Na Charles
Misango
Udhalilishaji wa dini nyingine?
NIANZE kwa
kuungana na wananchi wote duniani walioweza kutamka, kusikitika na kulaani
filamu ya mmarekani mmoja ambayo inaelezwa kukashifu imani ya dini ya Kiislamu.
Naungana nao
kwa sababu mimi ni miongoni mwa wanaoamini uhuru wa kuabudu na kuheshimu sio
mawazo tu, bali hata imani ya mwingine hata kama kwangu sikubaliani nayo.
Filamu hiyo imeleta
madhara makubwa katika baadhi ya nchi nyingi duniani. Kumefanyika maandamano
makubwa katika nchi hizo, lakini lililo baya zaidi, kumetokea vifo vya watu
wengi wasiohusika, wala hawakuwa na taarifa yoyote juu ya kuwepo kwa filamu
hiyo.
Waliokufa
wengine hata huyo mtengeneza filamu hiyo hawamjui wala hawajawahi kumwona.
Wameponzwa na kitu wasichokijua. Wamekufa! Wamekwenda! Hawatarudi tena!
Hapa nchini
tukio hilo halikupita bure. Viongozi
wengi wa Kislamu walitoa matamko ya kulaani filamu hiyo. Tumshukuru Mungu
kwamba, kwa busara za viongozi hao, walifanikiwa kufikisha ujumbe wao bila kuhamasisha
waumini wao kufanya vurugu na maandamano ambayo kwa namna yoyote yangeleta
balaa.
Narudia.
Nakubaliana na kuungana kwa dhati na wale wote waliolaani filamu hiyo, ingawa
nimesikitishwa sana na vifo vya watu wasio na hatia wala kuhusiana na
mtengenezaji kwa namna yoyote ile, kwa sababu maisha yao yamekatishwa bure.
Nasikitika pia juu ya uharibifu wa mali uliofanywa na wenzetu ambao
wamechukizwa na filamu hiyo. Nina uhakika, walioharibiwa, masikini ya Mungu
hawana mchango wowote na uwepo wa filamu ya kumkashifu Mtume Mohammed (SAW).
Ni tukio
jingine baya kama lile la kile kitabu cha AYA ZA SHETANI kilichotungwa na
Salmine Rushidde miaka ile ya 90. Wenye kumbukumbu njema wanajua kile
kilichotokea duniani kwa wake ule.
Bila
kujikomba kwa yeyote, kitabu, filamu, chapisho lolote lile ama hata mahubiri
yanayodhalilisha, kutukana na kukashifu imani ya dini ama dhehebu jingine,
hufanywa na mtu ama watu wasiojali imani za wengine. Hufanywa na watu waliokosa
staha, wabinafsi, wachoyo, wenye upeo mdogo wa kufikiri, na mbaya zaidi wasiosumbua
akili zao kuona madhara yatakayotokana na matendo yao katika jamii.
Suala la
imani ya dini ni zito kwa maana ya uzito! Linalogusa uhai wa mtu. Kucheza na
imani ya mtu ni kucheza na roho ya mtu, hivyo, kwa namna yoyote ile linahitaji
kuchukuliwa kwa uzito na kila mtu. Kila anayetambua kuwa ni muumini wa dini ama
dhehebu fulani, anajua kuwa kile anachokiamini ndicho bora, safi na sahihi
kuliko cha mwingine. Kwake, wale wasioamini kama yeye waliopotea.
Kumbe, mtu
makini anayejali wengine, sharti awe mwangalifu na mwenye staha anapojaribu
kugusa imani ya mtu mwingine. Watu
waliojaliwa kuwa na upeo wa kufikiri, wenye kujali utu na hadhi ya wengine,
kamwe huwasikii katika kutangaza imani zao wakigusia kwa namna ya kudhalilisha
na kuudhi imani za wengine. Daima watazama kuhubiri, kufundisha na kutangaza
kile wanachoamini wao. Wataonesha uzuri wa dini zao, watanogesha tunu ya dini
zao, na watatoa matumani ya baadaye yanayopatikana kwa wale waliondani ya dini
zao na watakaojiunga nazo baadaye.
Wakati sote
tunaungana kulaani filamu hiyo inayoudhalilisha uislamu na Mtume Mohammed
(SAW), hapa nchini na hususan katika jiji la Dar es Salaam, kwa miaka kadhaa
sasa kumeibuka kundi la watu ambao bila woga, wala kujali na kuheshimu uhuru wa
kuabudu na imani ya dini nyingine, wamekuwa wakiendesha mahubiri dhidi ya dini
nyingine kwa lugha zilizojaa matusi, kejeli, dhihaka na udhalilishaji wa hali
ya juu.
Kundi hili,
limefanya hivi mchana kweupe na wanaendelea hadi nyakati za usiku, wakitumia
vipaza sauti vyenye nguvu kubwa na hivyo, matusi yao husikika kwa umbali
mkubwa. Watu hawa ambao huendesha mambo yao kwa mtindo wa maswali, ni mabingwa
wa lugha chafu zilizojaa mafundisho ya uongo wa kutisha! Wanatukana
wanavyotaka! Mathalani, wanadiriki hata kuita kuwa watu wa dini hiyo ni wajinga
na ndio maana kengere zao hulia…’wajinga njoo, wajinga njoo’ wameitwa makafiri
mara nyingi mno!
Swali la
kujiuliza, nani kawapa mamlaka ya kutukana na kudhalilisha dini za wengine?
Jeuri ya kufanya haya yote bila kujali, inatoka wapi? Hivi ikiwa wao hawako tayari kuona mtu yeyote
anadhalilisha dini, imani na kiongozi wao mkuu, na wako tayari kupambana hata
kumwaga damu kutetea imani hiyo, iweje kwao iwe ruksa kusema, kuhubiri na
kuendesha mihadhara inayotukana dini za wengine?
Hivi kama
sio busara na uvumilivu wa wale wanaotukanwa, ama leo hii nao wakasema yatosha
na wakaamua kutetea imani yao kwa njia yoyote dhidi ya wale wanaowatukana, je,
itakuwa nchi ya kukalika tena? Kwa nini
basi, wale viongozi makini, wanaojali na kuheshimu uhuru wa dini ya wengine;
kwa nini viongozi wa serikali walio na wajibu wa kulinda uhuru wa watanzania
wote wakae kimya wakiwaacha watu wachache WASIOJALI kutamba kwa matusi dhidi ya wengine? Nyote hakuna asiyejali hali
hii?
mwisho
No comments:
Post a Comment