Mzazi wa Kiemba aja juu
Na Bilal
Soud
BABA Mzazi wa Kiungo mahiri wa Simba na timu ya
taifa, Taifa Stars Amri Kiemba
aliejitambulisha kama Tano Ramdhani almaarufu (Shungo), amesema kua
Simba inambania kijana wake kucheza soka la kimataifa.
Akiongea na
gazeti hili jana asubuhi posta, shungo amedai kua timu ya simba imekua ikiweka
vikwazo vya kutomruhusu kijana wake kucheza
soka la kulipwa nje ya nchi, hii inatokana na ukweli kwamba kijana wake
huyo alihitajika na timu ya Moroko iitwayo FAR Rabat.
Akithibitisha
hayo Shungo anasema kwamba simba walikataa ofa hiyo na wamekuwa wakitumia
mbinu ya kuweka dau kubwa ili kukwamisha
usajili huo, imedaiwa simba wamehitaji kiasi cha sh milioni 250 kwa timu
itakayo hitaji huduma ya kiungo huyo.
Akitilia
mkazo kauli yake alisema “ Amri Kiemba amekua wa kwanza kuhitajika kabla
ya Shomari Kapombe laikni nashangaa
kuona Kapombe akiruhusiwa na kuondoka kwenda Uholanzi kwa majaribio na mwanagu
akibaki kaika tetesi tu inauma sana.”
Kiemba ni
fauda kwa Tanzania hivyo kucheza kwake soka la kimatifa litampaizoefu wa
kutosha na kupausha jina la nchi yetu hivyo Simba watumie malalamiko haya
kupitia vizuri maamuzi yao.
Mwisho
Yanga kuanika
vifaa vipya leo
MABINGWA wa soka Afrika
Mashariki na Kati, Yanga, leo wanatarajia kutambulisha nyota wake wawili wa
kimataifa kupitia mechi ya kirafiki dhidi ya JKT Ruvu itakayochezwa kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam .
Nyota hao wamekuja kuziba
nafasi ya Mzambia Davies Mwape na Mghana Keneth Asamoah waliotemwa hivi
karibuni, hivyo Yanga kubaki na nyota watatu wa kimataifa, Mghana Yaw Berko,
Mrwanda Haruna Niyonzima na Mganda Hamis Kiiza.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam jana, Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu,
alisema nyota hao wapya
ambao hakupenda kuwataja, wataonekana katika mechi
hiyo ya kirafiki ambayo
ni kipimo kwa wakali hao wa Jangwani kabla ya Kagame.
Mechi hiyo inafanyika
kutokana na ombi la Kocha Mkuu wa timu hiyo, Tom Seintfiet, akitaka kupima kama
vijana wake wameshika mafunzo aliyowapa kwa siku tano kuanzia Alhamisi
iliyopita.
Kuhusu nyota hao wapya,
Sendeu alisema ni mapema mno kutaja majina na wanatokea wapi, akiwataka wapenzi
na mashabiki wa soka kujitokeza kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
kujionea nyota hao na ubora wa kikosi hicho kwa ujumla.
“Siwezi kuwataja majina wala wanatoka wapi, lakini ukweli ni kwamba
kesho (leo)
ndio tutawaweka wazi nyota wetu wawili wa
kimataifa watakaoziba nafasi za Mwape
na Asamoah,” alisema
Sendeu.
Sendeu aliongeza kuwa maandalizi
ya mechi hiyo yamekamilika na amewataka wapenzi na mashabiki kujitokeza kwa
wingi jioni ya leo kujionea wenyewe uwezo wa kila mchezaji, wasisubiri
kuhadithiwa.
Aidha, mechi hiyo itakuwa
wa kwanza kwa kocha huyo mpya Mbelgiji, Saintfiet tangu ajiunge nayo mwishoni
mwa wiki iliyopita kwa mkataba wa miaka miwili akirithi mikoaba ya Mserbia
Kostadin Papic.
Saintfiet aliyeikuta timu
hiyo ikijiandaa na michuano ya Kombe la Kagame itakayochezwa kwenye uwanja wa
Taifa na Chamazi, jijini Dar es Salaam, anakabiliwa na mtihani wa kutetea taji
hilo ililolitwaa Julai 10, 2011.
Yanga iliyo kundi C,
lenye pia timu za APR ya Rwanda na Wau Salaam ya Sudan Kusini, itaanza kampeni yake siku ya ufunguzi wa
michuano hiyo, Julai 14 dhidi ya Atletico ya Burundi.
Katika hatua nyingine,
mratibu wa mechi hiyo, Salum Mkemi, kiingilio cha chini kitakuwa ni sh 3,000
kwa viti vya kijani na bluu; viti vya rangi
ya chungwa sh 5000; VIP B na C ni sh 10,000 na VIP A watalipa sh 15,000.
Kocha Yanga
afagilia amani
KOCHA
mkuu wa timu ya Yanga, Mbelgij Tom Seintfiet, amefurahishwa
na
tunu ya amani iliyopo Tanzania kiasi cha viongozi wakubwa kuwa karibu zaidi na raia
wao.
Tom
aliyasema hayo juzi alipozungumza gazeti hili katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati wa mechi
iliyowakutanisha wabunge mashabiki wa Simba na Yanga iliyochezwa uwanja wa
Taifa, jijini Dar es Salaam.
Mechi
hiyo ambayo iliisha kwa Simba kushinda kwa penalti 3-2, ilikuwa
ni
maalumu kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya wasichana nchini chini ya
uratibu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).
Alisema,
amefurahia hali ya umoja na amani iliyopo nchini tofauti na nchini nyingine ambapo
si rahisi kuona raia wakiwa karibu na viongozi wakubwa kwa kiwango alichojionea
Tanzania.
“Nimefurahi sana kuona umoja na amani ya
kiwango hiki katika nchi hii, naamini hata kazi yangu ya kufundisha soka itafanyika
vizuri kutokana na mshikamano mkubwa uliopo kuanzia kwa wakubwa wa nchi,” alisema.
Kuhusu
kiwango cha wabunge, Tom alisema Tanzania ni nchi iliyo na
vipaji
vingi vya soka, kwani kwa mazingira halisi ya wabunge na umri, hakutarajia kama
wangecheza kwa kiwango alichokishuhudia.
Alisema
kwa kiwango chao, kama wangekuwa na mazoezi ya mara
kwa
mara kama ilivyo kwa wachezaji ambao soka ni kazi, wangetisha zaidi huku
akisifu uwepo wa mechi za aina hiyo.
Wabunge
Simba
sasa
nyodo tupu
NYODO,
Vijembe na Majigambo, jana vilitawala bungeni wakati Naibu Spika wa Bunge, Job
Ndugai, alipowaambia wabunge wenye mapenzi na Yanga, wavumilie vichapo kutoka
kwa watani zao Simba.
Ngudai
alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumzia kipigo cha mabao 3-2 walichopata
wabunge ambao wapenzi wa timu ya soka ya Yanga kutoka wenzao wa Simba.
“Tulichowafanyia
Jumamosi pale uwanja wa Taifa, ni
mwendelezo wa utaratibu wa kawaida wa kutoa dozi kwa mwaka 2012,
vumilieni,” alisema.
Kiongozi
huyo ambaye ni kati ya mashabiki wa Simba, alisema amepata vikaratasi kutoka
kwa Mbunge wa Donge (CCM), Sadifa Juma Khamis, kuwa mechi hiyo iliyochezwa
irudiwe.
“Wametaka mechi ile irudiwe na kwamba
wachezaji wa Simba walikuwa wamechoka, hivyo walikuwa wakijiangusha hovyo na
kumrubuni refa,” alisema.
Alisema
wamemtaka atoe uamuzi (rufaa) juu kipigo walichokipata ambacho kimewafanya
wasuesue kufika bungeni kutimiza wajibu wa kuwawakilisha wananchi.
Ndugai
aliwapongeza wabunge wote walioshiriki katika mechi hiyo akiwemo Mbunge wa
Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari, kwa kupangua mipira kutoka kwa
wabunge wa Yanga.
Aidha,
alimpongeza Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Amos Makala.
Naye
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Neema Hamid, alipongeza Nahodha wao Makala ‘Boban’
kwa kuonesha uwezo mkubwa katika mechi hiyo akiwachambua wapinzani wao na kutoa
pasi murua.
“Kipigo
tulichowapa kimewapa funzo, siku nyingine watajua sisi ni
wakali,
poleni sana watani zetu,” alisema
Usagaji waitesa
Twiga Stars
.Madina agoma kujiuzulu
Na Ruhazi Ruhazi
KASHFA ya vitendo vya
usagaji iliyoibuliwa hivi karibuni katika timu ya soka ya Wanawake, Twiga
Stars, inawaumiza vichwa viongozi wake.
Baada ya timu hiyo kukosa
tiketi ya fainali za Afrika, waking’olewa na Ethiopia kwa mabao 3-1, kukawa na
madai kuwa, baadhi ya nyota wamekuwa wakifanya vitendo hivyo.
Kutokana na tuhuma hizo
kuibuliwa wakati ambao timu imefanya vibaya huku wachezaji wakicheza kiwango
cha chini, madai hayo yakapata nguvu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti
wa Chama cha soka la Wanawake (TWFA), Madina Case, alisema madai hayo si ya
kweli, ni uzushi mtupu.
Akiungwa mkono na Meneja
wa timu hiyo, Furaha Francis na aliyekuwa Kocha wa timu hiyo, Charles Boniface
Mkwasa, Madina alikanusha kuwepo kwa vitendo hivyo.
Madina alisema kwa vile
jambo hilo ni
uzushi, limewaumiza wachezaji, viongozi na kuliumiza soka ya wanawake kwa
ujumla mbele ya jamii.
Alisema tuhuma hizo sio
tu zinawapaka matope wachezaji na viongozi wake, pia zinahatarisha ustawi wa
soka ya wanawake kwani wazazi watagoma kuwaruhusu watoto wao kucheza soka.
Alisema, licha ya Twiga
Stars kucheza kiwango cha chini, akiwa kiongozi mkuu wa soka la wanawake
nchini, bado haoni sababu ya kuachia ngazi.
Madina alitoa kauli hiyo
baada ya kuulizwa kwa nini asijiuzulu kutokana na timu hiyo kufanya vibaya huku
kukiwa hakuna mfumo rasmi wa mashindano.
Mkwasa alisema, awali alinukuliwa
vibaya kuhusu suala hilo
alipohojiwa na moja ya kituo cha televisheni.
“Ukifuatilia mahojiano
yangu…mimi sikusema
kuna vitendo hivyo. Tatizo nadhani lilianzia pale
jambo hilo
lilipoendelezwa na magazeti.
“Hata kujiuzulu kwangu,
hakuna uhusioano na jambo hilo ,
niliwajibika katika mazingira ya kawaida tu kutokana na matokeo mabaya,”
alisema Mkwasa.
Naye Furaha Francis
alisisitiza kuwa, hakuna vitu vya aina hiyo katika timu hiyo na kama kuna mtu
ana ushahidi wa hilo ,
ajitokeze.
“Madai juu ya vitendo vya
usagaji, vimetuchafua sana .
Tunaomba kama kuna mtu ana ushahidi wa jambo hili, atueleze kuliko kuendelea
kutuchafua,” alisema.
Mwisho
Yanga yapeleka
‘chekechea’ Zenji
Na Dina Ismail
WAKATI kiungo wa kimataifa wa Yanga, Haruna Niyonzima, akitua nchini
jana, safari ya vigogo vya soka nchini Simba na Yanga kwenda Zanzibar kwa
michuano ya Kombe la Tanzania ‘Urafiki,’ imegubikwa na utata mwingi.
Kundi la kwanza la Simba liliondoka jana asubuhi kabla ya wengine kufuatia jioni, wenzao Yanga kuamua
kupeleka kikosi cha pili.
Ingawa awali Yanga
waligoma kushiriki michuano hiyo kwa hoja ya kuhofia majeruhi kuelekea michuano
ya Kagame, juzi jioni walithibitisha ushiriki wao.
Simba chini ya Kocha wake
Milovan Cirkovic na Yanga chini ya Fred Felix Minziro, zinasaka makali ya Kombe
la Kagame litakaloanza Julai 14 hadi 28.
Ofisa habari wa Yanga,
Louis Sendeu, alisema mapema jana mchana kuwa, kikosi kingeondoka
jioni ya jana.
Hata hivyo, Sendeu alidai
pia kikosi cha Yanga kingefanya mazoezi jioni ya jana kwenye Uwanja wa Kaunda
akiwemo Niyonzima aliyetua akitokea kwao Rwanda .
Kauli hizo mbili tofauti
za Sendeu, zilionekana
kuleta utata na
alipobanwa juu ya timu ipi ingekwenda Zanzibar
na ipi ingebaki Kaunda, akaonekana kubabaika kabla ya kusema apigiwe simu
baadaye.
Kuhusu Niyonzima, Sendeu
alisema nyota huyo alichelewa kutokana na matatizo binafsi nchini kwao Rwanda .
Yanga, mabingwa watetezi
wa michuano ya Kagame wataanza kampeni Julai 14 dhidi ya Atletico ya Burundi katika kundi C, huku Simba wakianza na
URA ya Uganda .
Habari kutoka Simba, zinasema
baadhi ya wachezaji walikatwa kwenye kikosi hicho bila ya sababu ya msingi,
hivyo baada ya viongozi kuingilia kati, timu hiyo iliondoka jioni kwenda Zanzibar .
Simba ilitarajiwa kuanza
kampeni ya michuano hiyo jana jioni kwa kucheza na Mafunzo ya huko.
Hata hivyo hakuna kiongozi
yoyote wa Simba aliyepatikana kuzungumzia suala hilo hadi tunakwenda mitamboni.
Mwisho
Mchina
kuwanoa makocha wa wavu Dar
Na
Clezencia Tryphone, Kibaha
MKUFUNZI
Chuanlun Liu kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Wavu (FIVB),
anatarajiwa kuendesha kozi ya mchezo huo kwa makocha wa Tanzania Bara na
Visiwani itakayofanyika kuanzia Juni 30 hadi Julai 8 mwaka huu ukumbi wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam ,
(UDSM).
Akizungumza
na Tanzania Daima mjini hapa jana, Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania
(TAVA), Agustino Agapa alisema, kozi hiyo inatarajiwa kushirikisha walimu 35
kutoka bara na visiwani, ikiwa na lengo la kuwajenga zaidi na kuwapa upeo
katika kuujua zaidi mchezo huo.
Aidha,
Agapa alisema, kozi hiyo ya kimataifa ambayo imeandaliwa na TAVA wakishirikiana
na FIVB, itawashirikisha walimu hao kutoka shule za msingi na sekondari.
“Kozi
hii ni muhimu kwetu na nina imani kubwa itawafanya walimu, kuzidi kupata mbinu
na kuujua vema mchezo huu
ili uzidi kukua na kutamba katika nchi yetu,” alisema Agapa.
Aliongeza
kuwa, hadi sasa washiriki 20 wamethibitisha kushiriki semina hiyo na kuwa, siku
ya mwisho kuthibitisha ushiriki huo ni leo.
Baiskeli
Taifa sasa Septemba
Na
Elizabeth John
CHAMA
cha Baiskeli Tanzania (CHABATA), kimebainisha kuwa mashindano ya taifa yaliyokuwa
yafanyike Juni 23 na 24 mwaka huu sasa yanatarajiwa kufanyika Septemba mwaka
huu.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa CHABATA, Nazir Manji, mabadiliko hayo ni kutokana na
ukosefu wa fedha, ambapo juhudi zinaendelea kuwaomba wafadhili wawasaidie.
Manji,
alizitaka timu za mikoa ziendelee kufanya mazoezi hadi watakapoarifiwa upya
tarehe ya mashindano na sehemu yatakakofanyika.
Kuhusiana
na uchaguzi mkuu, alisema wamepeleka maombi Baraza la Michezo la Taifa (BMT),
kuomba maelezo ya taratibu za uchaguzi na watatoa taarifa baada ya kupata
ushauri kutoka huko.
Mwisho
Yondani atua Yanga, Okwi awatesa Simba
Na Mwandishi Wetu
WAKATI klabu ya Yanga ikitangaza rasmi kumsajili
beki Kelvin Yondan kutoka Msimbazi, mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel
Okwi, anaupa wakati mgumu uongozi wa klabu ya Simba kumbakisha kwa msimu ujao.
Kwa upande wa Okwi, klabu yake imekuwa ikijitahidi
kumwekea wigo kwa kupitia dau kubwa kutokana na nyota huyo aliyepo kwenye
kiwango bora, kumezewa mate na klabu nyingi.
Okwi aliyeifungia Uganda bao la kusawazisha dakika
ya 87 katika mechi ya Jumamosi dhidi Angola, ameifanya Simba kumweka sokoni kwa
dau tofauti ndani ya wiki moja.
Mei 30, Simba kupitia kwa Ofisa Habari wake,
Ezekiel Kamwaga, Ilisema klabu itakayomhitaji Okwi, iwe tayari kutoa kitita cha
sh bil 2; kumpatia mshahara mnono, pia isiwe klabu yenye mgogoro.
Mbali ya dau jipya lililotajwa jana na Mwenyekiti
wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, alisema watachukua hatua dhidi ya
atakayemshawishi nyota huyo kwani ni mali yao.
Rage amesema Okwi na Yondan, wote ni mali ya klabu
hiyo, wanaowataka wasubiri Juni 15, pale watakapotangaza wa kuwasajili, hivyo kuruhusu
mazungumzo dhidi ya nyota wao.
Kuhusu thamani ya Okwi aliyezaliwa Desemba 25, 1992,
Rage alisema, klabu inayomhitaji, iwe tayari kutoa Euro 500,000 sawa na sh mil 950
za Tanzania.
“Thamani ya Okwi ni Euro 500,000, na kila mmoja
anajua anachokifanya dimbani, hadi sasa kuna mawakala watatu kutoka Uingereza,
Serbia na Austria, wanamuhitaji kwa majaribio, tunajiandaa kuzungumza nao kujua
tutafikia wapi,” alisema Rage.
Alisema, wakati mawakala wa Serbia na Uingereza wakionesha
nia ya kumhitaji kwa majaribio, wakala kutoka Austria anamhitaji haraka zaidi
kwa lengo la kuwahi usajili wa kiangazi hiki.
Rage alisema, pia kuna vijana watatu wa chini ya
umri wa miaka 20 wanaotakiwa kwa majaribio nchini Ujerumani, akisema
watalitolea ufafanuzi zaidi jambo hilo wakati ukifika.
Aidha, Yondan huenda akaingia katika jela ya soka
baada ya kusainiwa na Yanga licha ya kusaini mkataba mpya na timu yake ya
Simba.
Hatua hiyo inatokana na Yanga kupitia kwa Ofisa
Habari wake, Louis Sendeu, jana kusema kuwa wamemsainisha nyota huyo kwa mwaka
mmoja kwa thamani ya sh mil 30.
Nje ya dau hilo, Yondan atakuwa akilipwa mshahara
wa shilingi 800,000 kwa mwezi na stahili nyinginezo.
Sendeu alisema wameamua kumsajili Yondan kwa
mkataba utakaodumu hadi Machi 20, 2013 kutokana na ukweli kuwa, mkataba wa
nyota huyo Simba umekoma tangu Mei.
Aliongeza, wamefuata taratibu zote zinazostahili
kwa mujibu wa kanuni na sheria za Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA),
ikiwemo kufanya naye mazungumzo kabla ya miezi sita.
Sendeu alisema, hawatayumba katika hilo, na hasa
vitisho kutoka kwa viongozi wa Simba dhidi ya wachezaji wao wenye nia ya
kujiunga na klabu nyingine.
Wakati Yanga wakisema hilo, Mwenyekiti wa Simba, Rage,
jana alisisitiza kuwa Yondan ni mchezaji wao halali kwa mujibu wa kanuni na
atakayemsajili, atakuwa anavunja kanuni na sheria za Fifa.
Yondan anazirejesha Yanga na Simba kwenye zama za
kugombea wachezaji baada kujisajili na klabu mbili kama ilivyowahi kutokea kwa
Victor Costa, Athumani Idd ‘Chuji’, Kenneth Assamoh, Amri Said, Mohammed
Mwameja na Keneth Mkapa.
Kuiona Gambia ‘buku’ tatu Taifa
Na Dina Ismail
KIMA cha chini cha kushuhudia mechi ya kimataifa ya
kusaka tiketi ya Kombe la Dunia mwaka 2014 kati ya timu ya soka ya Tanzania,
Kili Taifa Stars na Gambia, itakayopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa,
jijini Dar es Salaam, ni sh 3,000.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), kima hicho ni kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, huku kwa
mashabiki wa viti vya VIP watalipa sh 30,000.
Wambura alisema, kiingilio kwa mashabiki watakaokaa
viti vya rangi ya chungwa ni sh 5,000; VIP C sh 10,000; VIP B sh 20,000 na
kuongeza kuwa, mechi hiyo itaanza saa 10.00 jioni.
Alisema tiketi hizo zitaanza kuuzwa keshokutwa
kuanzia saa 2 asubuhi kwenye vituo mbalimbali, ikiwemo Mgahawa wa Steers ulioko
Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Soko Kuu la Kariakoo
na Uwanja wa Taifa.
Aidha, siku ya mechi pia mauzo yatafanyika katika
vituo hivyo na baadaye kuhamia Uwanja wa Taifa.
Kuhusiana na ujio wa Gambia, Wambura alisema kamati
ya maridhiano inayoendesha Chama cha Soka Gambia (GFA) hadi leo mchana ilikuwa haijatuma
taarifa rasmi kwao, ingawa kuna habari utakuwa msafara wa wachezaji 23 na viongozi
tisa.
Kwa mujibu wa Wambura, kupitia vyombo vya habari
vya nchi hiyo, Ofisa Habari wa GFA, Bakary Balder, alisema msafara wa timu hiyo
utakuwa chini ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana na Michezo, Malang
Jassey.
Viongozi wengine ni Ofisa Utawala wa timu, Modou
Sowe; Kocha Luciano Machini, makocha wasaidizi, Peter Bonu Johnson na Lamin
Sambou; kocha wa makipa, Alhagie Marong; mtaalamu wa tiba mbadala
(physiotherapist), Pa Matarr Ndow; mtunza vifaa, Sanna Bojang na daktari wa
timu, Kalifa Manneh.
Wachezaji ni Musa Camara, Abdou Jammeh, Momodou
Futty Danso, Lamin Basmen Samateh, Ousman Koli, Pa Saikou Kujabi, Mustapha
Kebba Jarju, Yankuba Mal Ceesay, Demba Savage, Saihou Gassama, Alieu Darboe,
Momodou Ceesay, Pa Modou Jagne, Tijan Jaiteh na Bubacarr Sanyang.
Wengine ni Christopher Allen, Musa Yaffa, Sulayman
Marr, Mamut Saine, Hamsa Barry, Ali Sowe, Omar Colley na Saloum Faal.
Stars itakutana na Gambia iliyotoka kuvuna sare ya
bao 1-1 na Morocco, ikiwa ni wiki moja tangu icheze na Ivory Coast, mjini
Abidjan na kufungwa mabao 2-0, yakifungwa na Didier Drogba na Solomon Kalou.
Mwisho.
MKUU wa wilaya ya Handeni Muhingo Rweyemamu pamoja na mwanachama wa klabu ya Yanga Abdallah Binkleb jana wamechukua fomu ya kuwania nafasi ya ujumbe katika uchaguzi wa klabu ya Yanga uliopangwa kufanyika Julai 15.
Katibu wa kamati ya uchaguzi
ya Yanga Francis Kaswahili alisema jana
kwamba wanachama hao wanafanya idadi ya wagombea waliochukua fomu za kuwania
nafsi mbalimbali za uongozi katika klabu hiyo kufikia 10 .
Alisema zoezi hilo ambalo
lilianza jumamosi iliyopita limekuwa la kusuasua tofauti na ilivyotarajiwa
hivyo amewaomba wanachama wa klabu hiyo wenye sifa kujitokeza kabla ya kufungwa
Juni 6.
Mbali na hao wanachama
wengine waliochukua fomu ni pamoja na John Jambele anayewania uenyekiti, huku
Ayoub Nyenzi akiwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti.
“Waliochukua fomu kuwania
ujumbe wa kamati ya Utendaji mbali na Muhingo na Binkleb ni Isack Chandi, Jumanne Mwamwenye na Salehe
Hassan,”alisema.
Uchaguzi huo unafuatia
kujiuzulu kwa aliyekuwa Mwenyekiti Lloyd Nchunga baada ya kushinikizwa na baadhi ya wanachama
wakiongozwa na baraza la wazee wa klabu hiyo kutokana na kushindwa kuiletea
mafanikio klabu hiyo chini ya uongozi wake.
Pia nafasi ya Makamu
mwenyekiti iliyokuwa inashikiliwa na Davis Mosha ambaye alijitoa miezi michache
baada ya kuchaguliwa kutokana na kutoelewana na Nchunga, huku mjumbe Theonest
Rutashoborwa akitangulia mbele ya haki.
Uchaguzi huo pia utajaza
nafasi nne za Wajumbe walioachia ngazi
ambao ni pamoja na Mzee Yusuf, Charles Mgondo na Ally Mayay.Mpaka sasa Yanga imebaki na wajumbe wanne, Mohammed
Bhinda, Sarah Ramadhan, Tito Osoro na Salum Rupia.
Baada ya kufanyika kwa uchaguzi
kamati ya utendaji itateua wajumbe wengine watatu kwa mujibu wa katiba, hiyo
inatokana na wajumbe hao wa kuteuliwa Seif Ahmed, Mbaraka Igangula na Pascal
Kihanga kujiuzulu.
mwisho
.
Dawa zamchelewesa Sajuki kurudi
Na
Nasra Abdallah
BAADA ya kufanikiwa kufanyiwa upasuaji wa uvimbe
uliokuwa ukimsumbua mwigizaji na muongozaji wa filamu nchini, Juma Kilowoko
’Sajuki’, imeelezwa kwamba dawa anazozitumia kwa sasa ndizo zinazomchelewesha kurejea
nchini.
Rafiki wa karibu wa msanii huyo, Dennis Sweya
’Dino’, alisema dawa ambazo Sajuki anazitumia kwa sasa zina nguvu sana kiasi
cha kwamba anatakiwa kuwa chini ya uangalizi maalumu wa wauguzi.
Dino alisema kwamba kadiri siku zinavyopita
ndivyo Sajuki anavyoendelea vizuri na akawaomba Watanzania kuendelea kumuombea
ili arudi nyumbani salama.
“Tunashukuru ndugu yetu Sajuki ameshafanyiwa
upasuaji na anaendelea vizuri sana
kwa kweli hivi sasa hawezi kurudi kwa kuwa anatumia dawa ambazo ni lazima asimamiwe
na wauguzi lakini hali yake inaimarika kila kukicha,” alisema Dino.
Alisema kuwa juzi mchana aliweza kuongea na
Sajuki mwenyewe kwa simu na sauti yake ilikuwa yenye kuleta faraja ikiwa
imeimarika sana
kulinganisha na wakati alipoondoka.
Sajuki alikuwa katika hali ngumu ya kuumwa
kutokana na uvimbe kwenye ini ambao ulimsababisha kupungua uzito na kutokana na
kutokuwa na fedha za kugharamia matibabu nchini India ilibidi aombe msaada kutoka
kwa wasamaria wema ambao walifanikisha.
Mwisho
Twanga kuzindua ‘amshaamsha’ Club
Bilicanas
Na Khadija Kalili
BENDI ya Twanga Pepeta International ‘Kisima cha Burudani’ imetangaza kuanzisha
kampeni ya kujitangaza itakayokwenda kwa jina la ‘Amsha amsha ya Twanga’
itakayozinduliwa ukumbi wa Club Bilicanas jijini Dar es Salaam kesho.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana, Asha Baraka, alisema, onesho hilo litaanza majira ya saa 3:00 usiku ambapo
kiingilio kitakuwa ni sh 8,000 kwa kila mtu.
Asha alisema, wameamua
kuanzisha kampeni hiyo, ambapo watakuwa wakipiga kwa mtindo wa ‘Non Stop’ hadi
kunakucha.
Pia mkurugenzi huyo,
alimtangaza msemaji mpya wa bendi, ambaye ni Muddy Pizaro, huku Hamisi Kayumbu
‘Amigolas’ akikamata mikoba ya meneja.
Aliongeza kuwa, bendi yake
bado iko imara kama chuma na wanajivunia kuwa,
wao ni sawa na shamba au mti wenye matunda, hivyo ni jambo la kawaida kwao
kupopolewa.
“Sisi tulianzisha Twanga
Academia, leo matunda yake yanaonekana tuna wanamuziki wengi, hivyo hatuwezi
kutetereka katika muziki, kwa sababu jadi yetu hapa ni bandika bandua labda
waninunue na mimi mwenyewe,” alisema.
Hivi sasa Twanga inatamba na
wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Shamba la Twanga’ uliotungwa na Rapa
Greyson Semsekwa na kutiwa nakshi na waimbaji wa bendi hiyo kwa ujumla.
Twiga Stars walia fitna Ethiopia
Na Clezencia Tryphone
BAADA ya kukubali kichapo cha
mabao 2-1 kutoka kwa Ethiopia, timu ya taifa ya soka ya wanawake Tanzania
‘Twiga Stars’ imerejea jijini Dar es Salaam jana huku ikilia fitna ndiyo
imewafanya wapoteze mchezo huo.
Akizungumza jijini Dar es
Salaam jana mara baada ya kurejea, Kocha Mkuu wa Twiga Stars, Charles Boniface
Mkwasa, alisema kufungwa kwao kumetokana na fitna iliyosababisha mchezo kuwa
mgumu.
Mkwasa alisema wachezaji wake
walionekana kuondoka mchezoni baada ya kufanyiwa fitna nyingi ambazo hakutaka
kuziweka wazi.
Alisema licha ya kufungwa lakini wanajivunia bao la ugenini na kwamba sasa kazi ni moja kujipanga ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi wa zaidi ya mabao 2 ili waweze kusonga mbele.
Aliwataka wachezaji wake, kujituma na kuongeza bidii katika mazoezi, ili kuepuka kufungwa kwenye uwanja wa nyumbani, Juni 16.
Mshindi katika mechi hiyo atafuzu kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (AWC), zitakazochezwa Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.
Alisema licha ya kufungwa lakini wanajivunia bao la ugenini na kwamba sasa kazi ni moja kujipanga ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi wa zaidi ya mabao 2 ili waweze kusonga mbele.
Aliwataka wachezaji wake, kujituma na kuongeza bidii katika mazoezi, ili kuepuka kufungwa kwenye uwanja wa nyumbani, Juni 16.
Mshindi katika mechi hiyo atafuzu kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (AWC), zitakazochezwa Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.
Mwisho
Makalla ajitoa Simba
Na Clezencia Tryphone
NAIBU Waziri wa Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo, Amos Makalla amejitoa katika Kamati ya Fedha ya klabu ya
Simba na kuanzia sasa atakuwa akizisaidia timu zote hapa nchini.
Makalla alibainisha hayo juzi,
katika sherehe za klabu hiyo kujipongeza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara
zilizofanyika ukumbi wa Dar Live Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Makalla, alisema, sababu
ya kujitoa ni kutokana na wadhifu mkubwa alionao kwa sasa.
“Mimi nilikuwa ni mmoja wa
viongozi waliokuwa katika Kamati ya Simba na kuchangia mafanikio haya ambayo
Simba imeyapata, lakini kwa sasa kwa kuwa ni waziri, jukumu langu ni kusaidia
timu zote nchini bila ya kujali Simba wala timu yoyote,” alisema Makalla.
Aliuasa uongozi wa Wekundu hao
wa Msimbazi, kutoridhika na mafanikio hayo na kuwaomba kuzidi kupigana kufa na
kupona ili kuendeleza hali ya mafanikio ndani ya klabu hiyo na kujipanga ili
kufanya vizuri zaidi.
Alisema ana imani kubwa klabu ya Simba ina uwezo mkubwa wa kujenga uwanja mzuri wa kisasa kutokana na ukongwe ambao inayo.
Alisema ana imani kubwa klabu ya Simba ina uwezo mkubwa wa kujenga uwanja mzuri wa kisasa kutokana na ukongwe ambao inayo.
Katika sherehe hizo, Makalla
akimkabidhi nahodha wa Simba, Juma Kaseja, tuzo na medali maalumu kwa ajili ya
aliyekuwa mchezaji wa timu hiyo, marehemu Patrick Mafisango aliyefariki hivi karibuni
kwa ajali ya gari, ambapo nahodha huyo alishindwa kujizuia na kuangua kilio na
kuwafanya baadhi ya wachezaji wenzake, mashabiki na wapenzi kuanza kumwaga
machozi.
Kabla ya kutolewa kwa tuzo hiyo,
ulipigwa muziki wa ‘Kazi yake Mola Haina Makosa’ wa Msanii Madee kumkumbuka
Mafisango na mara baada ya wimbo huo kumalizika, shughuli zote ukumbini hapo
zilisimama kwa dakika moja na watu wote walisimama na kumwombea mchezaji huyo.
Naye Meneja wa Global
Publishers Limited, Abdallah Mrisho, alikabidhi sh milioni 3 kwa Kaseja, kama
zawadi yao kwa wachezaji na benchi la ufundi ikiwa ni pongezi kwa kazi nzuri
waliyoifanya katika msimu uliopita wa 2011/12 hadi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu.
Sherehe hizo zilipambwa na wanamuziki na bendi mbalimbali hapa nchini, ikiwemo Msondo, Mshauzi Classic, Young D.
Sherehe hizo zilipambwa na wanamuziki na bendi mbalimbali hapa nchini, ikiwemo Msondo, Mshauzi Classic, Young D.
Sekretarieti Yanga yapewa rungu
Na Clezencia Tryphone
KAMATI ya Sheria,
Maadili na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imebainisha kuwa,
uteuzi uliofanywa na Kamati ya Utendaji ya Yanga Mei 21 kujaza nafasi zilizo
wazi ni batili hivyo kuagiza klabu hiyo iongozwe na sekretarieti.
Kamati hiyo
iliyokutana juzi chini ya Mwenyekiti wale Alex Mgongolwa, imebatisha uamuzi huo
kwa vile
Kamati hiyo iliyofanya
uteuzi huo haikuwa na akidi iliyojitosheleza.
Mgongolwa alisema
jijini Dar es Salaam jana kwamba, ili kamati hiyo ya utendaji ya Yanga yenye
wajumbe 13, inatakiwa kuwa wajumbe asilimia 50 ya wote, hivyo ili wafanye
uamuzi halali, hawatakiwi kupungua saba.
Alisema, kutokana
na wajumbe kadhaa wa klabu ya Yanga kujiuzulu na kubaki wanne, ambao ni Sarah
Ramadhan, Mohamed Bhinda, Tito Osoro na Salim Rupia, kwa sasa hawawezi kufanya
shughuli zozote za klabu hiyo, hadi nafasi zilizo wazi zitakapojazwa.
Aliongeza kuwa, kutokana
na wajumbe kutotimia, kazi zote za klabu hiyo kama
inavyoelekeza Katiba ya Yanga, shughuli za kila siku zitaendelea kufanywa na
Sekretarieti ya Yanga chini ya Katibu Mkuu, Selestine Mwesigwa.
Aidha, Mgongolwa
alisema, baada ya kupata taarifa rasmi kutoka Yanga, wamebaini kuwa, Kamati ya
Utendaji ya Yanga imekosa akidi baada ya wajumbe wake wengi kujiuzulu, hivyo
kutokuwa na uwezo wa kufanya uamuzi kwa mujibu wa Ibara ya 32(1) ya Katiba ya
klabu hiyo.
Alisema, wametoa
mwongozo kwa Kamati ya Uchaguzi ya TFF, ambayo ndiyo msimamizi wa Kamati ya
Uchaguzi ya Yanga kuwa, ili Kamati ya Utendaji ya Yanga iwe na nguvu za
kikatiba kufanya shughuli zake ikiwemo uamuzi wa masuala mbalimbali ndani ya klabu
hiyo ni lazima iwe na akidi.
Aliongeza kuwa, kwa
mujibu wa Ibara ya 29(3) ya Katiba ya Yanga, nafasi zilizo wazi katika Kamati
ya Utendaji zinatakiwa kujazwa katika Mkutano Mkuu wa kawaida ujao.
Mwisho.
Kim alia na washambuliaji Kili Taifa Stars
Na Clezencia Tryphone
KOCHA mkuu wa timu ya Taifa ya Soka Tanzania , ‘Kilimanjaro Taifa Stars’
Mdenish Kim Poulsen, amesema licha ya kuwa ni mara yake ya kwanza kukinoa
kikosi hicho ugonjwa unaokisumbua ni umaliziaji.
Akizungumza mara baada ya pambano la kirafiki kati ya Stars na Malawi
‘The Flames’ juzi Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam lililomalizika kwa sare
ya bila kufungana, Poulsen alisema, umaliziaji ndio tatizo linalowakabili
vijana wake.
Poulsen alisema, endapo tatizo hilo
litakwisha, ana imani kikosi chake kitafanya vema licha ya kuwa ni mara ya
kwanza kukabidhiwa mzigo mkubwa kama huo na kuwa, kwa sasa analifanyia kazi tatizo
hilo kubwa
juzi.
“Nimetazama na nilikuwa makini sana ,
lakini tatizo ni umaliziaji, ukiangalia utafutaji kwa maana ya kiungo
walijitahidi kufanya kazi yao
kwa umakini zaidi, tatizo ilikuwa katika kumalizia na hasa hapo wapinzani wetu
ndipo walipokuwa wakichukulia mpira,” alisema Poulsen.
Aidha Poulsen aliwapongeza vijana wake kwa jinsi ambavyo walijituma
na kusema kuwa mapungufu ni sehemu ya mchezo na ndo sababu ya kuwa na mchezo wa
kujipima nguvu kabla ya kuvaa na Ivory Coast kwenye
mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia itakayofanyika ugenini Juni 2 mwaka huu.
Naye Kocha wa The Flames, Kinnah
Phiri, amelipongeza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kwa kuona umuhimu na
kuwaomba kuja hapa nchini kucheza mchezo huo wa kirafiki na kuwa ni kipimo
kizuri kwa timu yake.
Aliongeza kwa kuwapongeza
wachezaji wa Stars, kwa uwezo wao na kusema kuwa, hata kama
kuna upungufu ni kidogo, kwa kuwa ni moja ya makosa katika soka kwani hata timu
yake ina upungufu iliyouonesha.
Katika hatua
nyingine, pambano hilo
kati ya Stars na The Flames, limeingiza sh 40,980,000, kutokana na mashabiki 10,767
waliokata tiketi kushuhudia
Mwisho
TFF yambeba Nchunga
.Yagoma
kutambua mapinduzi Jangwani
.Mwakalebela ashangazwa na ukimya wake
Na Dina Ismail
SIKU
moja baada ya wanachama zaidi ya 700 wa klabu ya Yanga kutangaza kuupindua
uongozi
wa klabu hiyo chini ya Lloyd Nchunga kwa hoja ya kushindwa kazi, Shirikisho la
Soka
Tanzania (TFF), limesema halitambui uamuzi huo.
Juzi
wanachama walikutana kwenye Uwanja wa Kaunda, kujadili mustakabali wa klabu yao na kuamua kuung’oa uongozi wa Nchunga huku
wakipanga kwenda kwa Msajili wa Vyama na
Klabu za Michezo wilaya ya Ilala, kumwomba awaitishie uchaguzi mkuu.
Kwa
mujibu wa hoja zilizoibuliwa kwenye mkutano huo na baraza la wazee wa klabu
hiyo chini ya katibu wake Ibrahim
Akilimali na vijana wakiongozwa na Bakili Makele, wamefikia hatua hiyo kutokana na kutoridhishwa na
utendaji wa uongozi wa Nchunga.
Mbali ya
wanachama hao kupanga kuwasilisha majina na sahihi za waliohudhuria mkutano huo wa juzi kwa Msajili, pia waliteua kamati ya
usajili wa wachezaji kwa msimu ujao.
Akizungumzia
maamuzi hayo ya wanachama, Katibu Mkuu wa TFF, Angetille Osiah, amezitaka pande
husika kukutana haraka kupata ufumbuzi wa kile kinachobishaniwa kwa lengo la
kujiweka sawa kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Kagame.
Yanga
ambao ni mabingwa wa kombe hilo ,
wamezama kwenye malumbano huku michuano hiyo
ikitarajiwa kutimua vumbi mwezi ujao.
Angetile
alisema shirikisho hilo
linasimamia katiba kwa wanachama wake wote, hivyo taratibu zozote zinazofanywa
na wanachama wake bila kufuata katiba hawazitambui; hivyo wataendelea kuutambua uongozi wa Nchunga. Alisema
maadam uongozi wa Nchunga umepanga mkutano mkuu Julai 15, wanachama walipaswa
kuwa na subira, badala ya kuitisha mwingine nje ya matakwa ya katiba hiyo.
“Busara
zinatakiwa katika mgogoro huo kupata nafasi ya kuiandaa timu yao kuelekea michuano ya Kombe la Kagame, kuna mambo mengi yanapaswa
kufanywa katika kipindi hiki ikiwemo suala
la usajili,” alisema.
Hata
hivyo, baadhi ya wadau wameielezea hatua ya shirikisho hilo kama ni kukawia
kuchukua hatua dhidi ya mvutano wa muda mrefu ndani ya klabu hiyo ukihusisha
wanachama na uongozi kutokana na hoja kadha wa kadha, kubwa ni ukata wa fedha uliokithiri.
Katibu mkuu
wa zamani wa TFF, Frederick Mwakalebela, alisema TFF kupitia kurugenzi yake ya utawala na wanachama, ilipaswa kuchukua
hatua muda mrefu dhidi ya sintofahamu inayoendelea
katika klabu hiyo tangu walipopokwa ushindi wa Coastal Union .
Alisema
miaka ya nyuma, walikuwa wakisimamia machafuko ya aina hiyo kwa baadhi ya maeneo, hali ambayo ilisaidia kupunguza
migogoro iliyokuwa kama utamaduini kwa baadhi ya klabu.
DC Mvomero bosi mpya RT
Na
Mwandishi Wetu, Morogoro
WAJUMBE
wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), wamempa kura za kishindo
Antony Mtaka kuwa Rais wa Shirikisho hilo akimbwaga Kanali mstaafu, Juma Ikangaa.
Katika
nafasi hiyo, Mtaka ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mvomelo, Morogoro, alishinda kwa
kura 50 dhidi ya 29 za Ikangaa, Katibu
Mkuu wa zamani wa shirikisho hilo wakati huo ikijulikama kama TAAA. Mtaka
alipata kura hizo katika kura za marudio baada ya raundi ya kwanza kukosekana
mshindi
wa moja kwa moja miongoni mwa wagombea wanne waliokuwa wamejitosa katika nafasi hiyo kwa Ikangaa kupata kura 25
na Mtaka kura 36.
Waliochemkia
raundi ya kwanza ni Francis John aliyeambulia kura 15 na Henry Nyiti aliyepata
kura 7,
hivyo
raundi ya pili kushudia ushindani mkali kati ya Ikangaa na Mtaka.
Akitangaza
matokeo ya uchaguzi huo majira ya saa 3:30 usiku, Mwenyekiti wa Kamati ya
Uchaguzi huo, Henry Tandau, alisema
kurudiwa kwa nafasi ya Rais na Katibu Mkuu, ilitokana na wagombea
kushindwa kufikia asilimia iliyohitajika kwa mujibu wa kanuni.
Ushindani
mwingine ulikuwa kwenye nafasi ya Katibu Mkuu iliyokuwa ikishindaniwa na watu
wanne, akiwemo Suleiman Nyambui aliyekuwa akitetea, John Bayo, Zainab Mbiro na
John Manyama, lakini Nyambui alishinda kwa kura 41 dhidi ya 38 za Bayo, katika
raundi ya pili.
Wagombea
wawili katika nafasi tofauti, Makamu wa Kwanza
wa Rais (Utawala) ilikwenda kwa William Kallaghe, aliyekuwa mgombea pekee kwa
kura 78.
Katika
nafasi ya Makamu wa Pili wa Rais (Ufundi), iliyokuwa ikiwaniwa na wagombea
wawili, Dk. Hamad Ndee alishinda kwa kura 55, akimbwaga Herman Ndisa aliyepata
kura 42. Nafasi nyingine iliyokuwa na ushindani ni Katibu Mkuu Msaidizi ,
iliyokuwa ikiwaniwa na watu wanne, lakini Ombeni Zavalla akishinda kwa kura 40,
Julius Murunya (32), Lucas Nkungu na Leonard Mandara, kila mmoja akipata tatu. Nafasi
ya Mweka Hazina ilikuwa na mgombea mmoja, Is- Haq Seleman, aliyepata ushindi wa
kimbunga wa kura 78 kati ya 79.
Mbali ya
nafasi ya Rais na Katibu Mkuu, kivumbi kingine kilikuwa kwenye nafasi 10 za
ujumbe wa shirikisho hilo ,
zilizokuwa zikiwaniwa na wanachama zaidi ya 30. Hata hivyo, mhariri wa michezo
wa gazeti la Tanzania Daima, Tullo Chambo, alifunga pazia la nafasi zilizokuwa
zikiwania baada ya kupata kura 37, akiungana na Mwinga Mwanjala ( 53), Lwiza
John (50), Peter Mwita ( 50)
na Zakaria Gwandu ( 47). Wajumbe wengine ni Meta Petro
Bare ( 46), Zakaria Barie (45), Rehama Killo ( 42), Robert Kalyahe ( 41) na Christian Matembo (38).
Jezi ya Mafisango
kutovaliwa
Simba
.Maelfu
waaga mwili wake Dar
.Rage
ashindwa kumaliza risala
Na
Clezencia Tryphone
JEZI
namba 30 iliyokua ikivaliwa na nyota wa kimataifa wa Rwanda ,
Patrick Mutesa Mafisango katika kikosi cha Simba, haitavaliwa tena na mchezaji wa
timu hiyo kama sehemu ya kumuenzi nyota huyo
aliyefariki usiku wa kuamkia
juzi kwa
ajali ya gari, eneo la Veta-Keko, jijini Dar
es Salaam .
Uamuzi
huo mgumu ulitangazwa jana na Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage,
wakati akitoa risala
fupi katika
tukio la kuuaga mwili wa mchezaji huyo lililofanyika jana kwenye viwanja vya
Sigara, Chang’ombe
jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mamia
ya watu.
Zoezi hilo la kuaga mwili wa
marehemu lililoanza majira ya saa 5 asubuhi, lilitarwajiwa kufungwa saa 9
alasiri kwa lengo la kutoa nafasi kwa watu wa kada mbalimbali kuuaga mwili wa
nyota huyo kabla ya mwili wake kusafirishwa
leo
kwenda kwao DR Congo.
Hatua ya
Simba, ni kama ilivyokuwa Manchester City ambao waliamua kuienzi jezi namba 23 ya Marc
Vivien Foe, aliyekuwa amefariki dunia akiwa na timu ya taifa ya Cameroon
katika michuano ya Kombe la Mabara, mwaka 2003 kwa kutovaliwa tena.
Akizungumza
kwa simanzi kubwa, Rage alisema ni pigo kubwa kwa Simba, kwani Mafisango
alikuwa ni nguzo muhimu sio tu kwa umahiri wake dimbani, bali akiwa mshauri kwa
wachezaji wengine ndani na nje ya dimba,
hivyo ni
pengo kubwa mno.
Rage
alisema, kifo hicho kilichoacha pengo kubwa katika kikosi cha sasa,
kimewakumbusha wanachama na
wapenzi
wa klabu hiyo tukio la mwaka 1978, Simba ilipompoteza mchezaji wake Hussein
Tindwa, aliyekuwa
ameteza
maisha kwenye Uwanja wa Uhuru.
Kwa
mantiki hiyo, jezi namba 30 iliyokuwa ikivaliwa na Mafisango, haitatumika tena
kwa lengo la kuendelea kuenzi mchango wa mchezaji huyo aliyewakuwa akiichezea
Simba kwa moyo wake wote na kuwataka wenzake kuiga yote mazuri yote ya nyota
huyo.
“Ni
pengo kubwa kwa sababu, mbali ya umuhimu wake kiuchezaji, alikuwa msaada mkubwa
kutokana na umahiri wake wa kujua lugha nyingi kikiwemo Kiswahili, Kingereza na
Kifaransa, hivyo kuwa mchezaji muhimu ndani na nje ya nchi tutamkubuka sana ,” alisema.
Kutokana
na kulemewa na simanzi, Rage alishindwa kumalizia risala katika zoezi la kuaga
mwili ya nyota huyo,
hivyo
kupokewa na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ aliyeimalizia, kubwa zaidi
ikiwa ni simanzi na
pigo
kubwa katika kikosi cha timu hiyo.
Kabla ya
kutua Simba, Mafisango aliwame kukipiga katika timu za Azam FC ya Tanzania , APR ya Rwanda na TP Mazembe ya DR Congo,
akiwa na sifa zote wa kuitwa mchezaji wa kimataifa.
Zoezi hilo la utoaji huo wa heshima
za mwisho, uliambatana na ibada iliyoongozwa na Mchungaji Tito Kihame,
Dk. Fenella
Mukangara na viongozi wengine wa kada mbalimbali, wote wakiwa na simanzi kubwa
ya kumpoteza mchezaji huyo mahiri.
Akizungumza
na ufupi, Mukangara aliwataka wachezaji wa Tanzania kuifa mfano wa Mafisango
katika kujituma, akisema hiyo ndio siri kubwa ya mafanikio ya jambo lolote
katika maisha ya mwanadamu.
“Kifo
chake ni pigo kubwa kwa Simba na Tanzania kwa ujumla, tunamshukuru
kwa kuvuka mipaka
na kuja
kucheza kwetu. Wachezaji wa Simba wasikate tamaa, kitu muhimu kwao kuendeleza
yote mazuri ya
marehemu,
” alisema.
Nyota
kadhaa wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars walijitokeza kubeba jeneza la nyota
huyo wakati wa kupelekwa viwanja vya Sigara, wakiongozwa na Juma Kaseja, Jonh
Bocco, Mwinyi Kazimoto, Shabani Nditi, Amiry Maftah, Nurdin Bakari, Agrey
Moris na Juma Nyoso.
Aidha,
Ofisa habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga, alisema katika msafara wa kwenda DR
Congo, Haruna Moshi Boban ndiye atakuwa mwakilishi wa wachezaji katika mazishi
hayo huku uongozi ukiwakilishwa na Joseph
Itang’are
ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji.
Kamwaga
alisema, msafara wa kwenda DR Congo utakuwa alfajiri ya leo huku mtoto wa
marehemu, Chris Paul mwenye umri wa miaka mitano, ametanguliwa
na Haruna Niyonzima, nyota wa kimataifa wa Rwanda anayekipiga katika klabu ya
Yanga.
Mwisho.
Wazee,
Vijana Yanga SC
wabariki
masharti ya Manji
.Waitisha
mkutano mzito kesho
Na
Dina Ismail
BARAZA
la Wazee wa klabu ya Yanga chini ya Mwenyekiti wake Dk. Jabir Katundu na kundi
la Vijana, wameunga mkono masharti yaliyotolewa na mfadhili wao wa zamani,
Yusufu Manji kukubali kurejea, kama masharti yake matano, yatatimizwa.
Akizungumza
jijini Dar es Salaam
jana, Katibu wa Baraza la Wazee, Ibrahim Akilimali, alisema
mbali
ya wao kuunga mkono masharti ya Manji, pia wanausihi uongozi wa Lloyd Nchunga,
kujiweka
kando kabla ya kesho Jumapili.
Akilimali
alisema, ni heri Nchunga akatumia busara ya kawaida kujiweka kando mwenyewe
badala
ya kusubiri kuondolewa kwa nguvu ya wanachama katika mkutano wa kesho kutokana
na
kushindwa kuongoza klabu hiyo.
“Leo
(jana) tunatoa agizo la mwisho kwa Nchunga na wenzake kuachia ngazi mara moja
kwa sababu wameshindwa kuongoza, wachezaji wanalia njaa, makocha wapo hoi
kifedha, hili
halivumiliki,
Yanga inadhalilika,” alisema Akilimali akiungwa mkono na wazee wenzake.
Alisema,
wanamtaka Nchunga na wenzake wajiondoe wenyewe kabla ya mkutano wa
kesho
Jumapili ambao utafanyika makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Twiga
na
Jangwani, Kariakoo, jijini Dar es
Salaam .
Kuhusu
maandalizi ya mkutano huo, Akilimali alisema tayari baadhi ya wanachama kutoka
sehemu mbalimbali ikiwemo Zanzibar ,
wameshaanza kuwasili kwa ajili ya mkutano huo wa kuikomboa klabu hiyo katika
hali ngumu kiuchumi.
Naye
Mwenyekiti wa Vijana, Bakili Makele alisema jana, wanaunga mkono masharti yaliyotolewa na Manji kwani
yatasaidia kuleta uwazi wa mambo yahusuyo matumizi ya fedha kwa kipindi cha
kuanzia 2006 hadi 2012.
“Tunaunga
mkono masharti ya Manji kabla ya kurejea kwenye ufadhili, katika hali ya
kawaida,
mtu huwezi kutoa fedha bila kujua
zinatumikaje… tumekuwa tukilipigia kelele jambo hili kila
siku,
tukitaka mikutano ya kikatiba, lakini viongozi wetu wamekuwa wagumu,” alisema
Bakili.
Bakili
aliyeungana na wazee kutoa tamko hilo , alisema mkutano
wa wanachama wa kesho, utafanyika kama
ulivyopangwa huku akitoa wito kwa wanachama wa klabu hiyo kujitokeza
kwa
wingi kufanya maamuzi ya kuiokoa Yanga.
Alisema
kutokana na ukata ambao unaikabili klabu hiyo hadi kuwa na madeni
yanayokadiriwa kufikia mil 106, kuna hatari mali
za klabu hiyo kupigwa mnada kama si jingo la
makao makuu, kitu ambacho wasingependa kitokee.
Makele
alisema, leo wanachama wa klabu hiyo kutoka matawi mbalimbali wanatarajiwa
kukutana katika tawi la Buguruni kujadili ajenda mbalimbali ambazo
watawasilisha katika mkutano huo wa kesho.
Kauli
ya Akilimali na Bakili, imekuja siku moja tangu Manji atoe masharti ya
kurejesha ufadhili
wake
katika klabu hiyo, baada ya vijana kumsihi afanye hivyo kuokoa jahazi;
wachezaji na
makocha
wakilia ukata mkali.
Masharti
hayo ni kufanywa uhakiki wa mahesabu ya akaunti ndani ya siku 90, tena ukaguzi
huo ufanywe na kampuni binafsi kwa hesabu za kuanzia mwaka 2006 hadi 2012.
Aidha,
kuanzia sasa akaunti za Yanga zichapishwe kwenye magazeti, siku 15 baada ya
kumalizika
robo ya mwaka, pia kuwepo na upigaji wa
kura ya maoni ndani ya siku 60,
kuamua
kama wanachama wanautaka mfumo wa kampuni au
la.
Sharti
jingine, ni kuwepo marekebisho ya katiba ndani ya siku 90, juu ya muundo wake
wa
uongozi kwa kukubali mojawapo ya mfumo huu chini ya Katiba ya Yanga.
mwisho
Banyana yatua
kuivaa Twiga
Na Ruhazi Ruhazi
TIMU
ya soka ya taifa ya Afrika Kusini ‘Banyana Banyana’ ilitarajiwa kuwasili nchini
jana jioni kwa mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Twiga Stars itakayopigwa
kesho kwenye Uwanja wa Taifa,
jijini
Dar es Salaam .
Kwa
mujibu wa Ofisa Habari za Shirikisho la soka Tanznaia (TFF), Boniface Wambura,
msafara wa wageni hao, utakuwa na watu 26, wakiwemo wachezaji 18, wakifikia
kwenye hoteli ya Sapphire Court Hotel, tayari kwa mechi hiyo.
Twiga
Stars inataka kuitumia mechi hiyo kama kipimo kabla ya kucheza mechi ya kwanza
ya mchujo katika kuwania tiketi ya fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi
ya Ethiopia itakayochezwa Mei
27, jijini Addis Ababa .
Mechi
hiyo inatarajiwa kuwa ngumu zaidi kwani Banyana Banyana nayo inasaka makali ya
kuwanyoa Zambia katika
kampeni hizo, wakianzia ugenini mjini Lusaka
kabla ya kurudiana
nchini
Afrika Kusini.
Wambura
alisema, makocha wa timu zote mbili, Boniface Mkwasa wa Twiga Stars na mwenzake
Joseph Mkhonza wa Banyana Banyana, leo mchana wazungumzia maandalizi yao kuelekea mechi hiyo.
Twiga
Stars na Banyana, zipo kwenye raundi ya mwisho ya kuwania tiketi kwani kama
zitafanikiwa kuvuka hatua ijayo, zitakuwa zimejitwalia tiketi ya fainali hizo zitakazofanyika Novemba
mwaka huu, nchini Guinea
ya Ikweta.
mwisho
TANZIA
Patrick Mafisango, ambaye ni mchezaji mahiri wa Simba,
amefariki dunia leo asubuhi kwa ajali ya gari katika eneo la Tazara. Juzi
alikuwa mmoja wa wachezaji waliokosa penalti pambano huko Sudan , lakini pia alikua ameitwa tena timu ya
Taifa ya Rwanda baada ya kuonesha kiwango cha juu katika Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara iliyomalizika.
RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA, NA MWANGA WA MILELE AANGAZIWE, APUMZIKE KWA AMANI- AMANI
Mafisango afariki Dunia
Na Clezencia Tryphone
KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Rwanda, anayekipiga katika klabu ya
Simba, Patrick Mutesa Mafisango, amefariki dunia baada ya kupata ajali ya gari
alfajiri
ya jana, jijini Dar es Salaam.
Mafisango, kati ya nyota mahiri walioitwa kwenye kikosi cha timu
ya taifa ya Rwanda, ‘Amavubi’ chini ya Kocha Mserbia, Sredejovic Milutin
‘Micho,’
amefariki kwa ajali aliyopata eneo la Veta- Chang’ombe, wilayani
Temeke.
Kwa mujibu wa Olilemba Mafisango ambaye ni mdogo wa marehemu, ajali
hiyo ilitokea majira ya saa 9, baada ya gari waliyokuwa wamepanda, kupinduka
katika harakati za kumkwepa mwendesha pikipiki.
“Katika harakati za kumkwepa mwendesha pikipiki kwa lengo la
kuokoa maisha yake, ndipo gari ikapinduka nay eye kuumia vibaya,” alisema
Olilemba na kusema wakati gari hiyo ikipata ajali, ilikuwa na watu watano ndani
yake.
Alisema, kati yao wavulana
walikuwa watatu na wasichana wawili, wakati
huo wakirejea nyumbani kutokea Maisha Klabu iliyopo Masaki, jijini Dar es
Salaam.
“Ni kweli mwandishi, Kaka yangu amefariki dunia, wengine tuko poa,
ila mmoja wetu amaepata majeraha kidogo kichwani, amepelekwa Muhimbili (Hospitali
ya Taifa), kwa uchunguzi,” alisema.
Akizungumza kwa simanzi kubwa kwa njia ya simu jana asubuhi, Olilemba
alisema, hadi muda huo kifo cha nduguye kwake kilikuwa kama alikuwa akiota
ndoto, lakini ndio ukweli kwamba, Patrick amefariki dunia.
Baada ya hapo mwandishi wa habari hizi, alikwenda hadi Hospitali
ya Muhimbili
na kukuta umati wa watu-kila mmoja akiwa kwenye majonzi makubwa,
wakishindwa kuamini kifo hicho cha ghafla.
Kati ya watu waliokuwa wamefikia Hospitalini hapo wakati huo mwili
wa marehemu ukisubiri kufanyiwa uchunguzi zaidi, ni wachezaji wenzake wa Simba,
viongozi kadhaa na wanamuziki wa Bendi ya Akudo ambao walijikuta wakiangua
kilio.
Baadhi ya nyota waliofika Hospitalini kwa muda huo, ni Uhuru
Suleiman, Emmanuel Okwi, Haruna Moshi Boban, Derick Walulya (Simba) na Haruna
Niyonzima, nyota wa kimataifa wa Rwanda anayechezea Yanga na wanamuziki, Chiristian
Bella, Clary Boteku na Canal Top.
Akizungumzia msiba huo, Makamu Mwenyekiti wa Godfrey Kabulu
alisema mwili wa nyota huyo utaagwa leo katika viwanja vya TTC Chang’ombe, kuanzia saa 2:00
asubuhi kabla ya kusafirishwa kesho kwenda kwao Rwanda kwa mazishi.
Kaburu alisema, kifo cha Mafisango ni pigo kubwa kwa kikosi cha
Simba na nchi yake ya Rwanda iliyokuwa ikimtegemea kwani amefikwa na umauti
akiwa
ameitwa kwenye kikosi cha Amavubi.
“Kifo cha Mafisango ni pengo kubwa kwetu (Simba) kutokana na
umuhimu wake, lakini hatuna mengi zaidi kwani hatuna la kufanya mbele ya kazi
ya Mwenyezi Mungu, Mafisango amemaliza safari yake Duniani,” alisema.
Katika hatua nyingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limepokea
kwa masikitiko
kifo cha nyota huyo kilichoacha pengo na simanzi kubwa kwa familia
ya soka kutokana na moyo wake wa kujituma uwanjani.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho hilo, Boniface Wambura,
kifo cha Mafisango sio pigo tu kwa timu yake ya Simba na nchi ya Rwanda, bali
kwa soka ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Wambura alisema Mafisango amefikwa na umauti kipindi ambacho nchi
yake
ikihitaji mchango wake, akiwa kati ya nyota walioitwa kwenye
kikosi cha Amavubi kwa mechi za mchujo wa kuania tiketi ya Kombe la Dunia kwa
Kanda ya Afrika.
“TFF inatoa pole kwa familia ya Mafisango, klabu ya Simba,
Shirikisho la Mpira wa Miguu Rwanda (FERWAFA), tunawataka kuwa na subira na
uvumilivu katika kipindi hiki kigumu kwao,” alisema Wambura.
Mwisho
Manji atoa msharti
kurudi Yanga SC
Na Salum Mkandemba
ALIYEKUWA mfadhili wa Yanga Yusufu Manji,
ameibuka kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa migogoro ndani ya klabu hiyo na
kudai kuwa yupo tayari kurudi kuifadhili kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa
masharti.
Manji ameyasema hayo jana kupitia barua yake
aliyosambaza katika vyombo vya habari na kusema kuwa yuko tayari kufikiria
kushiriki kikamilifu, kurudi Yanga kwa mwaka mmoja kwa masharti makubwa kadhaa.
Sharti la kwanza ambalo amelitoa kwa uongozi wa
Yanga ni ikubalike kufanywa uhakiki wa mahesabu ya akaunti za Yanga ndani ya
siku 90 na wakaguzi wa hesabu wa kujitegemea kukagua hesabu za kipindi cha 2006
hadi 2012 kwa ajili ya fedha zilizopokelewa na klabu.
Pili kuanzia sasa na kuendelea akaunti za Yanga
zichapishwe katika magazeti siku 15 baada ya kumalizika kwa robo ya mwaka.
Katika sababu ya tatu, Manji ametaka kuwapo na
upigaji wa kura ya maoni ndani ya siku
60 na kuamua kama wanachama wa Yanga wanataka kuendesha kampuni ya Yanga
au la.
Sharti la nne, Yanga ifanye mabadiliko ya katiba
ndani ya siku 90 juu ya muundo wake wa uongozi kwa kukubali mojawapo ya mfumo
huu chini ya Katiba ya Yanga.
Katika barua hiyo Manji pia ameutaka uongozi kuidhinisha
mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa klabu kuchagua Makamu Mwenyekiti wake na
wafanyanye kampeni kwa pamoja kupitia tiketi moja, na tiketi yoyote ile itakayo
fanikiwa kushinda itaunda Kamati ya Utendaji na Kamati zote chini ya Kamati ya
Utendaji kama wanatakavyoona inafaa kwa muda wao wa miaka 4, ikiwa ni pamoja na
kuondoa au kuongeza Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kulingana na uamuzi wao.
Manji ambaye ni kipenzi cha Wanayanga, pia
ameupa masharti uongozi uliopo chini ya Mwenyekiti wake Lloyd Nchunga, wagombea
wa Kamati ya Utendaji wafanye kampeni na baadaye wajumbe 12 wachaguliwe kwa
muda wa mwaka wa nne.
Baada ya Kamati ya Utendaji ya kuchaguliwa, basi
ichague Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti kwa muda wa mwaka mmoja kutoka ndani ya
Kamati ya Utendaji na kila mwaka wao kupiga kura ya ama kumbakiza au
kumbadilisha Mwenyekiti na au Makamu Mwenyekiti kutoka ndani ya Kamati ya
Utendaji.
Sharti la mwisho ni Mkutano wa Wanachama uitwe
ndani ya siku 30, ili kujadili masuala yaliyopo hapo juu na kama kutakuwa na
makubaliano ya masharti yaliyowekwa hapo juu, basi na yeye rasmi atarudi kushiriki kikamilifu
Yanga kwa muda wa mwaka mmoja.
Uamuzi wa Manji kutaka kurejea Yanga kwa
masharti, unakuja kufuatia wito hivi karibuni wa kundi la wanachama vijana wa
klabu hiyo likiongozwa na Bakili Makele, kumtaka kurejesha ufadhili wake
kuinusuru klabu hiyo na hali mbaya kifedha chini ya uongozi wa Nchunga.
Mwisho
Nchunga ahofia
maisha yake Yanga
Na Salum Mkandemba
MWENYEKITI wa Yanga Lloyd Nchunga, amesema
kwa sasa anahofia usalama wa
uhai wake ndani ya klabu hiyo kutokana
na mvutano uliopo kati ya uongozi wake
na Baraza la
Wazee, wakimtaka aachie ngazi.
Kabla ya baraza hilo
chini ya Mwenyekiti wake, Dk. Jabir Katundu, kutoa tamko hilo ,
liliomba kukabidhiwa timu kuelekea mechi
ya mwisho ya Ligi Kuu dhidi ya Simba ya
Aprili 6, kwa hoja ya kuiepusha na aibu
ya kufungwa baada ya kuvuliwa ubingwa.
Akizungumza siku tatu kabla ya mechi
dhidi ya Simba ambayo iliisha kwa Yanga
kufungwa mabao 5-0, Katibu wa Baraza hilo , Ibrahim Akilimali,
alisema waliitaka
timu kutokana na uongozi wa Nchunga
kushindwa kuiendesha.
Wazee walifikia hatua hiyo baada ya
uongozi wa Nchunga kushindwa kuwalipa
wachezaji mishahara kwa miezi miwili,
hivyo kushindwa kucheza kwa ari, wakifungwa
na Toto Africa
na Kagera Sugar.
Kitendo cha
Yanga kupoteza pointi hizo sita na zile kutoka kwa Coastal Union ya Tanga kwa
kosa la kumchezesha Nadir Haroub ‘Cannavaro,’ kukaifanya Yanga ibaki nyuma ya
Simba na Azam kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara.
Licha ya wazee
kuitaka timu, uongozi wa Nchunga uligoma ukiwataka kwanza kuainisha vyanzo vya
fedha za kuendesha timu hiyo, kitendo ambacho kiliwakera wazee hao na kuamua
kujiweka kando kuelekea mechi dhidi ya Simba.
Kitendo cha
Yanga kufungwa, ndicho kikawapa nguvu zaidi wazee, wakimtaka
Nchunga aachie
ngazi, hoja ambayo iliungwa mkono na kundi la wanachama vijana
wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wao,
Bakili Makele.
Akiizungumzia hali hiyo jana katika
mahojiano na Radio One kupitia kipindi cha Kumepambazuka, Nchunga alisema kauli
ambazo zimekuwa zikitolewa na vinara wa harakati za kutaka uongozi wake
uong’oke, ni kitisho cha usalama wake, ingawa hajachukua hatua za kisheria.
“Kauli tata juu yangu zinazotolewa tangu
kuanza kwa harakati za kutaka niondoke madarakani, ni hatari kwa usalama wangu,
ingawa sijachukua hatua zozote za kisheria,” alisema.
Nchunga alisema kama
atapatwa na lolote baya la kudhuriwa au vinginevyo, serikali itakuwa inatambua
nani wa kuulizwa, kwani amekuwa akitishiwa maisha, ikiwamo kupitia vyombo vya
habari.
Kupitia kipindi hicho, Nchunga
aliendelea kushikilia msimamo wake akisema pamoja na yote hayo yanayofanywa
dhidi yake binafsi na uongozi wake, lakini yupo Yanga kisheria, hivyo hata
kuondoka, yapaswa iwe kisheria.
“Kama inatokea leo, napatwa na tukio
lolote baya la kudhuliwa au vinginevyo, ni wazi kuwa serikali inamtambua
anayepaswa kuwa kiini cha hilo .
Natishiwa maisha, tena kupitia vyombo vya habari,” alisema Nchunga na
kusisitiza:
“Nipo Yanga kisheria, kuondoka kwangu
pia kufuate sheria, si matakwa ya kundi fulani,” alisema Nchunga aliyeingia
madarakani Julai 18, 2010, akirithi kiti kutoka kwa Imani Madega, aliyekuwa
amemaliza muda wake kwa mujibu wa katiba.
Nchunga alisema ukimya wake wa kujibu
mashambulizi kwa kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahusika, ndio unauponza
uongozi wake, kwani serikali inamtambua mtuhumiwa namba moja kama
ikitokea akapata madhara.
Kuhusu kiini cha mvutano, Nchunga alisema
mfumo wa muda mrefu wa uendeshaji wa klabu hiyo ndio chimbuko la migogoro ya kila mara huku wazee nao wakiwa
sehemu ya tatizo hilo
kutokana na kutaka kuwa na sauti.
Alisema, ndiyo maana amekuwa mvumilivu
kiasi cha kuamua kuitisha mkutano na wazee Mei 20 kabla ya Mkutano Mkuu wa
Julai 15 na kusema, anashangazwa kusikia siku hiyo itakuwa ya kuung’oa uongozi
wake.
Zaidi ya hilo, Nchunga alionesha kushangazwa
kwake na wazee hao kwamba yeye hakuwa chaguo lao, akisema hiyo ni kutokana na
kupinga matakwa yao, lakini akisema ni kweli kama si ridhaa yao, asingeshinda.
Kuhusu madai ya wachezaji, Nchunga
alisema ni majungu, kwani wachezaji ambao wanadai ni wawili tu, Jerry Tegete na
Nurdin Bakar; tena kwa sababu maalumu. Kuhusu kipigo cha mabao 5-0, amesema si
pekee wa kubebeshwa mzigo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment