Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Mgomo waingiza hasara ya bilioni 20



WAMILIKI wa Malori nchini wamesema kuwa Serikali imepata hasara ya sh bilioni 20 hadi 30 kufuatia kusitishwa kwa huduma kwa madai ya kulinda barabara zisiharibike.
Mbali na hasara hiyo wamiliki hao wamemuomba Rais Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhakikisha wanamchukulia hatua za kinidhamu Waziri wa Ujenzi John Magufuli kutokana na kupotosha suala hilo na kutoa maneno yasiyo na busara kwa Watanzania
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, kwa niaba ya wenzake mwakilishi wa wamiliki wa malori, Azim Dewji, alisema kuwa Serikali imepoteza mapato hayo kutokana na uwongo wa kiongozi mmoja.
Dewji alisema kuwa hasara waliyoipata wamiliki hao ni kubwa na sasa wapo katika kufanya mahesabu ili kubaini hasara hiyo ikiwa ni pamoja na kumchukulia hatua za kisheria Dk Magufuli na kumfungulia mashtaka.
“Serikali tu imepoteza zaidi ya bilioni 20 na mama lishe nayo wameshindwa kufanya kazi zao huko bandarini ni ajabu kuwa na kiongozi anayetesa Watanzania kutokana na uwongo wake,” alisema
Mkurugenzi huyo wa makampuni ya malori ya Simba, alisema kuwa wamiliki wa mamlori wamekuwa na mchango mkubwa katika uchumi wan chi na wametoa ajira kubwa kwa Watanzania.
Alisema kuwa kwa kipindi cha siku mmoja malori zaidi ya 1000 yamekuwa yakifanya safari nchini na kuingiza fedha nyingi kwa Serikali.
Alisema kuwa ni muhimu Dk Magufuli akatoa maneno yenye hekima na busara na sio kutumia mabavu na kutoa maneno ya kejeli dhidi ya Watanzania.
Mmiliki huyo alisema kuwa kiongozi huyo amewadhalilisha kwa kueleza kuwa wamekuwa wakitoa rushwa kwa wafanyakazi wa mizani jambo ambalo halina ukweli wowote.
“Hivi kama sio uwongo na upotoshaji unaofanywa na kiongozi huyo ni nini…hivi kweli ni mfanyabiashara gani aliyetayari kutoa rushwa ya fedha kwa vituo vya mizani zaidi ya 14 vilivyopo katika Dar es Salaam hadi Tunduma na anayeshindwa kuangalia faida,” alihoji
Mmiliki huyo alisema kuwa ni vyema kiongozi huyo akatumia vyombo vya dola kufanya uchunguzi juu ya masuala mbalimbali yanayohusu barabara kuliko kutoa kauli za ubabe na za kupotosha.
Alisema kuwa fedha ya faini ya kuzidisha mzigo haizidi sh elfu 50,000 hivyo hakuna mfanyabiashara anayeshindwa kutoa kiwango hicho.
Dewji alisema kuwa kutokana na kupotosha umma juu ya tozo hiyo ni vyema Rais Kikwete akamuondoa waziri huyo katika baraza lake na kumrudisha kufanyakazi za chama.
“Dk Magufuli anafaa sana kufanyakazi za propaganda katika chama chake naamini nafasi hiyo ataimudu vyema na ndiyo inayomfaa kuliko kuwa waziri kwa kuwa amemdanganya Waziri Mkuu Pinda juu ya suala hili,” alisema
Alisema kuwa kiongozi ni mtu anayepaswa kusaidia watu na sio kutoa kauli za kukomesha Watanzania.
Alisema kuwa Dk Magufuli amekuwa na chuki na wamiliki wa malori baada ya kubaini kuwa walikutana na Kamati ya Miundombinu kipindi cha Bunge na kueleza changamoto zinazowakabili.
Waziri Mkuu Pinda juzi aliagiza wamiliki wa malori kuyaruhusu magari yao yasafirishe mizigo kwa utaratibu wa zamani.
Siku kumi zilizopita Dk Magufuli , alitangaza kuanza kutumika kwa kanuni namba 7 (3) ya Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 2001.
Sheria hiyo inayataka malori yote yanayozidisha uzito uliopo ndani ya asilimia tano kupunguza mzigo, kupanga mzigo upya au kulipia uzito uliozidi mara nne ya tozo ya kawaida.
Mwisho   

No comments:

Post a Comment