Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

MARANDO: WAWEKEZAJI WAMEPEWA FEDHA ZETU






WAKATI Rais Jakaya Kikwete na Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, wakiwabeza Watanzania kuwa hawana uwezo wa kifedha kuwekeza katika utafiti wa gesi na mafuta, mwanasheria maarufu nchini, Mabere Marando, ametoboa siri za vyanzo vya fedha za wawekezaji wa nje wanaopigiwa debe na serikali.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya stendi ya Kibiti wilayani Rufiji juzi, Marando alisema wawekezaji wengi kutoka nje hawaji na fedha mifukoni, badala yake wanatumia mabenki ya hapa nchini kujipatia mitaji hiyo, jambo alilodai kuwa linaweza kufanywa na wawekezaji wazawa.
Marando ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Makamu Mwenyekiti wa chama Kanda ya Pwani, alisema serikali imeshindwa kuwasaidia wazawa kwa kuwachukulia dhamana ya kukopa mitaji mikubwa kama inavyofanywa na nchi nyingine.
Kwamba badala ya kuwawezesha imegeuka kuwasimanga na kuwabeza kuwa hawana uwezo wa kifedha wa kampuni zao kushiriki katika michakato hiyo ya kupewa vitalu vya utafiti wa gesi na mafuta. Alisema hali hiyo ni makusudi ya serikali ya CCM kuwazuia Watanzania kutumia fursa zilizopo na badala yake inakimbiza fursa hiyo kwa wageni.
“Niliposikia rais akitoa kuli hiyo niliumia sana lakini nikaja kutambua kuwa huyu mtu hakuwahi kupigika katika maisha ya tabu na wala hajawahi kufanya biashara kwa maana hao wageni aliokuwa nao juzi wengi wao wakiwa wanataka vitalu, mimi nimewaandalia nyaraka za kukopa katika mabenki yetu nchini,” alisema.
Marando aliongeza kuwa mmoja wa waombaji hao wa uwekezaji katika vitalu vya gesi, ameweka leseni ya kampuni yake kama dhamana katika moja ya benki hapa nchini ili aweze kupata mkopo, jambo aliloeleza kuwa linaweza kufanywa na Watanzania wengi wenye dhamana za kutosha.
Aliongeza kuwa sera ya CHADEMA ni kuwapa kipaumbele wazawa badala ya wageni katika kumiliki vyanzo vya rasilimali hali aliyoeleza kuwa ni tofauti na serikali ya CCM.
Marando alisisitiza kuwa makubaliano ya uwekezaji wa eneo lolote nchini unapaswa uanzie kwa mwekezaji kukubaliana na mmiliki wa eneo analotaka kuwekeza tofauti na ilivyo sasa kwa serikali kuamua bila kuwashirikisha wananchi.
Alitolea mifano uamuzi wa serikali kushindwa kuwashirikisha wananchi katika hatua za awali ni matokea ya migongano ya mara kwa mara baina ya wawekezaji na wananchi wa maeneo husika.http://www.freemedia.co.tz/images/blank.gif



No comments:

Post a Comment