Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

MEYA AMWOKOA MKURUGENZI


MADIWANI wa Manispaa ya Kinondoni jana nusura wamuwajibishe mkurugenzi wa manispaa hiyo Fortunatus Fwema kwa madai kuwa ameshindwa kusimaia kazi za maendeleo  alizopaswa kufanya katika robo ya tatu nya mwaka na kuzitolea taarifa.
Kufuatia maazimio hayo ilimlazimu Meya wa Kinondoni Yusuph Mwenda awaombe madiwani hao pasipo kujali vyama vyao wampe muda  mkurugenzi huyo, hadi kikao kijacho cha baraza hilo awe ameandaa ripoti itakayoonyesha kazi aliyoagizwa asiamaie kupitia kamati mbali mbali za baraza hilo.
Hali ya kutaka kumuwajibisha Mkurugenzi ilianzia wakati madiwani wa manispaa hiyo waliokuwa katika kikao cha kawaida kupitia muhtasari wa kikao kilichopita na kutaka kujua manispaa imefanya nini katika maeneo ya wazi ambayo yalikubaliwa yalindwe na taarifa zitolewe katika kikao kinachoendelea.
Mbali na taarifa hiyo pia madiwani hao walitaka ufafanuzi wa ujenzi wa nyumba mbali mbali zinazoendelea katika manispaa ya Kinondoni pasipo kuwa na vibali vya ujenzi huku manispaa ikiwa haichukui hatua zozote za kushughulika au kuwawajibisha wahusika.
Diwani wa Ubungo Boniface Jackob.(Chadema) alikuwa wa kwanza kuongea na kumuomba mwenyekiti wa kikao hicho Yusuph Mwenda amuagize mkurugenzi kutoa taarifa ya maazimio ya kamati mbali mbali juu ya kuyalinda maeneo ya wazi ya halmashauri ya manispaa ya Kinondoni.
Abbas Tarimba diwani wa Hananasifu (CCM)alisema katika ujenzi holela unaoendelea katika manispaa ya Kinondoni ni wazi watendaji wanachangia kwa kuwa hawachukui hatua na kwamba ni wakati muafaka kwa baraza la madiwani kuonyesha mfano kwa kuwawajibisha watendaji wanaoshindwa kusimamia wajibu wao huku wakiendelea kupokea mishahara ambayo ni kodi ya wananchi.
“Tusiwe wasemaji ambao hatuna maamuzi tutoe mfano kwa kuwawajibisha watendaji hawa hatujui hawa building Inspector (wakaguzi wa majengo) wanafanya nini kwa maana nyumba hizi zisizo na vibali zinaendelea kujengwa kila siku na haifanyiki katika giza” alisema Tarimba
Paschal Manota diwani wa Kimara (Chadema)alisema kama kuwawajibishga watendaji ni lazima waanze na mkurugenzi kwa kuwa ameshindwa kuhakikisha maagizo ya kamati yanatekelezwa huku akieleza maagizo ya kamati mabli mbali yanayotakiwa kufanyiwa kazi yamekuwa ni kama ngonjera katika masikioya watendaji.
Renatus Pamba ambaye ni diwani wa Sinza(Chadema)alitaka baraza lifahamishwe ni lini  na hatua gani zitachukuliwa kwa  maeneo ya wazi ya manispaa hiyo ambayo yamejengwa na hayana nyaraka
Diwani wa Msasani Aisha Sagamwiko (CCM)alisema licha ya kumtaarifu mkururugenzi juu ya ujenzi unaoendelea wa nyumba ya ghoarofa tatu lkatika eneo lake pasipo kuwa na vibali hakujafanyika jitihada zozote za kuzuia au kuangalia kama jengo hilo lipo kihalali na matokeo yake wahusika wanamalizia bati pasipo kuulizwa uhalali wa ujenzi huo.
Kwangu mimi pale Msasani  jengo la ghorofa tatu limanza msingi nikatoa taarifa kuwa linajengwa na haionyeshi mtaalamu ni nani na muhusika ni yupi lakini mpaka leo hakuna kinachofanyika sasa tunasubiri waje wahamie kwa matarumbeta huku manispaa ikiwa imelala”alisema.
Kwa upande wake Ester Samanywa, viti maalum Chadema alitaka kujua kama kuna mamlaka zaidi katika kumiliki ardhi ya manispaa ya Kinondoni kwa kile alichoeleza majengo katika maeneo ya Kawe Beach yanaendelea kujengwa huku wahusika wakiwa hawatekelezi maagizo ya manispaa kusitisha ujenzi wa maneneo hayo.
Kufuatia hoja hizo madiwani walisikika wakipaza sauti ya kutaka mkurugenzi awe wa kwanza kuwajibishwa na kasha wafuatie watendaji wa chini yake.
Kutokana na hali hiyo Mwenda alitaka majibu kutoka kwa mkurugenzi ambapo alisema maeneo ya wazi yanatarajiwa kuwekewa vibao vya kuonyesha kuwa hayaruhusiwi kuvamiwa na kwamba taarifa ya kamati mbali mbali atazitolea maelezo katika kikao kijacho.
Majibu hayo yaliamsha yowe katika ukumbi huo wa manispaa ya Kinondoni kwa madiowani kupaza sauti kuwa wanajibiwa kisiasa na kwamba hawaridhiki na majibu hayo, hali iliyomfany Mwenda awaombe wawe na subira mpaka kikao kijacho ndipo wachukue hatua kama hakutakuwa na utekelezaji.
“Tunatambua kuna udhaifu  katika kusimamia maeneo ya wazi katika maispaa yetu na hili halifdichiki nianachoweza kuwaomba ni kutoa muda kwa mkurugenzi kama alivyosema  na hapo tutaangalia way forward(nini kitafuata)alisema Mwenda
Mwisho



No comments:

Post a Comment