Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Maaskofu wamtingisha Papa




VATICAN CITY

MAKAO Makuu ya Kanisa Katoliki Duniani (Vatican), yamewaonya maaskofu kutofanya mageuzi ya haraka kabla ya kupata baraka za kiongozi wao, Baba mtakatifu Francis.

Onyo hilo lilitolewa juzi, baada Dayosisi ya Ujerumani kusema kuwa wanandoa walioachana na kuoa tena, kanisa hilo sasa litawaruhusu kupokea sakramenti ya ekaristi na sakramenti nyingine.

Msemaji wa Vatican, Padri Federico Lombardi, alisema kuwa Papa Francis atafanya sinodi maalum  ya maaskofu Oktoba mwaka 2014, kujadili  masuala yanayoikabili familia.

Alisema kuwa hatua ya makanisa kujitangazia mageuzi yao wenyewe  yanaweza kusababisha mkanganyiko siku za usoni.

Inavyoonekana Papa Francis anaweza kuyatilia maanani changamoto zinazojitokeza kwa mujibu wa sheria za kanisa, hasa kuhusu watu waliooa kwa mara ya pili kuruhusiwa kupokea sakramenti ya Ekaristi

Papa Francis ameonekana kukubali uwezekano wa mabadiliko katika sheria za kanisa, zinazowakataza watu walioowa au kuolewa kwa mara ya pili kutoruhusiwa kupokea sakramenti kwa kuzingatia kuwa vifungo vya ndoa havitenguliwi, jambo ambalo Maaskofu wengi wanaliona kuwa tatizo kubwa katika majimbo yao.

 Jimbo kuu la Freiburg nchini ujerumani, wiki hii limetoa kitabu cha mwongozo kwa ajili ya mapadre wanaofundisha watu Wakatoliki waliooa mara ya pili (mitara) kuelezea masitikiko kama njia ya toba kwa kushindwa kuendelea na ndoa ya kwanza ili waruhusiwe kupokea Sakramenti ya Ekaristi Takatifu na Sakramenti zingine

Akiongea Vatican, Msemaji wa Papa Askofu Kardinali Lombard alisema Papa Francis hakuzungumzia mwongozo wa kitabu hicho cha jimbo kuu la Freiburg, lakini alisisitiza kuwa Papa alifanya majadiliano na Maaskofu wake kuhusu namna ya kufanya mabadiliko katika Kanisa.

Papa huyu, mzaliwa wa Agentina amelitikisa Kanisa tangu kuchaguliwa kwake mwezi machi mwaka huu kwa kuelekeza mabadiliko zaidi kwenye masuala ya msamaha kuliko masuala ya utoaji mimba na ndoa za jinsia moja mahali ambapo ndio kuna changamoto za wazi kwenye mafundisho ya Kanisa hilo kongwe duniani.
Hata hivyo anaonekana kupokea ushauri wa wasaidizi wake kwa karibu na wamesisitiza mara kuwa mabadiliko hata kama yatatokea yatachukua muda kufikiwa.

Katika hali isiyotarajiwa, Askofu Mkuu wa Freiburg Robert Zollitsch, ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu nchini ujeruman alipokea mitazamo miwili tofauti wiki hii iliyojihusisha hasa na  hoja ya
Kuonesha namna gani watu wapo makini katika maisha yao ya imani wanaweza pia kutumia muda wao kushiriki katika maisha ya Kanisa, alisema Alis Glueck Rais wa Kamati kuu ya wakatoliki nchini Ujerumani

Kardinali wa Munich, Reinhard Marx mmojawapo kati ya makardinali nane walioteuliwa kama washauri wa Papa alikiita kitabu hicho cha mwongozo cha Freiburg kuwa ni “mchango katika mjadala usiokwisha” na kusisitiza kuwa suala hilo litatatuliwa kwa manufaa ya Kanisa zima ulimwenguni.

Maaskofu nchini Ujerumani wamekuwa wakitoa maombi mara kwa mara kuiomba Vaticani iruhusu watu kutengana na watu kuruhusiwa kuoa au kuolewa mara ya pili katika miaka ya hivi karibuni kufuatia waumini waliooa mara ya pili au kutoolewa mara ya pili kuhudhuria misa lakini wakiwa hawaruhusiwi kupokea sakramenti ya Ekaristi.

Kitabu hicho cha mwongozo kimesisitiza kuwa Wakatoliki wanapaswa kukubali kuwa kuna ndoa ambazo hazijafanikiwa, zimeshindikana hivyo wanapaswa kuzijadili na mapadre wao lakini waonyeshe kwa imani kuwa watakuwa waaminifu kwa ndoa zao za pili na ni haki wao kuwa na familia za aina hiyo, maana ndoa hizo pia zina roho wa Mungu kwani zinategemea imani binafsi ya mtu kwa mwenzake na ushiriki wao kwenye maisha ya Mama Kanisa


No comments:

Post a Comment