Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limeshangazwa na kitendo kilichofanywa na madaktari wanaofanya kazi chini ya usimamizi wa madaktari bingwa (interns), na kusema kuwa hatua waliochukua inaweza kuleta vurugu ndani ya nchi.
Madaktari wanaofanya kazi chini ya usimamizi wa madaktari bingwa (interns), ambao walisimamishwa wakati wa mgomo wa madaktari juzi walijitokeza na kuomba radhi kwa wananchi na serikali kwa kushiriki migomo na kusababisha madhara makubwa kwa baadhi ya wananchi.
Madaktari hao ambao walikusanya saini zaidi ya 200 kutoka kwa wenzao, walienda mbali zaidi na kuapa kwamba hawako tayari kushiriki tena kwa namna yoyote katika migomo inayoweka rehani maisha ya wananchi.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholaus Mgaya, alisema kuwa, hatua iliyochukuliwa na madaktari hao ni cha kushangaza kwa kuwa bado madai waliyokuwa wakihitaji yameshindwa kutekelezwa jambo linaloweza kuchangia kuwepo kwa vurugu.
Mgaya, alisema kuwa Tucta alielewi ni kitu gani kimewasibu madaktari hao hadi kufikia hatua ya kuomba radhi.
Alisema kuwa inawezekana madaktari hao sio wanachama wa vyama vya wafanyakazi hivyo wameshindwa kujua sheria za kuitisha kwa mgomo.
“Sasa inatupa mashaka juu ya mgomo wao…maana hawajapata walichogomea wanaanza kuomba radhi hapa ni lazima ‘system’ imefanyakazi yake na inawezekana kulikuwa na mamluki wengi katika mgomo ule,” alisema.
Katibu Mkuu huyo, alisema kuwa Tucta imejipanga kukutana na viongozi wa madaktari hao ili kuweza kuwaelewesha maana ya mgomo na kuacha kutoa matamko yasiyo kuwa na tija.
Alisema madaktari hao wakiingia katika vyama vya Wanyakazi wataweza kujua sheria za kuitisha mgomo na kuhakikisha wanasimamia na kupata kile walichokuwa wanakihitaji kuliko wanavyofanya sasa.

“Hawa waliotoa tamko hilo inaelekea hawapo katika chama cha wafanyakazi, hivyo wakiingia katika vyama wataacha kutoa matamko ya aina hiyo maana wanaonekana hawaelewi na wanajifunza,” alisema

Hata hivyo Mgaya alisema kuwa inaonyesha madaktari hao kama wametishwa na kulazimika kutoa tamko hilo.

“Hapa kuna jambo limefanyika kwa kuwa hata Dk Steven Ulimboka hatumsikii tena, lazima kuna kitu kinafanyika lakini hatua waliyoifanya watapata hasara zaidi kwani hawawezi kukutana tena na serikali …kwa kifupi wamekalia kuti kavu,” alisema

Mwisho

No comments:

Post a Comment