Mbunge wa Jimbo la Kawe Halima Mdee, Chadema amemshauri
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa, Philip Mangula kuhama katika
Jimbo hilo kama anaona ni vibaya kukaa katika Jimbo linaloongozwa na Chadema,
kwani mkakati uliopo sasa sio kurejesha Jimbo hilo CCM bali kuhakikisha Wilaya
nzima ya Kinondoni inaongozwa na Wabunge wa Chadema katika majimbo yote
Mdee pia amemshauri Mangula kama anataka mchango wa uzee
wake utambulike aende kwanza Dakawa yeye na wana CCM wenzake wanapotuhumiwa
kumiliki maeneo makubwa ya ardhi ya wananchi wanyonge waliyojipatia kinyume cha
taratibu ili awe safi kutoa ushauri kama mzee.
Kauli hiyo ya Mdee inafuatia kauli iliyotolewa na Mangula
akisema anajuta na anaona aibu kuishi katika Jimbo la Kawe linaloongozwa na
Halima Mdee (Chadema), na kuwataka wanachama wa CCM kuhakikisha uchaguzi wa
mwaka 2015 jimbo hilo linarudi kwao.
Mangula aliyasema hayo juzi alipozungumza na viongozi mbalimbali wa kata na wilaya zote za jijini Dar es Salaam pamoja na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam wa CCM.
“Ni aibu mimi ni mkazi wa Oysterbay jijini Dar es Salaam, na Mdee ndiye Mbunge wangu sasa siku akisema anataka kuongea na wazee wa jimbo lake mimi ntafanyaje? siwezi kwenda nitasingizia naumwa ili nisiende” alinukuliwa Mangula.
Mangula aliyasema hayo juzi alipozungumza na viongozi mbalimbali wa kata na wilaya zote za jijini Dar es Salaam pamoja na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam wa CCM.
“Ni aibu mimi ni mkazi wa Oysterbay jijini Dar es Salaam, na Mdee ndiye Mbunge wangu sasa siku akisema anataka kuongea na wazee wa jimbo lake mimi ntafanyaje? siwezi kwenda nitasingizia naumwa ili nisiende” alinukuliwa Mangula.
Mdee amesema Chadema ina madiwani wachache kuliko wale wa
CCM ambao huwa hawahudhurii hata vikao kubuni mapato ya Halmashauri, ndio maana
tangu wawepo wabunge wa Chadema wilaya ya Kinondoni mapato sasa yameongezeka
kutoka Bilioni 10 hadi Bilioni 25 na kuna uwezekano wa mapato hayo kuongezeka
zaidi kadiri madiwani wa CCM wanavyopungua kwani madiwani wa Chama hicho bado
wanalinda ulaji wao na wabunge wa chama chao.
Alimshangaa Mangula kwa kutaka majimbo yaliyoko Chadema
yarudishwe CCM kwani wabunge wa Chama cha Mapinduzi hawahudhurii vikao na
hawawakilishi wananchi wao na kushindwa
pia kuhudhuria mikutano muhimu ya maamuzi ya mapato na matumizi kwenye
Halmashauri zao.
Mdee vile vile alisema Mangula hana nia nzuri na maendeleo
ya wananchi, angekuwa na nia nzuri asingependa majimbo yarudi CCM ambayo
wawakilishi wake huwa hawaendi hata kwenye mikutano.
“Wazee wengi wa Chama cha Mapinduzi, kama Msekwa, Kinana,
Magufuli hata Rais Kiwete Mwenyewe, makazi yao yapo Kawe, usalama wa Taifa
makao yao yapo Kawe, Mawaziri wote wapo Kawe na wananipa ushirikiano wa kutosha
kusaidia maendeleo ya Jimbo la Kawe kinachomsumbua Mangula mimi sikielewi
anaendekeza siasa hata katika maendeleo, tutaiga nini kwa mzee huyu.
Aliongeza kuwa ameingia madarakani, amejitahidi kusimamia
ujenzi wa barabara kuu na barabara ndogo maeneo ya Mbweni, Mabwepande na Bunju,
maeneno ambayo yalikuwa hayana huduma za kijamii kama maji, umeme na barabara.
Mdee alisema, ni kutokana na utendaji mzuri wa wabunge wa
Chadema, Wilaya ya Kinondoni sasa imepanda kimapato na pesa zinazopatikana
asilimia 60 zinaenda kwenye shughuli za maendeleo, tofauti na ilivyokuwa awali
ambapo Wilaya yaTemeke ilikuwa inaongoza ikifuatiwa na Ilala.
Mdee aliongeza kuwa Mangula anachukizwa na utendaji bora wa
wabunge wa Chadema kwani hauonyeshi matumaini kama CCM wanaweza kuyarejesha
majimbo hayo siku za hivi karibuni.
“Jimbo la Kawe halitarudi CCM siku za hivi karibuni, akiona
hawezi kuhama Kawe basi ahame Chama ili aweze kuwa huru, lakini Jimbo la Kawe
litakuwa ndio chachu ya kusaidia majimbo mengine ya Wilaya ya Kinondoni
yachague Chadema”.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment