Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Pinda amuumbua Magufuli *Aruhusu malori yaendelee na utaratibu wa zamani



WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amemuumbua waziri wake wa Ujenzi John Magufuli, kwa kuruhusu wamili wa Malori waendelee kusafirisha mizigo kwa utaratibu wa zamani.

Pinda ametoa agizo hilo jana, ikiwa ni siku chache tangu Waziri Magufuli alipoweka msimamo na kuagiza wasafirishaji watakaokaidi agizo la kulipa asilimnia tano ya uzito unaozidi kwa mujibu wa kanuni namba 7 (3) ya Sheria ya Usalama Barabarani ya mwaka 2001, wasiingize magari yao barabarani.

Hata hivyo, agizo la Magufuli limezua mtafaruku mkubwa, baada ya karibu wasafirishaji wote nchini kusimamisha shughuli zao, kiasi cha kuzusha hofu ya kuanguka kwa uchumi nchini. Hadi sasa kiasi kikubwa cha mizigo kimekwama bandarini na sehemu nyingi za nchi kufuatia mgomo huo.

Pinda, katika agizo hilo ambalo limepokelewa kwa shangwe kubwa, alisema mwaka 2006 aliyekuwa Waziri wa Miundombinu Basil Mramba aliandika waraka wenye kumbukumbu namba CKA/16/419/01Julai 19/2006 ambao iliyotoa msamaha wa tozo ya magari kwa uzito uliozidi asilimia tano ya uzito unaokubalika kisheria.

amewataka watendaji wa serikali kuhakikisha wanawashirikisha wadau kila wanapotaka kufanya mabadiliko ya jambo fulani kwa manufaa ya nchi na kuepusha ghasia na migogoro isiyo ya lazima.


“Mramba alizingatia maombi ya wadau wa usafiri, ingawa ni kinyume cha sheria. Naye alifanya kwa nia njema,” alisema Pinda na kuongeza kuwa sheria anayoikazania Magufuli haitekelezeki kirahisi kutokana na hali halisi ya barabara zetu na mizani kulalamikiwa kuwa na matatizo katika upimaji hivyo kutaka wadau hao kupewa muda kabla ya kuanza kwa utekelezaji wa sheria hiyo.


“Baada ya kelele hizi niliamua kukutana na Waziri Uchukuzi, Ujenzi, Wakala wa Barabara (Tanroads) na watendaji wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kwa ufafanuzi zaidi wa kisheria, na nikakutana na wadau wa usafirishaji TATOA na TABOA katika kikao hicho nao walisema yao nikawaelewa. Nikaona tatizo ni utekelezaji wa sheria yenyewe,” alisema.

No comments:

Post a Comment