Msajili wa vyama vya siasa,Jaji Mutungi amekataa agizo la Mwenyekiti wa
PAC,Zitto Kabwe la kumtaka kusitisha ruzuku kwa vyama vya siasa,
Zitto alitoa agizo hilo wiki iliyopita kufuatia madai yake kuwa hesabu
za vyama karibu vyote hazijakaguliwa kwa takribani miaka mine sasa.
Hata hivyo, agizo hili limezua tafrani kubwa ambapo karibu vyama vyote
vilivyotuhumiwa vimekana madai ya Zitto vikidai kuwa, hesabu zao zimekaguliwa
kwa mujibu wa sheria na hivyo, hakuna sababu ya kunyimwa ruzuku.
Mutungi amesema hatafanya hvyo mpaka hapo atakapofahamu ni sababu gani
iliyofanya mhusika wa kusimamia ukaguzi huo, ambaye ni Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu
wa Hesabu za Serikali(CAG) hakufanya hivyo.
No comments:
Post a Comment