Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Magufuli agomea wamiliki wa Malori

Magufuli agomea wamiliki wa Malori
WAZIRI wa Ujenzi Dk John Magufuli amesema atahakikisha kuwa anasimamia sheria ili jitihada zinazofanywa na serikali za kudhibiti uharibifu wa barabara hazidhoofishwi na watu wachache wenye nia ya kujinufaisha binafsi bila kuja maslahi ya Taifa.

Kauli hiyo ni muendelezo wa mvutano kati ya wizara hiyo na  Wasafirishaji wa mizigo ambao wanapinga sheria ya tozo ya asilimia tano kwa Wasafirishaji wanaozidisha mizigo na kusababisha uharibifu wa barabara.

Akizungumza kwa niaba ya waziri huyo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Wizara hiyo, Martin Ntemo  alisema nia ya serikali sio kuwatoza faini wasafirishaji hao bali anachokusudia nikuwaona wasfirishaji hao wanakuwa wazalendo katika kulinda barabara nchini.

Alisema hivi karibuni kumejitokeza wasafirishaji wasio waaminifu waliokuwa na mawasiliano ya karibu na watendaji wa zamani waliokuwa wakishirikiana nao kupitisha mizigo kinyume na taratibu.

“Mianya hiyo kwa sasa imezidi kudhibitiwa na hali kwa sasa ni nzuri tofauti na awali kabla ya kupitisha zoezi la kuwabadilisha wafanyakazi takriban 400 ambao ni sawa na asilimia 85 ya watumishi wote katika vituo hivyo na kuajiriwa wapya”alisema.

Hatua hiyo ya kubadilishwa kwa watendaji hao inaelezwa kuwa ni chanzo kingine cha malalamiko kutoka kwa baadhi ya wasafirishaji hao wakishirikiana na watenaji wasiokuwa waaminifu.  

Aidha, Ntemo alizipongeza baadhi ya kampuni za usafirishaji kuwa mfano wa kuigwa, kampuni hizo ni Dar Express, Cargo Star, Hood bus, Coca Cola, BM Coach, Bakheresa (AZAM Transport), TBL, Golden Coach, Kanji Lanji bus, Taqwa, Consolidated Logistic, Lamada na Puma.

“Kumbukumbu ziliofanyiwa uchambuzi kwa kipindi cha miaka kumi zimebainisha kuwa yapo makampuni ambayo hayana rekodi ya kuzidisha mizigo wakati wote yanapopimwa katika vituo vya mizani ya barabarani”alisema.

Wamiliki

WAMILIKI wa malori wamemtunishia misuli Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, na kueleza kuwa wao hawajagoma ila wameamua kupaki malori yao ili wasiendelee kuharibu barabara.
Wamiliki hao walieleza kuwa Waziri huyo amerudisha tozo ya asilimia tano kwa maslahi yake na amekuwa mtu ambaye haambiliki, ashirikiani na wadau pamoja na kujichukulia sheria mkononi.
Wakizungumza jana jijini Dar es salaam, wamiliki hao walieleza kuwa sheria hiyo iliyotangazwa na Magufuli kuanza kutumika Oktoba mosi, wao walipatiwa barua Oktoba 2 na kueleza kuwa tozo hiyo imeondolewa hali iliyosababisha msongamano.
Karim Radha ni Mkurugenzi wa kampuni ya Consolidated Ltd alisema kuwa wanaomba sheria hiyo ifuate utaratibu wa kwenda bungeni na kupitishwa .
“ Anasema washafirishaji tunataka faida kubwa huo ni uongo na sheria ya tozo ipo nchi nyingi hata kwenye muunganiko wa nchi za Afrika mashariki, na hata nchi zilizo katika umoja wa SADC, aseme kuwa anaogopa barabara zake hazina viwango hivyo zitaharibika ,”alisema.
Davis Mosha kutoka Delina Group, alisema kuwa wao hawabishani na kiongozi ila waziri hana dhama ya kuvunja sheria iliyopo miaka 40 iliyopita.
“ Hatutaki kukurupuka kwenda mahakamani kama ambavyo waziri alisema, tunasubiri majibu, pia sisi hatupo kisiasa wala hatutumiki, hatujagoma ila tumepaki vyombo vyetu,”
Ibrahim Ismail alisema kuwa tozo hiyo ilikuwepo kutokana na mizani zote kutokuwa na viwango sawa.
Alisema kuwa Dk. Magufuli hapaswi kuwasukumia wasafirishaji mzigo kuwa wanaharibu barabara aseme tatizo lililpo na ukweli uonekane.
Faisal Edha alieleza kuwa wao kama watanzania wana uchungu na nchi na hawatakubali kuharibu barabara hivyo ni vyema Waziri akasimamia ujenzi wa uhakika wa barabara zilizo imara.
“Kwa mfano sasa baada ya kutengua tozo hiyo magari mengi yanayotoka Afrika kusini yamekwama Tunduma wakiwa wanaleta mzigo mgodini, hayo ni madhara, lakini bandarini pia mizigo inazidi kuongezeka, matokeo yake mchi inakosa maendeleo na hawatendei haki watanzania”aliongeza.
mwisho

No comments:

Post a Comment