Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Afisa ‘feki’ usalama wa taifa adakwa


Afisa ‘feki’ usalama wa taifa adakwa
JESHI la polisi linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za utapeli na wizi huku mmoja akikutwa na kitambulisho cha usalama wa taifa.
Akizungumza na Tanzania Daima jana jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, alisema kuwa watu hao walikamatwa kutokana na juhudi zilizofanywa na jeshi la polisi.
Kamanda Wambura alisema kuwa watu hao walikamatwa juzi usiku katika maeneo ya Kawe ambapo walikutwa na kadi mbalimbali za benki zinazosadikiwa kuporwa katika matukio mbalimbali.
Alisema kuwa mbali na kadi za benki walikutwa na laini za M- Pesa, Tigo –Pesa na Airtel Money ambazo zinadaiwa kutumika katika kutapeli watu.
Alidai kuwa watu hao hutongoza kina dada na kuahidiana nao kukutana ambapo huwawekea dawa katika vinywaji na kisha huwalewesha na kuwapora kila kitu.
Alisema kuwa baada ya kuwalewesha wadada hao huwalazimisha kutaja namba za siri za kadi zao za benki na hutumia nafasi hiyo kwenda kukomba fedha yote.
Kamanda Wambura alisema kuwa mbali na kuwalewesha wamekuwa wakiwatumia kwa shughuli nyingine na hata kuwabaka.
“Hili ni kundi kubwa na tunahofu kuwataja majina hadharani kwa kuwa tutashindwa kuendelea na upelelezi lakini hawa ndiyo wanatusaidia kulibaini kundi hilo na inaonekana wamefanya vitendo vingi vya kitapeli na wizi,” alidai
Alisema kuwa wameghushi kitambulisho cha usalama wa taifa ili kupata urahisi wa kuwatongoza wanawake hao.
“Hiki kitambulisho ni cha kughushi maana inaonyesha wamekuwa wakikitumia kuwalaghai wakina dada na wamekuwa wakirubunika na kujikuta mikononi mwa vijana hao ambao huwafanyia mambo ya udhalilishaji,” alidai
Mwisho

No comments:

Post a Comment