwa kama wanaona hali ni mbaya wasubili wakate rufaa mara baada ya kesi hiyo kuhukumiwa.
Baada ya kupitia pande zote mbili na kusoma kwa muda jaji huyo alitupilia mbali ombi hilo la Kafumu na kusema kuwa kesi hiyo inaendelea kusikilizwa kwakufuata taratibu na kanuni za kimahakama.
Jaji Mery alisema hakuna sababu za msingi zilizotolewa na kwamba maelezo yanayolalamikiwa yanaweza kufanywa katika Rufaa.
Pamoja na kutupilia mbali ombi hilo , Wakili Kanyama aliiomba mahakama hiyo kuahirisha kesi hiyo mpaka aongee na mteja wake kama ataendelea ama vipi.
Katika hatua nyingine, Jaji Mery ametaka mahakama iachwe uhuru na isiingiliwe katika mwenendo wake, kwa vile hadi sasa haijabainika nani atakuwa mshindi katika kesi hiyo kwani bado ushahidi unaendelea kusikilizwa kwa mjibu madai na upande wa serikali.
‘’Naomba muiachie Mahakama iendelee kusikiliza kesi hii na muheshimu mahakama kama jinsi tulivyo apishwa’’alisema jaji Mery.
Ndugu zangu na rafiki zangu. Kwanza niwape pole kwa mshituko mlioupata
kwa haya yaliyojitokeza.
Naomba msisikitikesana . Kila jambo alilopanga Mola hutokea kadiri ya
mapenzi yake. Route ya maisha ya mwanadamu hupangwa na Mola mara tu
anapompulizia pumzi ya uhai. Hili lilipangwa hata kabla sijatokea
duniani miaka 42 iliyopita!
Mungu hakushindwa kumwokoa mwanawe Yesu asisulubiwe, tena kwa kuonewa!
Hasha, tungeupataje ukombozi bilahilo kutokea? Wakati mwingine Mungu
hutoa nafasi kwa mambomagumu kuwafika waja wake, si kwamba hawapendi,
bali ili unabii utimie. Ilifika wakati hata Yesu akaonakama Mungu
kamuacha! Hasa sisi kwa hili tunaweza kudhani Mungu katuacha! Hasha,
ni njia ya kuufikia ukombozi wa kweli.
Pili, kwa kifupisana , niwafahamishe kuwa,yaliyotokea ni ushahidi
kwamba maliasili ni ngumu. Kukabiliala na wabaya ni kazi ngumu. Wapo
waliojipanga ukiwavamia ovyoovyo unaondoka wewe. Ndivyo ilivyotokea.
Niwahakikishie, wazalendo wamepoteza mpambanaji.
Nimepambana na wahalifu angani, majini, porini, mijini na vijijini
ndani na nje ya nchi. Nilitumia kila aina ya uwezo wangu kulizawadia
taifa langu utumishi uliotukuka. Sikubakisha chembe ya energy.
Waziri gani aliyesimamia sheria na kuwapa vitalu watanzania maskini
wenye sifa na kuwaacha wazungukama sheria ilivyoelekeza? Waziri gani
aliyewafikisha mahakamni watorosha twiga akina Kamrani na wenzake?
Watu wametumia records za matukio ya 2009/10 kuficha matendo na
maamuzi ya kishujaa ya maige ya 2011.
Yawezekana hawakutaka nipate sifa, lakini ipo siku nitaipata. Tena si
siku nyingi. Niliwaomba wenzangu wamwogope Mungu. Bado nasisisitza
hivyo, si Mungu wangukama ilivyodhaniwa, bali Mungu wetu wa haki.
Waziri gani aliyefunga biashara ya wanyamahai? Waziri gani
aliyeonyesha mfano wa kuchukua hatua kwa watumishi pale alipoona
hawatendi sawa? Maige hakusita kuchukua hatua.
Maamuzi haya ni magumu na yamegusa watu wenye nguvu na ushawishi
mkubwa. Nilitegemea vita hii, na ninaamini tutashinda. Nilisema
Bungeni, watanzania wapenda haki wanisikilize kwa makini. Muda
haukuruhusu, ila nitarudi Bungeni na nitasema.
Imesemwa issue ya nyumba. Nimefafanua na kutoa vielelezo. Kila mbunge
aliyetaka kukopeshwa shs 290m, wengine wameanzisha biashara na wengine
wamenununua magari na wengine majumba. Wapo walioficha, na tupo
tuliojiweka wazi! Mkopo wangu huo umekuwa my contribution na balance
kulipwa na benki na nyumba kuimortgage.
Nimetoa nyaraka zote kwa wanahabari na vyombo vyote husika. Nimesema
mwenye mashaka aende kwa Msajili wa hati wizara ya ardhi, au kwa
kamishna wa maadili, au CRDB Azikiwe naDodoma nilikokopa au amtafute
muuzaji. Kote huko utapata rekodi ya bei na mode of payment. Wapo
wahuni, kwa maslahi ya kisiasa na chuki binafsi wametangaza bei
tofauti na niliyonunulia.
Mwanasheria wangu anashughulikiahilo . Niwahakikishie, vita
nimepigana, imani na dhamana nimeilinda, muda wa kutuzwa na mwenye
kumbukumbu sahihi, Mungu utafika. Naamini nimejiwekea akiba isyooza
Mbiguni.
Yapo mengi yasiyo sahihi yaliyosemwa. Nitakuwa nafafanua kila nipatapo
fursa na muda utazidi kutufunua. Kwa kifupi, kwa suala la vitalu,
hakuna kampuni hata moja iliyopewa kitalu cha uwindaji bila kuomba,
kukaguliwa na kamati ya ushauri na hatimaye kupewa alama. Kampuni
zisizokuwa na sifa ni zile zilizopata chini ya alama 50.
Na kwa kampuni zilizokuwa kwenye biashara, passmark ni alama 40 kwa
mujibu wa kanuni ya 16(5) ya kanuni za uwindaji wa kitalii za mwaka
2010.
Hakuna kampuni iliyopata chini ya alama 50 iliyopata kitalu. Hakuna
kampuni ya kizalendo iliyopendekezwa na kamati ya ushauri ambayo
haikupewa kitalu.
Kwa upande wa report ya CAG, haikunigusa binafsi kwani ilikuwa
inaishia juni 2010 wakati mimi ilishika dhamana Novemba 2010.
Ka upande wa biashara ya wanyama hai, hakuna wanyama waliosafirishwa
kinyume cha sheria wakati wangu (2011), na matukio ya utoroshaji
tulipoyabaini,tulifungua mashitaka kwa watuhumiwa nakufunga biashara
hiyo.
kwa haya yaliyojitokeza.
Naomba msisikitike
mapenzi yake. Route ya maisha ya mwanadamu hupangwa na Mola mara tu
anapompulizia pumzi ya uhai. Hili lilipangwa hata kabla sijatokea
duniani miaka 42 iliyopita!
Mungu hakushindwa kumwokoa mwanawe Yesu asisulubiwe, tena kwa kuonewa!
Hasha, tungeupataje ukombozi bila
hutoa nafasi kwa mambomagumu kuwafika waja wake, si kwamba hawapendi,
bali ili unabii utimie. Ilifika wakati hata Yesu akaona
kamuacha! Hasa sisi kwa hili tunaweza kudhani Mungu katuacha! Hasha,
ni njia ya kuufikia ukombozi wa kweli.
Pili, kwa kifupi
kwamba maliasili ni ngumu. Kukabiliala na wabaya ni kazi ngumu. Wapo
waliojipanga ukiwavamia ovyoovyo unaondoka wewe. Ndivyo ilivyotokea.
Niwahakikishie, wazalendo wamepoteza mpambanaji.
Nimepambana na wahalifu angani, majini, porini, mijini na vijijini
ndani na nje ya nchi. Nilitumia kila aina ya uwezo wangu kulizawadia
taifa langu utumishi uliotukuka. Sikubakisha chembe ya energy.
Waziri gani aliyesimamia sheria na kuwapa vitalu watanzania maskini
wenye sifa na kuwaacha wazungu
aliyewafikisha mahakamni watorosha twiga akina Kamrani na wenzake?
Watu wametumia records za matukio ya 2009/10 kuficha matendo na
maamuzi ya kishujaa ya maige ya 2011.
Yawezekana hawakutaka nipate sifa, lakini ipo siku nitaipata. Tena si
siku nyingi. Niliwaomba wenzangu wamwogope Mungu. Bado nasisisitza
hivyo, si Mungu wangu
Waziri gani aliyefunga biashara ya wanyamahai? Waziri gani
aliyeonyesha mfano wa kuchukua hatua kwa watumishi pale alipoona
hawatendi sawa? Maige hakusita kuchukua hatua.
Maamuzi haya ni magumu na yamegusa watu wenye nguvu na ushawishi
mkubwa. Nilitegemea vita hii, na ninaamini tutashinda. Nilisema
Bungeni, watanzania wapenda haki wanisikilize kwa makini. Muda
haukuruhusu, ila nitarudi Bungeni na nitasema.
Imesemwa issue ya nyumba. Nimefafanua na kutoa vielelezo. Kila mbunge
aliyetaka kukopeshwa shs 290m, wengine wameanzisha biashara na wengine
wamenununua magari na wengine majumba. Wapo walioficha, na tupo
tuliojiweka wazi! Mkopo wangu huo umekuwa my contribution na balance
kulipwa na benki na nyumba kuimortgage.
Nimetoa nyaraka zote kwa wanahabari na vyombo vyote husika. Nimesema
mwenye mashaka aende kwa Msajili wa hati wizara ya ardhi, au kwa
kamishna wa maadili, au CRDB Azikiwe na
muuzaji. Kote huko utapata rekodi ya bei na mode of payment. Wapo
wahuni, kwa maslahi ya kisiasa na chuki binafsi wametangaza bei
tofauti na niliyonunulia.
Mwanasheria wangu anashughulikia
nimepigana, imani na dhamana nimeilinda, muda wa kutuzwa na mwenye
kumbukumbu sahihi, Mungu utafika. Naamini nimejiwekea akiba isyooza
Mbiguni.
Yapo mengi yasiyo sahihi yaliyosemwa. Nitakuwa nafafanua kila nipatapo
fursa na muda utazidi kutufunua. Kwa kifupi, kwa suala la vitalu,
hakuna kampuni hata moja iliyopewa kitalu cha uwindaji bila kuomba,
kukaguliwa na kamati ya ushauri na hatimaye kupewa alama. Kampuni
zisizokuwa na sifa ni zile zilizopata chini ya alama 50.
Na kwa kampuni zilizokuwa kwenye biashara, passmark ni alama 40 kwa
mujibu wa kanuni ya 16(5) ya kanuni za uwindaji wa kitalii za mwaka
2010.
Hakuna kampuni iliyopata chini ya alama 50 iliyopata kitalu. Hakuna
kampuni ya kizalendo iliyopendekezwa na kamati ya ushauri ambayo
haikupewa kitalu.
Kwa upande wa report ya CAG, haikunigusa binafsi kwani ilikuwa
inaishia juni 2010 wakati mimi ilishika dhamana Novemba 2010.
Ka upande wa biashara ya wanyama hai, hakuna wanyama waliosafirishwa
kinyume cha sheria wakati wangu (2011), na matukio ya utoroshaji
tulipoyabaini,tulifungua mashitaka kwa watuhumiwa nakufunga biashara
hiyo.
Naanza kazi ya kuwawakilisha wananchi wa Msalala.
Nitawawakilisha kwa mujibu wa katiba na ahadi zangu kwao hadi 2015
watakapopata fursa ya kuamua vinginevyo.
Mara nyingi watenda mema hufanyiwa hiyana. Kwa wakristo, naomba msome
Mwanzo 4:1-15.
Wasalaam.
Nitawawakilisha kwa mujibu wa katiba na ahadi zangu kwao hadi 2015
watakapopata fursa ya kuamua vinginevyo.
Mara nyingi watenda mema hufanyiwa hiyana. Kwa wakristo, naomba msome
Mwanzo 4:1-15.
Wasalaam.
Muleba yakumbwa na mafuriko
Na Ashura jumapili,Kagera
MVUA kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani Kagera zimesababisha mafuriko katika maeneo mengi ya Wilaya ya Muleba na kubomoa nyumba zaidi ya 20, huku kata ya Muhutwe ikiwa imeathirika zaidi.
Mbali na kubomoa nyumba, mvua hiyo imesababisha vyoo vingi kufurika na kinyesi kutapakaa eneo kubwa la makazi ya watu, hivyo kuwepo na tishio la magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu.
Akiongea na Tanzania Daima kwa niaba ya wananchi wenzake Rajabu Juma mkazi wa Kijiji cha Bisore Kata Muhutwe alisema, nyumba yake ni miongoni mwa zilizoathirika baada ya kujaa maji, kiasi cha kumlazimu kubomoa matundu katika kuta za nyumba yaweze kutoka.
Diwani wa Kata hiyo Justus Magongo alisema hali ni mbaya na nyumba nyingi zimebomolewa na mafuriko, na huenda kukawa na maafa zaidi ikiwa mvua hizo zitaendelea kunyesha. Alisema uongozi wa kata umetoa taarifa kwa mkurugenzi na katibu tawala wa wilaya hiyo.
Alivitaja vijiji vilivyoathirika zaidi kuwa ni Bukoki,Kagondo senta, Muhutwe, Eibanga, Nshambya na Kagondo Eifo, na kwamba mvua hiyo imeaharibu pia miundo mbinu ya barabara, na karibu zote hazipitiki.
Kutokana na hali hiyo, uongozi wa shule ya msingi Nyarigamba ulilazimika kusimamisha masomo kwa siku ya jana wakihofia maafa kutokana na maji mengi kujaa madarasani, na hasa ikizingatiwa kuwa majengo yake hayajasakafiwa kwa saruji.
Hata hivyo alisema kuwa uwezekano wa nyumba kuendelea kubomoka ni mkubwa kwani kuna baadhi ya nyumba za matofali mabichi bado zimezungukwa na maji karibu robo ya nyumba kuta zimelowana.
Aidha diwani huyo alitoa wito kwa serikali ya wilaya ya Muleba kujiandaa kunyunyizia dawa katika maeneo yaliyobomoka vyoo na kusababisha kinyesi kusambaa ovyo ili kuepuka magonjwa ya milipuko.
Katibu Tawala Wilaya ya Muleba Projestus Lubanzibwa alipoulizwa jitihada zilizochukuliwa na halmashauri yake kuwanusuru wanachi hao alisema ofisi yake haina taarifa za mafuriko hayo.
“Mimi sina taarifa isipokuwa jana nilipita huko nikakuta maji yamejaa nika wasiliana na mtendaji wa kata hiyo leo amesema maji wameisha yaondoa kama kuna tatizo labada nifuatilie”alisema Lubanzibwa.
Naye afisa mtendaji wa Kata hiyo Ally Rajabu alipoulizwa alisema matukio hayo yametokea bado anaendelea na tathimini kwa kushirikiana na watendaji wa vitongoji.
Sakata la Bastora ya Rage laibukia tena
Na Mustapha Kapalata, Nzega.
SAKATA la bastora lililowahi kumfikisha polisi mbunge wa Tabora Mjini, Aden Rage na kupigwa faini ya sh laki moja na kamati ya maadili wakati wa kampeni za ubunge wa jimbo la Igunga, jana liliibuka tena jana wakati wa kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo hilo.
Akiwa mmoja wa mashahidi waliosimama jana katika Mahakama Kuu kanda ya tabora, Rage akijibu maswali kutoka kwa wakili wa mlalamikaji na aliyekuwa mgombea ubunge kupitia Chadema, Josephat Kashindye, alisema
waziri wa Utawi wa jamii njisia na watoto Sophia Simba jana walipanda kizimbani kutoa ushahidi wa kesi ya kupinga matokeo yakumpatia ushindi Dk,Peter Kafumu katika Mahakama Kuu kanda ya Tabora.
Shauri hilo lilifunguliwa na mlalamikaji Joseph Kashindye dhidi ya Dk.Kafumu, Mwanasheria Mkuu wa serikali pamoja na msimamizi wa uchaguzi.
Akiwa shahidi wa kumi na tano kwa upande wa wajibu madai Adeni Rage alikili kushiriki kampeni hizo za uchaguzi mdogo jimbo la Igunga akipangiwa kata ya Tarafa ya Igulubi wilayani humo.
Rage alitoa maelezo yote wakati akiulizwa maswali na wakili wa mjibu madai kwanyakati tofauti huku akiwa ameketi katika kiti kilichokuwa kimewekwa kizimbani.
Baada ya kutoa maelezo hayo wakili wa mlalamikaji alianza kumuuliza maswali shahidi huyo juu ya umiliki wa Bastora yake na kwanini alikuwa nayo katika mikutano mbalimbali ya kampeni ambazo alizoshiriki.
Mbunge huyo mambo yaliyo kuwa yakimkabili nipamoja na kutangaza kuwa mgombea wa chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) Joseph Kashindye amejihudhuru kugombea kiti hicho haliambayo ilileta tafrani katika uchaguzi huo.
Wakati akijubu maswali hayo Rage alikili kumiliki Bastora hiyo pamoja na kushiriki nayo katika shuguli nzima za kampeni wakati huo.
Hata hivyo alisema upepo ulimponza hasa pale ulipo peperusha shati lake na Bastora hiyo kuonekana hadharani na vyombo vya habari kumpiga picha mara mmoja.
’’Pamoja na kufanya mikutano mbalimbali hata wakati nikipanda kwenye jukwaa kulikuwa na upepo mkali uliofunua shati langu na kusababisha Bastora kuonekana hadharani nandipo waandishi walianza kuniangalia na hatimaye walinipiga picha iliyoonekana kwenye gazeti la mwananchi’’alisema rage.
Rage alisema kuwa mara baada ya kutokea tukio hilo bastora hiyo ilichukuliwa na Jeshi la Polis kwa maagizo ya waziri wa mambo ya ndani na yeye kuhojiwa pamoja na kupigwa faini ya laki mmoja na kamati ya maadili.
Akitumia muda mrefu kujibu maswali hayo zaidi ya masaa matatu alisema kuwa richa ya kuwa na batora katika majukwaa ya kampeni kamati ya maadili ya uchaguzi ilimpiga faini.
Wakati huo huo waziri wa Ustawi wa jamii na njinsi na watoto Sophia Simba akiwa shahidi wa kumi na sita kwa upande wa mjibu madai akitoa ushahidi wa kula chakula na wananchama wa CCM katika Hospitali ya Nkinga kata ya Inkiga.
Alikili kula chakula hicho na kudai kuwa alikuwa na mwaaliko wa chakula cha mchana na ndugu yake katika Hospitali hiyo hata hivyo alipoulizwa jina la ndugu huyo alishindwa kulitaja.
Richa ya kula chakula hicho alikili kula na watu zaidi ya 50 hali ambayo mawakili wa mlalamikaji waliendelea kumuuliza maswali mbalimbali ikiwepo na maneno aliyoyatamka kuwa msimchague kashindye kwani hana mke pia ni masikini hata hivyo waziri huyo alikanusha maneno hayo.
Kesi hiyo ikisilizwa na Jaji Mery Shangali inaendelea leo May 18 mwaka huu huku mashahidi wa mlalamikaji 22 wakiwa tayali wametoa ushahidi na sasa mashahidi 16 wa mjibu madai wanaendelea kutoa ushahidi huo ambapo upande wa serikali ukisubili kuanza kutoa ushahidi wake wa watu 10.
mwisho
Mawaziri wapya wagongana
* Mmoja asema, hakuna fedha, mwingine adai zipo
Irene Mark na Dunstan Bahai
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, mawaziri watatu wapya wa serikali, wametoa matamshi yanayokinza, kuhusiana ukweli wa hali ya fedha ilivyo ndani ya serikali.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawamba akiwaambia wadai kuwa serikali haina fedha kiasi cha kushindwa kutoa fedha za mikopo ya wanafunzi wote walioomba mikopo ya elimu ya juu kutokana na ufinyu wa bajeti unaoikabili Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Kwa mujibu wa Dk. Kawambwa, mwaka wa fedha wa 2011/12 serikali imetenga bajeti ya sh. bilioni 317.8 kwa ajili ya ukopeshaji lakini hadi kufikia Machi 15,2012, kati ya wanafunzi 113,356, waliokopeshwa ni 94,092 wakiwemo 26,272 wa mwaka wa kwanza, 66,744 wanaoendelea na masomo, 772 wanaosoma nje ya nchi na 304 wanaosoma shahada za uzamivu nchini waliopata huku zaidi ya wanafunzi 19,264 wakikosa.
Aidha, Waziri William Lukuvi juzi alionesha hofu yake ya serikali kuwa katika hali mbaya ya fedha, baada ya hatua ya wafadhili kuamua kutoipa serikali moja kwa moja fedha za maendeleo, badala yake kuamua kuziweka katika miradi iliyokusudiwa.
Hata hivyo, jana Waziri wa Fedha na Uchumi Dk. William Mgimwa amesema serikali inazo fedha za kutosha na kwamba wafadhili hawajajiondoa katika kuisaidia Tanzania , bali sasa fedha zao zilizokua zikitolewa katika bajeti hiyo zitaelekezwa kwenye miradi mbalimbali moja kwa moja..
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana Dk. Mgimwa aliwaondoa wasiwasi watanzania kwa maelezo kwamba wafadhili bado wataendelea kuisaidia Tanzania na kwamba hadi sasa Hazina ina fedha za kigeni kiasi cha dola bilioni 3.6 za Marekani zinazoweza kuilisha nchi kwa miezi minne hivyo si kweli kwamba Tanzania imefilisika.
“Naomba niwaondoe wasiwasi wananchi wahisani bado wanayo imani sana na sisi walichokifanya ni kuelekeza fedha hizo kwenye miradi moja kwa moja badala ya kuingiza kwenye bajeti kuu.
“…Tusisikilize maneno hayo wafadhili bado wapo wanaweza kutusaidia kupitia madirisha matatu, kwanza bajeti, pili miradi na kwenye kapu la maendeleo sasa wao wameamua kupeleka katika miradi, njia zote zinafaida yake,” alisema waziri huyo.
Hata hivyo Dk. Mgimwa ambaye ni Mbunge wa Kalenga alishindwa kueleza baadhi ya miradi itakayofaidika na fedha za wahisani moja kwa moja baada ya kuwepo kwa taarifa rasmi kwamba hawatachangia tena kwenye Mfuko wa Ukimwi.
Aidha waziri huyo aliyewahi kuwa mtumishi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) alisema serikali itaongeza umakini kwenye utunzaji wa fedha na uwajibikaji.
“Katika bajeti ijayo ya serikali tutaongeza nguvu kwa kuishirikisha sekta binafsi kwa sababu tunaamini kwenye dhana ya Public, Private Partnership (PPP) na vipaumbele vyetu tutawaeleza tukishakua tayari,” alisema Mgimwa.
Hata hivyo, pamoja na utetezi huo, katika hali nyingine Waziri Kawambwa katika hotuba yake iliyosomwa na Kaimu Kamishina wa Elimu wa Wizara hiyo, Mary Stella Wassene kwenye hafla ya uzinduzi wa Mpango Maalum wa kutoa elimu ya fedha ujulikanao kama NMB Financial Fitness shuleni uliofanyika kitaifa katika shule ya Sekondari ya Pugu na kufuatiwa na uzinduzi wa nakala 50,000 za vitabu vitakavyotumika kutoa elimu hiyo nchini, alisema serikali haina uwezo wa kuwapa mikopo wanafunzi wote waliokidhi vigezo kwa sababu ya ukosefu wa fedha.
Badala yake, aliwataka wazazi na watanzania kujifunza utamaduni wa kujiwekea fedha kidogo kidogo kwa ajili ya maendeleo ya elimu kwa watoto wao.
Wakati hayo yakiendelea, kumekuwa na malalamiko mengi karibu katika vyuo vingi, kupinga kucheleweshewa kwa posho na mikopo hata kwa wanafunzi walioteuliwa kupewa mikopo, huku mamia ya wengi wakiishia kulalamika kwa kuikosa.
Kawamba katika hafla hiyo jana ambayo Benki ya NMB inakusudia kutoa elimu ya fedha kwa wananchi, aliwahimiza watanzania wenye uwezo kuchangia sekta ya elimu.
“Hivi leo tunayo changamoto kubwa ya namna ya kugharamia elimu ya watoto wetu katika vyuo vya elimu ya juu. Pamoja na serikali kutenga fedha kila mwaka katika bajeti kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, bado mahitaji ya mikopo hiyo ni makubwa kuliko uwezo wa serikali wa kutenga fedha kwa ajili ya kukopesha,” alisema
“Wito wangu kwa wananchi ni kwamba, pamoja na mchango mkubwa wa serikali katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii hapa nchini, tujifunze utaratibu wa kujiwekea akiba kidokidogo kama tunavyo elekezwa na wenzetu wa NMB. Tukifanya hivyo wengi tutakuwa na uwezo wa kujitegemea zaidi katika kujiletea maendeleo yetu ikiwa ni pamoja na uwezo wa kugharamia pamoja na mambo mengine elimu ya vijana bila kuisubiri serikali itenge fedha ambazo hazitoshelezi mahitaji ya kila mmoja,” alisisitiza.
Dk. Kawambwa alisema mpango huo wa elimu ya fedha utasaidia jamii nyingi kuwa na nidhamu ya fedha lakini pia kuwa na mwamko wa kutumia huduma za benki ikiwa ni pamoja na kuhifadhi fedha zao huko.
Alisema utafiti uliofanywa na taasisi moja ya utafiti wa mambo ya fedha ya Financial Sector Deepening Trust (FSDT) unaonyesha kwamba, ni asilimia 10 tu ya Watanzania wanaotumia huduma za kibenki na kwamba moja ya sababu zinazoelezwa kuwa chanzo cha uwiano huu, ni uelewa mdogo wa masuala ya kifedha.
Kutokana na tatizo hilo , alisema kuwa Benki ya NMB imetambua changamoto hiyo na kudhamiria kuanzisha mkakati huo, wenye lengo la kuongeza uelewa wa masuala ya kifedha kwa Watanzania hususani wanafunzi.
Naye Mtendaji Mkuu wa NMB, Mark Wiessing, alisema wamelazimika kuchagua uzinduzi huo kufanyika katika shule hiyo kutokana na kuwa ni ya kihistoria kwa kutoa marais wa Tanzania lakini pia viongozi kadhaa wa ngazi za juu serikalini na kwenye mashirika mbalimbali.
Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Meshark Ngatunga, alisema benki hiyo imekuwa mstari wa mbele katika kufanya shughuli mbalimbali hasa za kijamii kama vile za elimu, afya na michezo na wameongeza huduma nyingine hiyo ya elimu ya fedha.
Alisema kwa mwaka jana pekee, benki hiyo imetumia zaidi ya sh. milioni 500 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo ya kijamii ikiwa ni pamoja na kukarabati madarasa katika shule ya sekondari ya Pungu na masuala ya michezo shuleni hapo.
Mwisho
Arusha, Muleba wazidi kuikimbia CCM
Grace Macha Arusha na Antidius Kalunde, Muleba
KIMBUNGA cha Operesheni Vua Gamba, Vaa Gwanda ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezidi kutikisakote nchini, baada ya kumzoa mjumbe wa Halmashauru Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Arusha mjinia Emmanuel Temba.
Temba ambaye pia amewahi kuwa Diwani wa Kata ya Kimandolu, Emanuel Temba, alikuwa miongoni mwa wanaCCM 400) wa Kijiji cha Enduleni akiwemo Mwenyekiti wao, Pettey Kitaika waliohamia Chadema na kukabidhiwa kadi jana na katibu wa Chadema mkoani hapa, Amani Golugwa.
Wakati Mwenyekiti huyo wa kijiji hicho, Kaita akisema ataeleza sababu za yeye kujitoa ndani ya chama hicho tawala mwishoni mwa wiki kwenye mkutano mkubwa utakaofanyika kijijini hapo utakaowashirikisha viongozi wa Chadema mkoa, Temba yeye alisema viongozi wa CCM hawashauriki na wamemeacha misingi ya kuanzishwa kwa chama hicho kwa sasa wanajilimbikizia mali na familia zao.
Alisema kuwa kuna wanachama wengi wa CCM toka vijiji vya jirani ambao nao wanatarajia kujiunga na Chadema siku hiyo ya mkutano ambao unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa wilaya na mkoa toka Chadema.
Temba alisema kuwa amevutiwa na operesheni hiyo ya vua gamba vaa gwanda ambayo imekuwa ikiwahamasisha wananchi kujua haki zao na kuikataa CCM.
Alisema kuwa viongozi wa CCM wamesahau kuwatumikia wananchi ambao kila kukicha maisha yao yanazidi kuwa magumu kutokana na kupanda kwa gharama za maisha kunakosababishwa na mfumuko wa bei za bidhaa.
“CCM hawashauriki mimi nilikuwa nikiongea kwenye vikao lakini hakuna anayesikiliza, nimeamua kuja huku (chadema) ili niweze kuongea kwa sauti, sina nia ya kugombea uongozi wowote nitashirikiana na wanachama wenzangu kuendeleza operesheni Vua gamba Vaa Gwanda” alisema Temba.
Naye mwana CCM mwingine Lucas Eliahu ambaye alitangaza rasmi kukihama chama hicho alisema kuwa amechoka kudanganywa kila siku maisha bora kwa kila Mtanzania huku maisha yanazidi kuwa magumu.
“Nimechoka hata nikifa acha nifie Chadema, ni bora kufia kwenye haki niweze kupumzika kwa amani kuliko kuendelea kukaa CCM ambayo haiwajali na inawakandamiza wananchi walio maskini kwa kutumia rasilimali za nchi kwa manufaa yao ” alisema Eliahu.
Kwa Prof Tibaijuka hoi
Huko Bukoba, Chadema kimeendeleza wimbohilo baada ya kuvuna wanachama wapya 112 katika jimbo la Muleba Kusini ambalo mbunge wake ni Prof. Anna Tibaijuka.
Huko Bukoba, Chadema kimeendeleza wimbo
Wanachama hao walipokelewa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Msalaba Mwekundu mjini Muleba juzi join, ambapo pia ulifanyika ufunguzi wa ofisi ya chama jimbo, na kufuatiwa na mkutano wa hadhara uliyoongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa Kagera, Wilfred Lwakatare.
Wengine waliohudhuria mkutano huo uliyofurika mamia na wananchi ni Mbunge wa Viti Maalum, Conchesta Rwamulaza (Chadema), Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake mkoa (Bawacha), Anna Mukono na madiwani mbalimbali kutoka vyama vingine vya upinzani wilayani humo.
Katika idadi hiyo ya wanachama waliojiunga na chama hicho, 45 walirudisha kadi kutoka vyama vingine vya siasa na 67 ni wapya. Hao ni 21 kutoka CCM, 11 wa TLP, 7 wa CUF na 6 kutoka NCCR Mageuzi.
Mwisho
Katika idadi hiyo ya wanachama waliojiunga na chama hicho, 45 walirudisha kadi kutoka vyama vingine vya siasa na 67 ni wapya. Hao ni 21 kutoka CCM, 11 wa TLP, 7 wa CUF na 6 kutoka NCCR Mageuzi.
Mwisho
Jaji Mkuu awashukia mahakimu
Na Datus Boniface
JAJI Mkuu Othuman Chande ameshangazwa na hatua ya mahakimu nchini, kung’ang’ania adhabu ya kifungo gerezani kwa wahalifu badala ya kuwatumikisha kifungo cha nje.
Huku, akiwataka wajiulize ni wahalifu wangapi wamepewa adhabu zao kwenye jamii nje ya magereza, na kitu kipi kinazuia kufanya hivyo.
Aidha, Jaji amesema kitendo hicho kinaingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya msongamano wa wafungwa mgarezani, hivyo taifa kutumia fedha nyingi.
Jaji Chande alisema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati akifungua mafunzo ya mahakimu wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu matumizi ya adhabu mbadala.
“Hebu tuyaache magereza yabaki kwa wale wahalifu hatari kama majambazi, wabakaji na wengine ambao tunaamini kwa hakika kuwa hawastahili kubaki kwenye jamii” alisema
Alisema miaka mingi mahakimu wamekuwa na mazoea kuona kuwa adhabu mbadala ya kifungo gerezani haitoshi katika kuwarekebisha wahalifu, na kupendekeza kutoa hukumu za vifungo vya magerezani pekee hata kwa makosa yanayostahili adhabu mbadala.
Katika maelezo yake, sheria za nchi zinatoa fursa kwa wafungwa kutumikia adhabu mbadala ya kifungo magerezani, lakini kwa bahati mbaya na kwa mazoea mahakimu wamekuwa hawapendi kuzitoa adhabu hizo.
Kwa mujibu wa kauli ya Jaji Chande, litakuwa ni jambo la kushangaza na aibu, kung’ang’ania utaratibu wa kizamani uliozoeleka.
Hivyo, alitaka mahakimu hao kubadili mtizamo huo, na kuwa tayari kwenda sambasamba na mabadiliko ya Idara ya Mahakama nchini ikiwemo kutumia kifungo mbadala.
Alienda mbali zaidi na kusema, takwimu zinaonyesha kuwa nchi jirani ya Kenya mwishoni mwa Machi, walikuwa na wafungwa 50,000 ambao wanatumikia vifungo mbadala, wakati Tanzania inatoa adhabu hiyo kwa wafungwa chini ya 900.
Aliwataka mahakamu wajiulize kwa nini Idara ya Mahakama nchini iko nyuma kiasi hicho ikilinganishwa na Kenya.
Alisema, adhabu mbadala hasa ya kutumikia jamii bila malipo mfano kutunza mazingira, ujenzi wa shule, zahanati, barabara, zimeonekana kuleta manufaa makubwa kwa jamii.
Aliongeza kuwa, matokeo ya tafiti nyingi zilizofanyika juu ya matumizi ya adhabu mbadala zinaonyesha wahalifu wanabadili tabia zao na kuwa watu wema kuliko wa wanaopelekwa magerezani.
Aliongeza, utafiti huo unaonyesha kwe upande mwingine kwamba, wahalifu wanaotoka magerezani wanakuwa wabaya kuliko walivyokuwa mwanzo, kutokana na kufundishwa tabia chafu magerezani.
Mwisho
JK kufukuza mawaziri
* NEC yanywea kwa shinikizo la wabunge
Na Edson Kamukara
BAADA ya vuta nikuvute ya muda mrefu ya wabunge kumtaka awawajibishe mawaziri wake, hatimaye Rais Jakaya Kikwete, amekubali kuwatimua wale wote waliotuhumiwa kwa ubadhilifu na kufanya mabadiliko makubwa katika serikali yake.
Katika kikao chake cha dharura kilichoketi jijini Dar es Salaam jana chini ya Mwenyekiti wake Rais Kikwete, Kamati Kuu ya CCM, iliafikiana na kubariki uamuzi wa kuwatimua mawaziri hao na maafisa wote wa serikali wanaotuhumiwa kwa ufujaji wa mali ya umma na kusuka upya kwa baraza hilo na taasisi zingine zilizoainishwa katika ripoti za Kamati za Kudumu za Bunge na ile ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).
Hatua hiyo inakuja zikiwa ni siku chache tangu Kamati ya Wabunge wa CCM katika kikao chake cha ndani kuwashinikiza mawaziri kadhaa waliotajwa moja kwa moja kwenye ripoti hizo kuachia ngazi.
Shinikizo hilo pia lilichagizwa zaidi na hatua ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (Chadema), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), kuwasilisha kusudio la kutaka wabunge wapige kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumalizika kwa kikao hicho cha CC, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kikao hicho kimechukua uamuzi huo kutokana na ukweli kwamba suala hilo ni zito na linahitaji kuweka mfumo mzuri wa utendaji na uwajibikaji serikalini.
Hata hivyo, licha ya Nape kusita kuwataja kwa majina mawaziri wanaotakiwa kung’oka, mawaziri walioshambuliwa bungeni na kutakiwa kutimuliwa ni pamoja na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mstafa Mkulo, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Prof. Jumanne Maghembe, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu na Naibu wake, Athuman Mfutakamba.
Wengine katika orodha hiyo ni Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda na naibu wake, Dk. Lucy Nkya, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk. Cyril Chami, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Mkuchika, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima.
Alipoulizwa ni kwa nini Rais angoje shinikizo la wabunge wa CCM na wapinzani ndipo achukue hatua ya kuwaondoa watendaji wabovu, Nape alitetea akisema kuwa si kweli kuwa mkuu huyo wa nchi ameshinikizwa, bali huo ni uamuzi wake na wao wameuridhia.
Alisema kuwa chimbuko la vuguvugu hilo ni hatua ya Rais Kikwete kuweka uwazi wa kuruhusu ripoti hiyo ya CAG iwasilishwe na kujadiliwa bungeni kwani imetoa mwanya kwa wabunge kuchambua kwa kina na kubaini watendaji wabovu.
“Rais amepokea taarifa na maazimio ya Kamati ya wabunge wa CCM na Kamati ya uongozi wa wabunge wa CCM juu kilichojitokea kwenye Bunge lililopita mjini Dodoma , taarifa hizo zimewasilishwa na kujadiliwa na CC,” alijigamba Nape na kuongeza kuwa;
Alisema kuwa Rais Kikwete aliwaeleza jinsi alivyojipanga kuchukua hatua za kuwawajibisha mawaziri na watendaji wa serikali na wale wa mashirika ya umma waliobainika kuhusika na ubadhilifu ulioanishwa na taarifa ya CAG, kamati za kudumu za Bunge na wabunge.
“Hivyo CC tumaridhia na kutaka uamuzi huo uchukuliwe mara moja, tuna imani kuwa Rais atafanya mabadiliko haraka iwezekanavyo maana alikuwa amebanwa na majukumu kidogo ya safari nje ya nchi, mazishi ya Rais Bingu wa Mutharika na sherehe za Muungano. Ila sasa wakati wowote atafanya,” alisema Nape.
Kuhusu ni funzo gani CCM imelipata kutokana na watendaji hao kugoma kujiwajibisha hadi mamlaka iliyowateua iwachukulie hatua, Nape alisema ziko aina mbili katika uwajibikaji yaani kujiondoa mwenyewe au kusubiri mamlaka ichukue hatua.
Hata hivyo alisisitiza kuwa chama hakijatikisika bali tukio hilo linaweka mfumo mzuri wa watu kujifunza utendaji wa uadilifu na kujiwajibisha pale wanapokuwa wamekwenda kinyume.
Wabunge CCM wapongeza
Baadhi ya wabunge wa chama hicho, wamepongeza hatua hiyo na kudai kuwa itarudisha heshima na nidhamu ndani ya serikali ambayo imeporomoka kiasi kikubwa.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe, alisema kuwa kilio chake na cha wabunge wenzake, hakikuwa na lengo la kumkoa yeyote wala kuleta madhara kwa chama chao, bali kilitokana na uchungu mkubwa walionao kwa watanzania na mali zao.
Filikunjombe alisema kuwa ajenda yao katika suala hilo , ilikuwa kuhakikisha kuwa serikali ya CCM inatekeleza kikamilifu ilani yake ya uchaguzi ambayo imelenga kuleta maisha bora kwa kila mtanzania, na hivyo, iliwaumiza zaidi baada ya kuona kuwa wapo baadhi ya wenzao kwa kutumia madaraka yao wamelenga kuiangamiza nchi kwa kutimia kofia ya chama.
“Hilo ndilo tulilotaka la kuhakikisha kuwa tunaisimamia serikali yetu iliyoaminiwa na watanzania kuwaongoza kwa kupambana na wenzetu waliotugeuka. Tutaendelea kupigania haki za watanzania, bila kuchoka” alisema mbunge huyo.
Mbunge mwingine ambaye aliomba jina lake lisitajwe gazetini, alidai kuwa uamuzi huo wa CC umempa faraja kubwa na sasa anaweza kurudi jimboni kwake akiwa na amani kubwa
“Siamini unachosema ndugu mwandishi. Kwa sasa sitaki utaje jina langu, langu, lakini kama ni kweli wamekubaliana hivyo, naweza kurudi jimboni kwangu kwa amani” alisema mbunge huyo.
Makatibu watano wateuliwa
Kamati Kuu ya CC, imewateuwa makatibu watano kukaimu nafasi za ukatibu katika mikoa mitano ya Geita, Njombe, Simiyu, Katavi, Kaskazini Magharibi.
Nape aliwataja walioteuliwa kuwa ni Hilda Kapaya, Shaibu Akwilombe, Hosea Mpagike, Alphonce Kinamhala na Aziz Ramadhani Mapuri, ambapo vituo vyo vya kazi vitapangwa baadaye.
Mwisho
No comments:
Post a Comment