MAKAMU
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ambaye ni mstaafu, Nicholus
Kuhanga amekiri kuwa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi wanaoanza vyuo vikuu
nchini ni tatizo, hivyo alishauri Tanzania kuingia kwenye mpango wa kuwakopesha
kwa kupitia benki.
Kuhanga
alisema hayo alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima kuhusu suluhu kwa
wanafunzi wanaohitaji mikopo ambao wamekidhi vigezo lakini hawakupata.
Alisema,
njia mojawapo ni kuingia kwenye mpango huo wa benki kama nchi za wengine ili
kuondoa mgongano uliojitokeza baina ya serikali na wanafunzi hao.
“Kwa
kutumia mfumo huu wa benki nafikiri kila mmoja ataweza kunufaika mkopo huo,
watakapomaliza watatumia vitambulisho vyao ili kuanza kuzirejesha,” alisema na
kuongeza kuwa wale ambao watakuwa hawana vigezo vya kupata mkopo benki, ndio
hao wasaidiwe na Bodi ya Mikopo Tanzania (HELBS).
Alisema
kuwa, serikali haina fedha ya kutosheleza kumlipa kila mhitaji, japo wazo la
kuanzisha bodi hiyo lilikuwa serikali isaidie kuongeza idadi ya wanaokwenda
vyuo vikuu kutoka katika familia za wasiojiweza.
Kwa
upande wake Naibu Makamu Mkuu wa UDSM, alisema bodi ina bajeti kwa idadi
fulani, hivyo wale ambao hawakupata sasa ni jukumu la wazazi, ndugu na jamii
kuwasaidia.
mwisho
No comments:
Post a Comment