Social Icons

NDOA YANGU, Ningejua!

NDOA YANGU, Ningejua!

Wassira, Lukuvi, Chikawe washambuliwa



RAIS Jakaya Kikwete amepongezwa kwa hatua ya kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani Ikulu na kuwa kitendo hicho ni pigo kwa baadhi ya mawaziri ambao wameifanya ikulu kuwa hatimiliki yao.

Akizungumza na Tanzania Daima jana Mwenyekiti wa kamati ya viongozi wa dini wa taaluma, maadili na haki za binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga, alisema kuwa kiongozi huyo ana nia njema lakini watendaji wake wamekuwa wakimpotosha.

Mwamalanga alisema kuwa hatua hiyo ya kuwa na majadiliano ya pamoja yameonyesha ujinga uliokuwa ukifanywa na baadhi ya watendaji ambao wamekuwa wakitoa kauli za kudhalilisha dhidi ya viongozi wa vyama vya upinzani juu ya kukutana na Rais Kikwete.

“Huwezi kuwa na hatimiliki ya Ikulu hili ni lazima Waziri William Lukuvi, Mathias Chikawe na Steven Wasira wakatambua…maana hatua ya Rais Kikwete kukutana na viongozi hao kimewadhalilisha wao,” alisema.

Kiongozi huyo alisema kuwa watendaji hao ndiyo waliokuwa wakipotosha suala hilo na kumlazimisha Rais Kikwete asaini haraka.

Alisema kuwa ni muhimu sasa Rais Kikwete akasimamia utekelezaji wa makubaliano hayo ili malengo yaliyowekwa yakaweza kufikiwa.

Mwamalanga alisema kuwa iwapo Rais Kikwete atayaacha makubaliano hayo na kuwaachia watendaji hao kuna uwezekano wa kutokea kwa mtafaruku mkubwa ndani ya nchi katika suala hilo.

Alisema kuwa kuna uwezekano wa kuwepo kwa baadhi ya vipengele kurejeshwa Bungeni pamoja na muswada huo kusainiwa lakini hilo halitafanya mchakato huo kushindwa kuendelea.

Mwisho

No comments:

Post a Comment